Kamati ya siasa ya Mkoa wa Dodoma ikiongozwa na Katibu Wa Itikadi na uenezi (NEC ) Mkoa wa Dodoma Bw.Jawadu Mohammed imewapongeza wasimamizi wa miradi inayotekelezwa Katika Halmashauri ya Wilaya ya Chemba ikiwemo Miradi ya Shule na Hospitali kwa kuzingatia ubora na ufanisi unaotakiwa.
Akizungumza na baadhi ya viongozi walioshiriki katika ziara ya ukaguzi wa Miradi hiyo Bw. Mohammed amewataka watumishi wa Umma kuitangaza na kuwa Mabalozi Wazuri wa Miradi inayotekelezwa na Serikali ya awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Amesema "ni lazima tuwe na watu makini wa kufuatilia miradi inayoletwa na Rais wetu ili wananchi wasiwe na changamoto katika kupata huduma na ndio maana zimejengwa shule na Hospitali ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma nzuri na zinazostahili.
“Serikali ipo imara na imedhamiria kuhakikisha wananchi wanapata huduma za umeme, maji, mabweni, madarasa na majengo yote yanakua kwenye ubora na uimara wa Hali ya juu.Ni lazima miundombinu zote zikamilike kwa wakati kama mikataba inavyotaka hatufikirii kuona miradi inavuka muda wake wa utekelezaji,” Amesema Bw. Mohamed.
Pia Bw. Mohamed amesisitiza suala la upandaji Miti kwa Kila mradi ili kuhakikisha mazingira yanakuwa bora na imara hivyo kudumisha Sera ya Serikali ya Mkoa ya "Kijanisha Dodoma".
Kamati hiyo ilipata fursa ya kutembelea mradi wa Barabara kwa kiwango cha lami uliogharimu Kiasi cha Shilingi Milioni 599, ujenzi wa kituo cha afya Farkwa uliopokea kiasi cha Shilingi Milioni 500, Ujenzi wa Shule ya Msingi na awali Sankwaleto uliopokea kiasi cha shilingi Milioni 396, ujenzi wa Zahanati ya Sankwaleto ambao umepokea kiasi cha Shilingi Milioni 97, na ujenzi wa Mradi wa maji Babayu uliopokea kiasi cha shilingi Milioni434.
Ukaguzi wa Miradi mbalimbali unaofanywa na Kamati hiyo chini ya Mwenyekiti wa Kamati Bw. Mohhamed ni muendelezo wa ziara ya kikazi wanayoifanya katika halmashauri mbalimbali za Mkoa wa Dodoma.
Home »
» "TUMERIDHISHWA NA UTEKELEZAJI NA UBORA WA MIRADI YA CHEMBA " -JAWADU
"TUMERIDHISHWA NA UTEKELEZAJI NA UBORA WA MIRADI YA CHEMBA " -JAWADU
Related Posts:
WADAU WA MAENDELEO WAHIMIZWA KUCHANGIA VIFAA VYA MISAADA YA KIBINADAMU WAKATI WA MAAFA. Na Mwandishi wetu- Kilimanjaro Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga amewahimiza wadau wa maendeleo na watu binafsi kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kuchangia vifaa vya mi… Read More
SERIKALI YAOMBA VIONGOZI WA DINI KUKEMEA MATUMIZI YA DAWA ZA KULEVYA NA MWANDISHI WETUSerikali imetoa rai kwa viongozi wa dini kuendelea kuhimiza jamii kuepuka uraibu wa matumizi ya dawa za kulevya na kujenga uelewa kuhusu madhara ya madawa ya kulevya.Hayo yamesemwa na Naibu Wa… Read More
SERIKALI INAENDELEA KUWEKEZA KWA WATAALAMU WA NDANI WA MIFUMONa WAF - DSMKatibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe amesema kuwa, Serikali itaendelea kuwekeza kwa Wataalamu wa ndani wa mifumo ili kuhakikisha miradi yote inayoanzishwa na Wafadhili inaendelea kusimama siku Wafad… Read More
MCHUNGAJI AWATAKA WAGONJWA WANAONGUDULIKA NA TATIZO LA AFYA AYA AKILI WAPELEKWE HOSPITALI BADALA YA KWA WAGANGA WAKIENYEJI.Na Peter Mkwavila CHAMWINO. ASKOFU wa kanisa la Pentecostal Holiness Association Mission Tanzania PHAM (T) Kanda ya Kati Brayson Msanjila,amewashauri familia zinazogundulika kuwa na wagonjwa wa afya ya akili waac… Read More
WAZIRI PINDI CHANA AZINDUA BODI YA WAKURUGENZI TAWAWaziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana leo tarehe 12 Oktoba, 2022 amezindua Bodi ya Wakurugenzi ya TAWA aliyoiteua hivi Karibuni.Akizungumza katika hafla ya Uzinduzi iliyofanyika Makao Makuu ya TAWA Mk… Read More
0 Comments:
Post a Comment