Na WMJJWM, Dodoma
Serikali kupitia Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum imekubaliana na Kamisheni ya Uingereza kushirikiana ili kuimarisha usawa wa kijinsia nchini.
Hayo yamebainika wakati wa kikao cha Wizara na Kamisheni hiyo kilichofanyika jijini Dodoma Juni 7, 2023, kwa lengo la kutambulisha Programu na mkakati mpya wa kusaidia wanawake na wasichana kufikia ndoto zao (International Women and Girls strategy) utakaotekelezwa kati ya mwaka 2023 hadi 2030.
Akizungumza wakati wa kikao hicho, Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Dorothy Gwajima, amesema, lengo la Serikali ni kuhakikisha elimu ya usawa wa kijinsia inatolewa kuanzia ngazi ya malezi ya awali huku akiwaomba wadau hao kuongeza ushirikiano kwenye maeneo hayo.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Maendeleo wa Kamisheni ya Uingereza Nchini Kemi William, amebainisha kuwa, Kamisheni ipo tayari kuunga mkono jitihada za Serikali kupitia Programu za Elimu hasa mradi wa Shule Bora unaotekelezwa na Wizara ya Elimu kwa kuzingatia na kuhusisha makundi yote ndani ya jamii.
Katika hatua nyingine, Mkurugenzi huyo amekutana na Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu ambapo wamejadili ushirikiano bora wa kimaendeleo kwa lengo la kuwalinda Watoto na kuwawezesha wanawake na katika suala zima la utoaji wa elimu ya Afya ya uzazi kwa Wanawake na Wanaume ndani ya jamii.
Wakati wa Ziara hiyo, Kemi alifuatana na Wataalamu Waandamizi wa Elimu kutoka Kamisheni hiyo, Colin Bangay na John Lusingu.
MWISHO
Home »
» TANZANIA, UINGEREZA KUIMARISHA USAWA WA KIJINSIA
TANZANIA, UINGEREZA KUIMARISHA USAWA WA KIJINSIA
Related Posts:
KATAMBI- MFUKO WA MAENDELEO YA VIJANA UMEANZA KUTOA MIKOPO KWA KIJANA MMOJA MMOJA.Na Mwandishi wetu- Dodoma.Naibu Waziri- Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu Mhe. Patrobas Katambi amesema kuwa serikali imeendelea kufanya jitihada za kuweka mazingira wezeshi kwa vijana kuweza k… Read More
DUWASA KUMALIZA CHANGAMOTO YA MAJI NZUGUNINa. Mwandishi wetu Dodoma. KATIKA kukabiliana na suala la upungufu wa maji katika Jiji la Dodoma, Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dodoma (DUWASA) inaendelea na uchimbaji wa visima pembezoni wa mji ili … Read More
*DKT. KIRUSWA AIAGIZA GST NA STAMICO KUFANYA TAFITI ZA MADINI MUFINDI NA KILOMBERO* Na. Mwandishi wetu Dodoma Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa ameiagiza Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) pamoja na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kufanya tafiti za madin… Read More
WAZIRI MKUU ATOA MAAGIZO KWA NIDA KUONGEZA KASI UZALISHAJI WA VITAMBULISHONa Moreen Rojas DodomaMamlaka inayoshughulika na utoaji wa vitambulisho vya Taifa NIDA wametakiwa kuongeza kasi ya uzalishaji wa vitambulisho vya Utaifa ili kumsaidia mwananchi kupata wepesi wa kutambulika anapokuwa … Read More
CHANZO KIKUBWA CHA NDOA NYINGI KUVUNJIKA NI HIKI.Mwanzilishi na mwasisi wa kwanza wa Ndoa ni Mungu,Mungu alipomuumba Adam alimpa kazi 2 kubwa kulima bustani na kuitunza,pia akampa kazi ya kuwapa wanyama wote majina.Baada ya yote hayo Mungu alimwangal… Read More
0 Comments:
Post a Comment