Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amekemea Vikali kuhusu upotoshaji mbalimbali unaosambaa kwenye mtandao ya kijamii kuhusu Jeshi la kujenga Taifa na kuwahakikishia Watanzania kuwa JKT ni mahali sahihi na muhimu kwa vijana kuongeza tija katika Taifa kwa ujumla.
Kauli hiyo ameitoa leo Septemba 13,2023 wakati akifunga mafunzo ya 19 kwa mujibu wa Sheria Operesheni ya miaka 60 ya Jeshi la Kujenga Taifa, katika viwanja vya 834 KJ Makutupora Jijini Dodoma.
Amesema lengo kuu la vijana kuhudhuria mafunzo hayo ya mujibu wa Sheria ni kuwajengea Uzalendo, Moyo wa Kupenda kazi, kuwapa mbinu za kujitegemea, kujenga umoja na mshikamano utakao imarisha umoja wa kitaifa ili kuwa na Taifa bora lenye ustawi mzuri na viongozi bora wenye fikra chanya kwa Taifa .
"Nimefurahishwa na tamko lenu mlilolitoa leo juu ya upotoshaji mbalimbali juu ya Jeshi la Kujenga Taifa, Nami nawahakikishia Watanzania JKT ni mahali sahihi na muhimu kwa vijana wetu ili kuongeza tija ya utaifa wetu, hivyo mtoto akipata nafasi ya kujiunga na JKT ni fursa nzuri na aitumie" amesisita Senyamule
Katika hatua nyingine, Mhe. Senyamule amewaasa vijana wahitimu hao kuwa na matumizi bora ya mitandao ya kijamii kwa kupata elimu na kufanya biashara za njia ya mtandao.
"Napenda kuwasihi sana mkaitumie mitandao kwa ajili ya kujielimisha na siyo kutumia kuangalia mambo yasiyofaa ambayo ni kinyume na maadili yetu hivyo kuchangia mmomonyoko wa maadili
"Amesisitiza Senyamule
Aidha, Mkuu wa Mkoa huyo ametumia jukwaa hilo kuwaasa wananchi wanaochoma moto ovyo katika eneo la Kikosi ambalo pia ni eneo oevu la bonde la Mzakwe ambacho ndicho chanzo kikuu cha maji kwa Mkoa wa Dodoma kuhakikisha wanatunza mazingira yake.
"Wananchi tunaoishi maeneo ya kuzunguka bonde tafadhali sana tutunze maeneo haya ili tuweze kuwa na uhakika wa maji kwani maji ni Uhai, yeyote atakaye kutwa anafanya shughuli ambazo zinachangia kuharibu mazingira kama uchomaji mkaa, kukata miti na Kilimo atachukuliwa hatua za sheria "amehimiza Senyamule
Kwa Upande Wake, Kaimu Kamanda Kikosi Meja James Andrew Macheta amesema wahitimu hao wamefanikiwa kujifunza Ukakamavu, Utii, Ujasiri, Stadi za Maisha, Ujasiriamali pamoja na ulinzi wa Taifa sambamba na kufanya kazi bila kuchoka sehemu yeyote hivyo wako tayari kutumika kama walinzi sehemu yeyote watakapo hitajika .
Vilevile, amewahasa vijana hao kuwa mabalozi wazuri kwa yote waliyojifunza kwa muda wa miezi mitatu kwa kuwa Wachapakazi na Kutekeleza kwa vitendo yote waliyofunzwa .
Home »
» JKT NI MAHALI SAHIHI NA MUHIMU KWA VIJANA-MHE SENYAMULE
JKT NI MAHALI SAHIHI NA MUHIMU KWA VIJANA-MHE SENYAMULE
Related Posts:
MATUKIO YA PICHA ZA MAADHIISHO YA MIAKA 25th YA HUDUMA YA MAENDELEO YA MTOTO NA KIJANA TANZANIA KWA MAKANISA YA KLASTA YA DODOMA MAGHARIBI– 26 APRILI 2024 Na.Kadala Komba BahiPICHA WATOTO WAKIFANYA MAANDAMANO MAENEO MBALIMBALI HALMASHAURI YA WILAYA YA BAHI Mwezeshaji wa Ushirika wenza kutoka shirika la Compassion International Tanzania Ndg. PF Maximina Goa Alisema Compass… Read More
UKIMWI,KIFUA KIKUU NA MALARIA MBIONI KUTOKOMEZWA. Na Moreen Rojas,Dodoma.Katibu Mkuu Wizara ya Afya,DK.John Jingu amezindua mradi wa mzunguko wa saba wa Mfuko wa Dunia (Global Fund Circle7)ambao utatekelezwa kwa muda wa miaka mitatu kuanzia sasa kwaai… Read More
*Waziri Nape Afanya Mazungumzo na Balozi wa Finland Tanzania*Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Moses Nnauye (Mb.) amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Finland nchini Tanzania Mhe. Theresa Zitting Ofisini kwake jijini Dar es Salaam aliyeambatana na… Read More
TANGAZO LA NAFASI YA KAZI - RUWASA, NYASA Fursa hii … Read More
WAKULIMA ZAIDI YA 400 WAMEPATIWA MAFUNZO JINSI YA KUTUMIA TEKNOLOJIA ZA KISASA ZA KILIMO Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE … Read More
0 Comments:
Post a Comment