Home »
» DIWANI NDONU AMETOA SIKU SABA KWA WAZAZI WA WANAFUNZI AMBAO HAWAJARIPOTI SHULE
DIWANI NDONU AMETOA SIKU SABA KWA WAZAZI WA WANAFUNZI AMBAO HAWAJARIPOTI SHULE
Na. Kadala Komba Dodoma
Diwani Kata ya Bahi Mkoa wa Dodoma Mhe.Augustino Ndonu ametoa siku saba kwa wazazi wa wanafunzi ambao bado hawajaripoti shule hadi sasa baada ya kufaulu darasa la saba na kuchanguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka 2023 kuhakikisha wanafanya hivyo na atakae kaidi agizo hilo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.
Mhe Ndonu ametoa agizo hilo wakati akitoa msaada wa vifaa vya shule kwa wanafunzi 59 kwenye kata hiyo kwa wanafunzi wanaohishi mazingira magumu, Miongoni mwa vifaa alivyotoa kwa wanafunzi hao ni pamoja na vitambaa vya kushona sare za shule ikiwa ni kaptula sketi, shati ,viatu,daftari soksi,pamoja na kalamu.
“Zaidi ya Million Tatu zimetumika kununua vifaa hivi fedha ambazo zimetoka kwenye Halmashauri yetu kwenye mfuko wa Elimu kwa lengo la kuboresha mzingira ya kupata Elimu Bora leo tumegawa shule 5 zilizopo kwenye kata yetu ,hivyo naagiza kuanzia leo January 24,2023 hadi ifikapo January 30 ,2023 watoto hao wawe wamekwisha ripoti shule na kuanza masomo.
Mhe Ndonu amesema baada ya siku hizo wataanza msako na kukamata wazazi wote ambao watakeuka agizo hilo na kulipa faini ya Elfu 50. Pia nakuwaeleza faida za kusomesha mtoto kwamba akifanikia mtoto faida itakua ya mzazi na familia nzima.
Kwaupande wake Afisa Elimu Sekondary Bahi Mery Chakupewa amesema kupitia mfuko wa Elimu Bahi ambao umeanzishwa na Halmashauri kwa lengo la kusaidia wanafunzi wanaotoka katika mazingira magumu, mfuko umewezesha wanafunzi kuwa na ufaulu mzuri katika mitihani ya shule za msingi na secondary, sababu wazazi wanatambua uwepo wa mfuko huo hivyo wanaimiza watoto kuanza shule na kumaliza.
Aidha Mamos Longoye Mkuu wa shule Bahi B sekondari ameishukuru serikali kwa kuanzisha mfuko huo ambao unawasaidi sana watoto wanaotoka mazingira magumu kuna wanafunzi wanashindwa kuja shule hawana sare za shule na viatu kupitia mfuko huu watoto hao wameludi shule na sasa wanaendelea na masomo.
Hapines Sevelina mwanafunzi wa kidato cha kwanza secondary B mnufaika wa mfuko huo ameshukuru kwa serikali kuwasaidi na kuahidi kufanya vizuri katika masomo yake.
Diwani Kata ya Bahi Mkoa wa Dodoma Mhe.Augustino Ndonu wakati akizungumza na wazazi wa wanafunzi wanaoishi mazingira magumu.
Diwani Kata ya Bahi Mkoa wa Dodoma Mhe.Augustino Ndonu wakati akikabidhi vifaa vya shule kwa wanafunzi
wazazi wa wanafunzi wanaoishi mszingira magumu
Related Posts:
MAONESHO YA MADINI YAUFUNGUA MKOA WA LINDI Ruangwa - LindiMaonesho ya Kwanza ya Madini na Fursa za Uwekezaji yanayoendelea Mkoani Lindi yametajwa kuufungua mkoa huo kiuchumi na kuongeza fursa mbalimbali za uwekezaji katika Sekta ya Madini.Hayo yamebainishwa na W… Read More
RAIS SAMIA AMEFANYA UTEUZI WA KATIBU MKUU … Read More
WOWAP IMEWATAKA WAZAZI KUHAKIKISHA WANASAIDIA KUTIMIZA NDOTO ZA WATOTO WA KIKE.Na. Kadala Komba Chemba Mratibu wa Miradi Women Wake Up(WOWAP) Nasra Suleimani ameiasa jamii kuhakikisha wanasaidia kutimiza ndoto za watoto wa kike ikiwa ni pamoja na kutokomeza mimba za utotoni na vikwazo v… Read More
WAZIRI MHAGAMA AMEWATAKA WANANCHI KUTUMIA MVUA ZA EL_NINO VIZURI Na Moreen Rojas,Dodoma.Waziri wa nchi,ofisi ya waziri mkuu,sera,bunge na uratibu Mhe.Jenista J.Mhagama ametioa wito kwa umma kutumia vizuri mvua za EL_NINO vizuri ili ziwe na manufaa kupitia shughuli za uzalishaji mali kama k… Read More
WAZIRI MHAGAMA APOKEA MWONGOZO WA KITAIFA Na; Mwandishi wetu - DodomaWaziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu nayeshugulika na Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama, Amepokea Rasimu ya kwanza ya Mwongozo wa Kitaifa wa Ufuatiliaji na Tathmini ya Utendaji wa Sh… Read More
0 Comments:
Post a Comment