Home »
» MTAKWIMU MKUU ASILIMIA 99.93 WAMEHESABIWA NCHI NZIMA
MTAKWIMU MKUU ASILIMIA 99.93 WAMEHESABIWA NCHI NZIMA
Na. Kadala Komba Dodoma
MTAKWIMU Mkuu wa Serikali Dk.Albina Chuwa amesema tangu kuanza kwa zoezi la Sensa ya Watu na Makazi Agosti 23 Mwaka huu Nchini kote hadi kufikia Leo kiwango Cha Kaya zilizohesabiwa imefikia asilimia 99.93na zimebaki asilimia 0.07 tutaendelea kuhesabu Hadi tarehe 5 Septemba 2022.
"Ambapo simu zilizotolewa zitatumika kuwafikia ambao hawajahesabiwa kwa kuwa utaratibu maalumu ulishaandaliwa wa namna ya kuzifikia Kaya hizo kupitia viongozi wa mitaa na vitongoji.
Dk Chuwa ameyaeleza hayo Leo Jijini Dodoma wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusiana na zoezi hilo ambalo linamalizika rasmi kesho.
Katika hatua nyingine amesema kuwa Sensa ya Majengo Hadi leo asubuhi tarehe 31Agosti, 2022 jumla ya majengo yaliyokwisha hesabiwa ni 6,351,927 Ambapo taarifa za umiliki,mahali yalipo na taarifa nyingine zinazoanisha katika Dodoso la majengo zimekusanywa.kwa makadirio ni kufikia Majengo Milioni 12.
Aidha Dk.Chuwa amesema kama mnavyofahamu ,Sensa kwa mara ya kwanza tangu tupate Uhuru mwaka 1961 imefanyika Sensa ya watu na makazi (Traditional Census) ya kidigitali ambayo imejumuisha Sensa ya Majengo na Sensa ya Anwani za Makazi katika mfumo wake wa utekelezaji .
"Alisema Ubunifu huu umeongeza ufanisi katika utekelezaji wa shughuli za Serikali ikiwa ni pamoja na kupunguza gharama ya kufanya mazoezi makubwa matatu ya kitaifa endapo yangefanyika katika kipindi tofauti.
MTAKWIMU Mkuu wa Serikali Dk.Albina Chuwa akizungumza na waandishi wa habari
Related Posts:
WAZAZI NA WALEZI WAKUMBUSHWA KUPELEKA WATOTO SHULE. Na Mwandishi Wetu- KilimanjaroWazazi na walezi nchini wametakiwa kuhakikisha watoto wao waliofikia umri wa kwenda shule wanapelekwa ili kupata elimu itakayowawezesha kuwa wataalam wa fani mbalimbali pamoj… Read More
SERIKALI IMETUTUPA,HAITUTAMBUI WANANCHI ZEPISA WATEMA NYONGO. Na Moreen Rojas,Dodoma.Wananchi wa kijiji cha ZEPISA Dodoma jiji wameilalamikia Serikali kwa kushindwa kuwatimizia huduma muhimu kama maji,umeme,miundombinu ya barabara pamoja na kituo cha afya.Pendo Wilson ambaye ni mw… Read More
*MHE.KAPINGA AZINDUA JUKWAA LA UZIDUAJI 2023* # Asema vyanzo vya umeme hasa Sekta ya Gesi ina uhusiano wa moja kwa moja na Sekta ya UziduajiNaibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga asema kuwa vyanzo vya kuzalisha umeme vina uhusiano wa moja kwa moja na Sekta ya… Read More
MCH.MARKO AMEWATIA MOYO WAKRISTO MSIKATE TAMAA Na. Kadala Komba ,DodomaWakiristo wametakiwa kuachana na hali ya kukata tamaa na kuishiwa nguvu hasa pale wanapokutana na changamoto mbalimbali katika maisha yao kwa maana tumaini lipo katika Mungu.Hayo yamebainishwa na… Read More
𝗧𝗨𝗞𝗢 𝗧𝗔𝗬𝗔𝗥𝗜 𝗞𝗨𝗦𝗛𝗜𝗥𝗜𝗞𝗜𝗔𝗡𝗔 𝗡𝗔 𝗦𝗘𝗞𝗧𝗔 𝗕𝗜𝗡𝗔𝗙𝗦𝗜: 𝗲-𝗚𝗔 Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), imeahidi kushirikiana na Benki ya NMB ili kuimarisha, kukuza na kuendeleza ujuzi na vipaji kwa vijana wa Kitanzania wabunifu na wale wanaosoma fani ya TEHAMA, katika Vyuo … Read More
0 Comments:
Post a Comment