Imeelezwa kuwa, Mitaa 28 ambayo bado
haina umeme katika Jimbo la Handeni mjini ipo katika mpango wa
kupatiwa umeme kupitia mradi wa umeme vijijini Awamu ya Tatu mzunguko wa
Pili unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).
Hayo
yamesemwa bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Nishati, Wakili
Stephen Byabato wakati akijibu swali la Mbunge wa Handeni Mjini,
Mheshimiwa Reuben Nhamanilo Kwagilwa ambaye aliuliza kuhusu mpango wa
Serikali wa kupeleka umeme katika mitaa 28 ya Jimbo la Handeni Mjini
ambayo bado haijapata umeme.
Naibu Waziri alisema kuwa, mitaa
hiyo inapelekewa umeme na mkandarasi kampuni ya DERM ELECTRICS TANZANIA
ambae yupo katika eneo la kazi na anaendelea na ujenzi wa miundombinu ya
umeme katika maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Handeni.
Naibu
Waziri aliongeza kuwa, Jimbo la Handeni Mjini lina jumla ya mitaa 60
ambapo kati ya mitaa hiyo, 32 ina umeme sawa na asilimia 53.3 na mitaa
28 haina umeme sawa asilimia 46.7.
Alisema kuwa kazi ya kupeleka umeme kwenye mitaa hiyo itakamilika Mwezi Desemba, 2022.
Home »
» MITAA ISIYO NA UMEME IFIKAPO DESEMBA 2022 IWE IMESAMBAZIWA UMEME
MITAA ISIYO NA UMEME IFIKAPO DESEMBA 2022 IWE IMESAMBAZIWA UMEME
Related Posts:
VIJANA NA WANAWAKE CHANGAMKIENI FURSA ZA KILIMO. Na Moreen Rojas,Dodoma.Waziri wa Utamaduni,Sanaa na Michezo Mhe.Balozi Pindi Chana amewataka vijana na wanawake kuchangamkia fursa za kilimo.Waziri Pindi ameyasema hayo katika ufunguzi wa kongamano la zao la mtama maony… Read More
HABARI PICHA : MHE.MEJITII AVUTIWA NA ZANA ZA KILIMO MAONESHO YA 88 DODOMA BANDA LA DASPANa. Kadala Komba Dodoma Mwenyekiti wa Halmashauri ya Bahi Mh. Donald Mejitii na Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM Taifa ametembelea Mabanda wakati wa Maonesho ya Kilimo Kimataifa Nane Nane yanayoendelea kat… Read More
MKUU WA MKOA SENYAMULE AMELIPONGEZA SHIRIKA LA DASPA KWA KUZALISHA MBEGU BORA Mhe.Mkuu wa Mkoa Rosemary Senyamule amelipongeza Shirika la DASPA kwa kuwa wazalishaji wa mbegu bora ikiwa ni njia nzuri ya kuimarisha maisha ya mkulima kwa kumpatia lishe na kipato.Mhe.Senyamule ameyasema hayo wakati w… Read More
NAIBU WAZIRI KATAMBI AMEIPONGEZA DASPA KWA KUUNGA MKONO JITIHADA ZA RAIS SAMIA Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE … Read More
YALIYOJIRI LEO AGOSTI 15, 2023 WAKATI WA UFUNGUZI WA JENGO LA KITEGA UCHUMI (SAFINA HOUSE) LA KANISA LA ANGLIKANA* *Aliyosema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan*#Pamoja na kutoa huduma zilizopangwa, jengo hili la kitega uchumi limebadili mandhari na limeleta mandhari ya kupendeza ndani ya Jiji la Dodoma… Read More
0 Comments:
Post a Comment