Home »
» TAASISI YA KUMBUMBU YA MWALI NYERERE IMEKUJA NA MIKAKATI HII
TAASISI YA KUMBUMBU YA MWALI NYERERE IMEKUJA NA MIKAKATI HII
Na Sifa Lubasi Dodoma
TAASISI ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere Mkoa wa Dodoma imeweka mkakati wa kuanzisha kituo cha utamaduni kwa ajili ya kukusanya na kufanya shughuli za kiutamaduni
Taasisi hiyo kwa mkoa wa Dodoma inaongozwa na Mwenyekiti wa taasisi Mkoa Peter Mavunde na Katibu wa taasisi Mkoa ni Anamringi Macha ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara.
Àkizungumza wakati wa kikao juzi, Katibu wa Mkoa Anamringi Macha alisema miongoni mwa mikakati ni kuanzisha kituo cha utamaduni kwa ajili ya kukusanya na kufanya shughuli za kiutamaduni na hivyo kuwezesha kituo hicho kuwa na kitega uchumi.
Alitaja mikakati mingine ni kubuni, kuandaa na kutekeleza mipango mikakati ya kuinua mapato ya Taasisi ikiwemo ada ya uanachama, ada ya kila mwezi na maandiko ya mradi ya muda mrefu na mfupi.
Katika hatua nyingine, wajumbe wametumia nafasi hiyo kumpongeza Anamringi Macha aliyeteuliwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa CCM bara na kumtakia utekelezaji mwema wa majukumu aliyokabidhiwa na chama tawala
Katika kikao hicho wajumbe pia walipokea taarifa kutoka makao makuu ya taasisi ya kumteua Peter Mavunde kuwa Makamu Mwenyekiti wa Taasisi Taifa, huku Rehema Omary Hamis akichaguliwa na wajumbe hao kuwa mtunza hazina wa Mkoa.
mwisho.
Related Posts:
WALIOITWA KWENYE USAILI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA BAHI PART 1 … Read More
MHE. UMMY NDERIANANGA APONGEZWA KUWASAIDIA WATU WENYE ULEMAVU Na Mwandishi wetu-KilimanjaroBaadhi ya Watu Wenye Ulemavu Mkoa wa Kilimanjaro wamemshukuru Mbunge wa Viti Maalum kundi la Watu Wenye Ulemavu na Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nde… Read More
INEC, VYAMA VYA SIASA KUANDAA KANUNI ZA MAADILI YA UCHAGUZI Na Mwandishi wetu- Dodoma Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga amesema, Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi kwa kushauriana na vyama vyote vya siasa itaandaa… Read More
Naibu Waziri Ummy, Apokea jedwali la uchambuzi la Sheria Ndogo Na Mwandishi wetu- DODOMANaibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Ummy Nderiananga amepokea Jendwali la Uchambuzi la Sheria Ndogo za Mwaka 2024 katika Mkutano wa Kumi na Tano, Kikao cha sita cha Bunge … Read More
TUME WATANGAZA NAFASI ZA KAZI DAFTARI LA WAPIGA KURA … Read More
0 Comments:
Post a Comment