Wito umetolewa kwa watendaji wa Tarafa na Kata za Mkoa wa Dodoma kuonesha thamani ya vyeti vyao vya Elimu kwenye utendaji wa kazi kwenye Tarafa na Kata zao kwani wao ndio wanatarajiwa kuiletea Serikali heshima kwa wananchi wake kwa. Hayo yamebainishwa leo Novemba 20, 2023 na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya siku mbili kwa watendaji hao yanayofanyika kwenye ukumbi wa Roma Complex Jijini Dodoma.
Mhe. Senyamule amesema watendaji wa Kata wanapaswa kufuata Sheria na kanuni za kiutendaji ili kuwapunguzia mzigo wa kero wananchi wa chini na sio kusubiri viongozi wa juu kufika kwenye maeneo yao kutatua kero.
"Serikali imeekeleza kila mtendaji asikilize kero na kuzitatua. Kazi kubwa ya mtendaji ni kuonesha njia kwenye Tarafa yako kwani changamoto kubwa iliyopo hapa ni mabadiliko bado ni madogo kulingana na matarajio ya Serikali. Mumewekwa pale kulinda heshima ya Serikali kwa kazi, maneno na matendo yenu. Jambo hili halifanyiki kwa uthabiti wa kutosha ndio maana munapewa mafunzo haya ili kuwakumbusha Sheria na kanuni mpya ili kuongeza maarifa kwa watumishi waweze kumudu majukumu yao" amesema Mhe. Senyamule.
Awali akimkaribisha mgeni rasmi, Mkurungenzi wa TAMISEMI Bi. Angelista Kihanga, amesema kuwa, mafunzo haya yamepewa umuhimu wa hali ya juu kwani yalianza awamu ya kwanza kwenye Mkoa wa Mbeya na Mikoa ya Magharibi na Sasa yanafanyika kwenye Mikoa ya Kanda ya kati kwa kuhusisha Maafisa Tarafa na Kata kwani ndio watekelezaji wa sera za nchi kwa wananchi.
Mafunzo kwa Maafisa wa Tarafa na Kata yaliyoandaliwa na Wizara ya TAMISEMI, yanagusia mada mbalimbali zikiwemo mwongozo wa ushughulikiaji malalamiko ya wananchi katika utumishi wa umma na huduma kwa wateja, ununuzi wa umma, nafasi ya Afisa Tarafa na Mtendaji wa Kata katika mafanikio ya Serikali, kanuni za maadili ya utendaji katika utumishi wa umma na Sera na Sheria za uendeshaji wa Serikali za Mitaa.
Home »
» WATENDAJI WA TARAFA NA KATA WATAKIWA KUONESHA ELIMU ZAO KWA VITENDO
WATENDAJI WA TARAFA NA KATA WATAKIWA KUONESHA ELIMU ZAO KWA VITENDO
Related Posts:
WATU 12 WAMEPOTEZA MAISHA KWA AJALI DODOMADodoma WATU 12 wamepoteza maisha baada ya basi a Frester lililokuwa likitokea Bukoba kwenda Dar es salaam kugongana uso kwa uso na Lori la Texas majira usiku wa kuamkia leo. Ajali hiyo imetokea eneo Kiiji Cha Silwa wilaya… Read More
NSSF IMEJIPANGA KUANZA KUTOA MAFAO KWA SEKTA ISIYO RASMI Na. Kadala Komba Dodoma. Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii(NSSF)umewataka wafanyakazi wa sekta isiyo rasmi kujiunga na mfuko huo kwa kupeleka michango yao na hatimaye kuwa kwenye mfumo wa mafao hali itakayosaidia kupun… Read More
DK.SWEKE: BAHARI KUU IPO SALAMA TUNATUMIA NDEGE KUFANYA DORIA Na. Kadala Komba Dodoma. MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi na Bahari Kuu Dkt.Emmanuel Andrew Sweke,ameeleza kuwa katika kulinda usalama wa bahari kuu wameweka mifumo ya kulinda usalama ikiwa ni pamoja na kutum… Read More
UTEUZI: EPHRAIM BALOZI MAFURU ATEULIWA KUWA MTENDAJI MKUU AICC … Read More
PROF.MKENDA :BADO UCHUNGUZI UNAENDELEA KWA WANAFUNZI NA WASIMAMIZI WA MITIHANI KIDATO NNE MWAKA 2022 .Na. Mwandishi wetu Dodoma SERIKALI kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, imesema imedhamiria kukomesha vitendo vya wizi wa mitihani huku ikiridhishwa na uamuzi wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) kwa wanafunz… Read More
0 Comments:
Post a Comment