Na Eleuteri Mangi, WUSM Dar es Salaam
Timu ya soka ya Tanzania Taifa Stars imeicharaza timu ya Niger goli 1-0 na kufufua matumaini ya kufuzu michuano ya Mataifa ya Afrika (AFCON) mwaka 2023 nchini Ivory Coast.
Saimon Msuva mfungaji wa goli hilo ndiye shujaa wa mchezo huo uliochezwa Juni 18, 2023 katika Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam.
Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Hamis Mwinjuma amewaongoza watanzania kuishangilia timu yao akiwa Mgeni Rasmi katika mchezo huo hatua iliyoongeza hamasa.
Mchezo huo umeshuhudiwa pia na viongozi mbalimbali akiwemo Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Saidi Yakubu na Naibu Katibu Mkuu wake Bw. Nicholas Mkapa, Rais wa Shirikisho la Mpira nchini (TFF) Wales Karia.
Tanzania ipo kundi F pamoja na timu za mataifa ya Algeria, Niger na Uganda kwa mujibu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF).
Home »
» *TAIFA STARS YAFUFUA MATUMAINI AFCON 2023, YAIFUNGA NIGER 1-0*
*TAIFA STARS YAFUFUA MATUMAINI AFCON 2023, YAIFUNGA NIGER 1-0*
Related Posts:
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 19, 2022… Read More
CHAMWINO YAJIWEKEA MPANGO MKAKATI WA KUONDOA ZIRO MASHULENINa Peter Mkwavila CHAMWINO. MKUU wa wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma Gift Msuya amesema kuwa ili kuepukana na ziro shule za masingi na sekondari wamejiwekea mpango mkakati wa kuwasaka watoto wasioenda shule na ikiwemo na k… Read More
NBS IDADI YA WATALII WALIOINGIA NCHINI YAONGEZEKA HADI ASLIMIA 62.7. Na.Kadala Komba Dodoma OFISI ya Taifa ya Takwimu (NBS), imesema kuwa idadi ya watalii walioingia nchini kuanzia Januari hadi Julai yaongezeka hadi kufikia 742,133 ikilinganishwa na 456,266 kwa kipindi Cha mwaka 2021, saw… Read More
Habari kubwa za Magazeti ya Tanzania leo August 18, 2022… Read More
JIFUNZE KUHUSU MTI UNAFUNDISHA MENGI Na.Mwl Triple J. "Basi *KWA MTINI JIFUNZENI* mfano; *TAWI LAKE likiisha KUCHIPUKA NA KUCHANUA MAJANI* , mwatambua ya kuwa *WAKATI WA MAVUNO U KARIBU"*(Mathayo 24:32) ...MAISHA Ya MWANADAMU ni Kama MTI, Matendo Yake … Read More
0 Comments:
Post a Comment