Na Moreen Rojas,
Dodoma.
Rais Mstaafu wa Serikali ya Awamu ya nne, Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amewaongoza Viongozi, Majenerali, Maafisaa, Askari, Vijana, Watumishi na Wananchi mbalimbali katika Mbio za JKT Marathon Zilizofanyika jana Juni 25, 2023, Jijini Dodoma. Mbio hizo za Kilomita 5, 10 na 21 ziliazia na kutamatika kwenye Uwanja wa Jamhuri.
Katika hotuba yake, Dkt Kikwete amepongeza Kazi nzuri inayofanywa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania Pamoja na kumshukuru Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Innocent Bashungwa (Mb) kwa kumwalika ili awe Mgeni rasmi wa shughuli hiyo.
Dkt. Kikwete pia, amelitaka Jeshi, kupitia Wizara, lione uwezekano wa kufanya mbio za Marathon mara kwa mara Jijini Dodoma ili Wananchi waweze Kushiriki na kuimarisha afya zao.
Awali, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mheshimiwa Innocent Bashungwa (Mb), amemshukuru na kumpongeza Dkt. Kikwete kwa kumuunga mkono Rais na Amri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anavyotoa hamasa kwenye Michezo nchini ikiwemo Jeshini.
Kwa upande wake, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania, Mhe.Dkt. Tulia Ackson Mwansasu, amepongeza kufaana kwa JKT Marathon 2023, aidha, alivutiwa na Kutoa zawadi kwa Mshiriki wa Mbio za Kilometa 5, aliyejitambulisha kwa Jina Mzee Mashaka, Kwa namna aliyokimbia na kumaliza ruti huku akiwahamasisha viongozi akiwemo Mgeni rasmi.
Nae, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Jacob John Mkunda amesema Jeshi litaendelea kutoa kipaumbele katika sekta ya michezo ndani na na nje ya Nchi.
Pamoja na mafanikio mengi kwa Wanamichezo Jeshini, Mkuu wa Majeshi pia ametumia fursa hio kuwapongeza Timu ya Jeshi ya Mashujaa fc, kwa kufuzu kucheza Ligi Kuu ya Tanzania Bara, baada ya kuifunga Mbeya City fc kwa uwiano wa magoli 4 kwa 1 baada ya mechi mbili za nyumbani na ugenini.
Home »
» DKT. KIKWETE AONGOZA MBIO ZA JKT MARATHON.
DKT. KIKWETE AONGOZA MBIO ZA JKT MARATHON.
Related Posts:
TANGAZO LA AJIRA JESHI LA POLISI … Read More
*INEC YAWATAKA WATENDAJI WA UBORESHAJI KUTUNZA VIFAA* Na Mwandishi wetu, KigomaTume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetaka watendaji wakati wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Mpiga Kura Mkoani Kigoma kuhakikisha wanatunza vifaa vya uandikishaji ili vikaweze kutumika m… Read More
MBUNGE NOLLO AMPONGEZA RAIS SAMIA KWA MIRADI MINGI YA MAENDELEO JIMBO LA BAHI Na. Kadala Komba Bahi Haya yamebainishwa na Mheshimiwa Mbunge wa jimbo wa Bahi Kenneth Nollo katika mkutano wa hadhara aliyofanya Mkuu wa Mkoa Dodoma Rosemary Senyemule akisikiliza kero za wananchi kata ya Ba… Read More
*TOFAUTI ZA DINI, SIASA ZISIWAGAWE WATANZANIA - DKT. BITEKO*📌 Awataka waumini kushirikiana na Askofu Pangani📌Serikali kuendelea kushirikiana na taasisi za dini nchini📌 Rais Samia apewa tuzo kwa uongozi uliotukuka na kulinda amani*Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati*N… Read More
MWAROBAINI WA VITENDO VYA UKATILI NA USHOGA UMEPATIKANA ASKOFU MALEKANA Na. Kadala Komba DodomaMwenyekiti wa Bodi ya Chama cha Biblia cha Tanzania Askofu Mkuu Mark Walwa Malekana Amesema tunaamini taifa la leo na kanisa la leo limejengwa juu ya Watoto tusipofanya bidii kuwatahadharish… Read More
0 Comments:
Post a Comment