Home »
» FAIDA FUND YAPATA MAFANIKIO YA MAUZO HAWAMU YA KWANZA
FAIDA FUND YAPATA MAFANIKIO YA MAUZO HAWAMU YA KWANZA
Na. Johndickson Gaudin Dodoma
Mfuko wa Uwekezaji wa pamoja FAIDA FUND umefanikiwa kuwa Mfuko wa kwanza wa aina yake kupata mafanikio makubwa katika kipindi cha mauzo ya awali ikilinganishwa na lengo lililowekwa la kuanzishwa kwake.
Hayo yamebainishwa leo Februari 9,2023, Jijini Dodoma na Mkurugenzi Mtendaji wa Watumishi Housing Investiments (WHI), Dkt. Fred Msemwa mbele ya waandishi wa habari wakati akielezea utekelezaji wa majukumu ya Watumishi Housing Investiments katika kipindi cha Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.
Dkt. Msemwa amesema Mfuko huo umeyalenga makundi yote ya kijamii na lengo lake likiwa ni kuwawezesha wananchi kiuchumi kupitia uwekezaji wa pamoja wakiwemo watoto, wakulima, wavuvi, watumishi wa umma, wafanyakazi, makampuni na taasisi.“Faida Fund imenzishwa chini ya sheria ya masoko ya Mitaji na dhamana sura 79 ya sheria za Tanzania, Mfuko huu unasimamiwa na mamlaka ya masoko na dhamana (Capital Market and Securities Authority - CMSA) ambaye ndiye mdhibiti wa Sekta,”
amesema.
Amesema mfuko huo umekuja sokoni kuongeza nguvu na kuchochea tabia ya kuwekeza ukiwa na lengo kuwawezesha watanzania kiuchumi kwa kukuza mitaji yao.“Mwekezaji anaweza kufungua akaunti ya uwekezaji kwa kutumia menyu kuu ya serikali ya *152*00# au kwa kutumia WekezaWHI App ambayo inapitikana kwenye simu janja au kwa kutumia mfumo wa FAS (Fund Administration System) ambao umebuniwa na Mamlaka ya serikali Mtandao,”amesema.Aidha ameongeza kuwa tangu kuanzishwa kwake WHI imejenga jumla ya nyumba 983 katika maeneo mbalimbali ambazo zimeuzwa kwa watumishi wa umma na wanachama wa mifuko ya hifadhi ya jamii.Vilevile amesema Watumishi Housing Investiments imeendelea kuwauzia nyumba kwa mkopo nafuu watumishi wa umma ambao walikuwa hawawezi kununua nyumba kwa mkopo kutoka taasisi zingine katika soko.“Hii imewanufaisha watumishi haswa kanda ya kati na chini wakiwemo wauguzi na watumishi wa manispaa,
”amesema.Watumishi Housing Investment (WHI) ni taasisi ya umma iliyo chini ya Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora (OR-MUUUB), iliyoanzishwa mwaka 2014 kupitia mifuko ya Pensheni kwa watumishi wa umma (PSSSF), Mfuko wa hifadhi ya Jamii (NSSF), shirika la Nyumba la Tatumishi wa Umma na Utawala Bora (OR-MUUUB), iliyoanzishwa mwaka 2014 kupitia mifuko ya Pensheni kwa watumishi wa umma (PSSSF), Mfuko wa hifadhi ya Jamii (NSSF), shirika la Nyumba la Taifa na Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF).
Mkurugenzi Mtendaji wa Watumishi Housing Investiments (WHI), Dkt. Fred Msemwa mbele ya waandishi wa habari wakati akielezea utekelezaji wa majukumu ya Watumishi Housing Investiments
Related Posts:
UBORA WA HUDUMA ZA AFYA UNACHANGIWA NA WAKUNGA NA WAUGUZI.Na Moreen Rojas,Dodoma.Naibu Waziri wa Afya Dkt. Godwin Mollel amesema asilimia 60 ya watumishi katika sekta ya afya nchini wanatoka kada za uuguzi na ukunga hivyo kuchangia ubora wa huduma zinazotolewa katika Hos… Read More
UKIMWI,KIFUA KIKUU NA MALARIA MBIONI KUTOKOMEZWA. Na Moreen Rojas,Dodoma.Katibu Mkuu Wizara ya Afya,DK.John Jingu amezindua mradi wa mzunguko wa saba wa Mfuko wa Dunia (Global Fund Circle7)ambao utatekelezwa kwa muda wa miaka mitatu kuanzia sasa kwaai… Read More
TUENDELEE KUUNGANA KUKABILIANA NA MAAFA NCHINI” MKURUGENZI MSAIDIZI JANE NA. MWANDISHI WETUMkurugenzi Msaidizi Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Bi. Jane Kikunya amesema Serikali itaendelea kutoa ushirikia… Read More
*Waziri Nape Afanya Mazungumzo na Balozi wa Finland Tanzania*Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Moses Nnauye (Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Finland nchini Tanzania Mhe. Theresa Zitting Ofisini kwake jijini Dar es Salaam aliyeambatana na… Read More
UNDP YAZINDUA WAZO LA KIBUNIFU LA MATUMIZI BORA YA NISHATI NCHINI. Na Moreen Rojas,Dodoma.Shirika la Maendeleo la Kimataifa UNDP limezindua wazo la kibunifu la matumizi bora ya Nishati nchini.Akizungumza na vyombo vya habari Machi 15,2024 jijini Dodoma Mtaalamu mshauri wa Shirika hilo … Read More
0 Comments:
Post a Comment