Na Moreen Rojas,
Dodoma.
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu ametoa wito kwa madaktari bigwa upasuaji kufanya kazi mikoa yote na kuhakikisha wanazalisha wataalamu wazuri kwani kuna uhaba wa madaktari bigwa wa upasuaji nchini.
Waziri Ummy ameyasema hayo wakati wa mkutano wa mwaka na kongamano la kisayansi linalohusisha chama cha madaktari wa upasuaji Tanzania lililofanyika St.Gasper Hotel jijini Dodoma.
Aidha Waziri Ummy amesema kuwa wakati umefika wa madaktari kupangiwa vituo vya chini vya afya huku akihimiza kuwa hospitali kubwa za rufaa zisiwe sehemu za kuanzia ajira.
"Ningependa kuwashauri na kuwahimiza madaktari bigwa wa upasuaji kuanzia chini kabisa na sio kukimbilia hospitali za rufaa kwani huku chini ndio tuna wananchi wenye uhitaji zaidi kwani tumeshuhudia baada ya wananchi kukosa huduma hizi ndipo huamua kwenda hospitali za rufaa hivyo ningewaomba muanzie huku chini na sisi kama serikali tupo tayari kutoa ushirikiano pale mnapotuhitaji" Amesisitiza Waziri Ummy.
Aidha ameongeza kuwa kuhusu suala la kusambaza madaktari bigwa wa upasuaji mikoani watafatilia kazi na kuendelea kuboresha mazingira ya wafanyakazi.
Kwa upande wake rais wa Chama cha madaktari bigwa wa upasuaji Tanzania Prof.Larry Akoko amesema kuwa wakati umefika serikali kuangalia namna ya kuboresha mikataba pamoja na kuipa kipaumbele tasnia ya udaktari pamoja na kusisitiza masuala ya maadili kwenye kazi kwa sababu wamekuwa wakiletewa malalamiko mengi.
Kauli mbiu ya mkutano na kongamano hilo la chama cha madaktari bigwa wa upasuaji Tanzania (TSA) ni kujenga mfumo wa utoaji huduma za upasuaji madhubuti unaofikika na wenye gharama nafuu Tanzania.
Home »
» WAZIRI UMMY AMETOA WITO KWA MADAKTARI BIGWA UPASUAJI KUFANYA KAZI MIKOA YOTE.
WAZIRI UMMY AMETOA WITO KWA MADAKTARI BIGWA UPASUAJI KUFANYA KAZI MIKOA YOTE.
Related Posts:
ANZANIA KUWA MWENYEJI MKUTANO MKUU WA JUKWAA LA MAJAJI WAKUUWA NCHI WANACHAMA Na Mwandishi wetu- Dodoma Tanzania inatarajiwa kuwa mwenyeji wa Mkutano Mkuu wa Jukwaa la Majaji Wakuu wa Nchi Wanachama kutoka Kusini na Mashariki mwa Afrika utakaofanyika Ji… Read More
WOWAP IMEWATAKA WAZAZI KUHAKIKISHA WANASAIDIA KUTIMIZA NDOTO ZA WATOTO WA KIKE.Na. Kadala Komba Chemba Mratibu wa Miradi Women Wake Up(WOWAP) Nasra Suleimani ameiasa jamii kuhakikisha wanasaidia kutimiza ndoto za watoto wa kike ikiwa ni pamoja na kutokomeza mimba za utotoni na vikwazo v… Read More
RAIS SAMIA AMEFANYA UTEUZI WA KATIBU MKUU … Read More
WOWAP WATOA FEDHA TASLIMU KWA WANAFUNZI IKIWA NI MWENDELEZO WA KUSAIDIA WATOTO WA KIKE Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE … Read More
WAZIRI MKUU ATOA AGIZO KWA NAIBU WAZIRI MKUU CHANGAMOTO YA MAFUTA Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amemuagiza Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Dotto Biteko aendelee kushughulikia suala la changamoto ya upatikanaji wa nishati ya mafuta katika maeneo mbalimbali nchini.“...Wata… Read More
0 Comments:
Post a Comment