Home »
» DHAMANI YA MAZAO CHINI YA PANDA KWA WASTANI WA 12%KWA MWAKA 2020/2021
DHAMANI YA MAZAO CHINI YA PANDA KWA WASTANI WA 12%KWA MWAKA 2020/2021
Na Johndickson Gaudin.
Bodi ya usimamizi wa stakabadhi imefanikiwa kuongeza bei ya mazao Mafanikio yaliyopatikana baada ya kuanzishwa kwa Mfumo wa Stakabadhi za Ghala ikiwa nipamoja kuongeza mapato ya wakulima na mapato ya serikali kwa wastani wa 200%huku ikiongeza kukuza huduma za fedha vijijini,kufanikisha uanzishaji wa Soko la Bidhaa Tanzania.
Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya usimamizi wa stakabadhi za ghala (WRRB),Asangye Bangu wakati wa mkutano na waandishi wa habari Leo februari 15,2023 ambapo amesema Baada ya kuanzishwa kwa Mfumo huo mwenendo wa bei na ushalishaji ulibadilika na kuanza kuwa na mwenendo chanya.
Aidha Mtendaji huyo amesema kwa upande wa uzalishaji, tokea kuanzishwa kwa Mfumo 2007/08 hadi 2020/21 ukuaji wa uzalishaji umekuwa ukiongezeka kwa wastani wa 12% kwa mwaka ukilinganisha na ukuaji wa 2% kwa mwaka kabla ya kuanzishwa kwa Mfumo waStakabadhi za Ghala.
"Mwaka 2021, Bodi imewezesha kuanza kutumika kwa Mfumo mkoa wa Songwe katika zao la Ufuta na Morogoro katika zao la Kakao licha ya upinzani mkubwa uliokuwa ukiletwa na wanafaika wa mifumo holela katika maeneo hayo.
"Mkoa wa Morogoro kwa mara ya kwanza wakulima waliuza kakao yao kupitia Mfumo wa Stakabadhi za Ghala na kufanikiwa kupata bei wastani wa Shilingi 4,892.50 ongezeko hili la bei lilikuwa ni la wastani wa asilimia 244.6 kutokea wastani wa Shilingi 2,000.00 bei waliyokuwa wakipata kupitia mifumo holela.",amesema.
Kwaupande mwingine mkurugenzi huyo ametoa wito kwa wakulima wa kahawa mkoa wa Kagera kuhakikisha wanakuwa wazapendo katika kuuza mazao kwakuzingatua na kufata utaratibu ili kuweza kuuza zao Hilo kwa bei elekezi.
Pia amewataka wanaoendesha na kusimamia maghala mikoa yote nchini kuhakikisha Wana mfumo wa CCTV camera ili kuwezesha kuona kuona kinachoendelea kwenye maghala hayo ili kuhakikisha wanafata Sheria zinazo waongoza kama taasisi.
Related Posts:
HATUKUBALIANI NA SHERIA YA WENZA WA VIONGOZI KULIPWA MAFAO "CHADEMA". Na Moreen Rojas,DodomaCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepinga kitendo cha Bunge kupitisha sheria ya wenza wa viongozi kulipwa mafao huku kikishauri kufanyiwa kwa marejeo ya sheria ya Kikokotoo ambacho kime… Read More
SERIKALI IMETIA SAINI YA MKATABA WA UPEMBUZI YAKINIFU Na Moreen Rojas,DodomaSerikali imetia saini ya mkataba wa upembuzi yakinifu na ununuzi wa meli za uvuvi wa bahari kuu na ujenzi wa viwanda viwili vya kuchakata samaki(kilwa na fungurefu)kupitia programu ya kuendel… Read More
TENGENEZENI HISTORIA NZURI YA CHUO CHA VETA BAHI-RC SENYAMULE Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amewataka uongozi wa Wilaya na Chuo cha Ufundi stadi VETA Bahi kuhakikisha wanatengeneza historia nzuri ya chuo hicho ili kilete matokeo chanya na kiwanufaishe watu mbalimb… Read More
SERIKALI IMEOMBWA KUPUNGUZA BEI YA NISHATI YA GESI YA KUPIKIA.Na Moreen Rojas,DodomaMwenyekiti Taifa wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mary Chatanda ameiomba Serikali kupunguza bei ya Nishati ya gesi ili wanawake Waweze kuachana na Matumizi ya kuni na mkaa kwenye shughuli za mapishi.M… Read More
PROGRAMU YA AFDP YALETA MATOKEO CHANYA SEKTA YA KILIMO UVUVI. Na. MWANDISHI WETUNaibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga amesema Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) inalengo la uzalishaji endelevu wa kibiashara na wenye kuzingatia … Read More
0 Comments:
Post a Comment