Home »
» RC SENYAMULE MAANDALIZI YA SENSA YAMEKAMILIKA ASILIMIA 98
RC SENYAMULE MAANDALIZI YA SENSA YAMEKAMILIKA ASILIMIA 98
Na.Kadala Komba Dodoma
MKUU wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule amesema ili kuhakikisha zoezi la sensa ya watu na makazi linalotarajiwa kufanyika Agosti 23,2022 linafanyika kwa ufasaha Mkoa wa dodoma umezindua namba maalumu ya simu ambayo kaya yoyote isipofikiwa na karani kuhesabiwa mwananchi atapiga namba hiyo bure.
Mwananchi atapiga simu kwa kupitia namba za bure ambazo ni 0800110083 na kueleza mtaa au kitongoji anapoishi na uongozi wa Mkoa utawasiliana na karani aliyepangiwa katika eneo hilo na kufika kuhesabu kaya husika.
Akizungumza na wandishi wa habari jijini Dodma leo Agosti 21,2022 Senyamule amesema maandalizi ya sensa yamekamilika kwa asilimia 98 ikiwemo mafunzo kwa makarani, vifaa vya sensa,usafiri na masuala ya kifedha kwa ajili ya kuwezesha zoezi la sensa kufanyika.
"Hadi sasa makarani wamesambaa Katika maeneo yao waliyopangiwa kwa ajili ya kujitambulisha kwa viongozi wa maeneo hayo kutambua eneo lake la kuhesabu watu katika eneo lake ambapo Mkoa wa dodoma una jumla ya makarani 10,353 ambao watafanya kazi ya kuhesabu Katika maeneo waliyopangiwa,"amesema Senyamule
Ameongeza kuwa"Serikali inawaomba wananchi wote kushiriki zoezi la sensa kuanzia siku ya jumanne kwa kuhakikisha wanashiriki kihesabiwa na wanahesabiwa mara moja tu na wanatakiwa kutambua kuwa ni kosa kisheria kukataa kushiriki zoezi hilo.
Senyamule amewataka wananchi kuandaa taarifa za kaya Ili kurahisisha zoezi la sensa ya watu na makazi ,ambapo taarifa hizo ni pamoja na umri wa wanakaya,hali ya ajira,Elimu,taarifa za Kilimo na mifugo namba za kitambulisho cha taifa (NIDA) na namba ya simu ya wanakaya.
Pa Senyamule amewataka makarani kuhesabu watu katika eneo lake alilopangiwa kwa ufasaha na kutunza siri za kaya alizohoji na kutambua kazi hiyo inafanyikia kwa maslahi ya taifa Katika kupanga mipango ya maendeleo.
"Nitumie fursa hii kuwa sisitiza wakuu wa wilaya wote wa Mkoa wa dodoma kwa kushirikiana na kamati za ulinzi na Usalama za wilaya na Wakurugenzi wa Halmashauri.
kuhakikisha wanasimamia zoezi hilo Ili lifanyike kwa mafanikio kama ilivyopangwa,"amesema.
Related Posts:
MHE. UMMY NDERIANANGA APONGEZWA KUWASAIDIA WATU WENYE ULEMAVU Na Mwandishi wetu-KilimanjaroBaadhi ya Watu Wenye Ulemavu Mkoa wa Kilimanjaro wamemshukuru Mbunge wa Viti Maalum kundi la Watu Wenye Ulemavu na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nde… Read More
TUME WATANGAZA NAFASI ZA KAZI DAFTARI LA WAPIGA KURA … Read More
RAIS SAMIA APONGEZWA MIRADI YA MAENDELEO KILIMANJARO Na Mwandishi wetu -KilimanjaroRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Dkt. Samia Suluhu Hassan, amepongezwa kwa juhudi kubwa anazozionesha za kuruhusu kuendelea ujenzi wa miradi mikubwa ya kimkakati kwa kutoa… Read More
“WAGONJWA WANAHITAJI FARAJA KUTOKA KWA WAUGUZI” MHE. NDERIANANGA Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga amewataka Viongozi wa Kata na Wahudumu wa afya ngazi ya jamii kushirikiana kuwatambua wagonjwa waliofichwa ndani na watu wenye ulemavu ili w… Read More
MBEGU BORA YA MTAMA TARISOR1 LIMA KIDOGO PATA ZAIDI WAKULIMA wa zao la mtama wameshauriwa kutumia mbegu ya mtama aina ya TARISOR1 kwa kuwa mtama huo hauliwi na ndege kama ilivyo kwa mtama mwingine.Mbegu ya mtama TARISOR1 ukomaa kwa siku 120. Nafasi za kupanda… Read More
0 Comments:
Post a Comment