Home »
» WANAWAKE 15 WAMEFANYIWA UPASUAJI WA UGONJWA WA FISTULA
WANAWAKE 15 WAMEFANYIWA UPASUAJI WA UGONJWA WA FISTULA
Na. Mwandishi wetu Mbeya
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Maji Maryprisca Mahundi Amezindua Rasmi kambi ya matibabu ya Fistula katika Hospitali ya kanda ya Rufaa Mbeya ,amesema Ugonjwa wa Fistula unawasababishia maumivu makali wanawake huku ukiwahathiri kisikolojia hasa pale wanaponyanyapaliwa na jamii pamoja kukimbiwa na wenza.
Aidha Naibu Waziri amesema tangu kuanzishwa kwa kambi hiyo Januari 16 mwaka huu mpaka sasa ni wanawake 15 pekee ndio waliofanyiwa upasuaji kati ya wanawake 60 wanaolengwa kunufaika na huduma hiyo ambayo inatolewa bure.
“Kambi hiyo imeandaliwa kwa ushirikiano kati ya Hospital kanda ya Mbeya na Ofisi ya Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Mbeya
Kwaupande wake mwakilishi wa chama cha Madaktari wa Upasuaji wa Fistula Tanzania ,Dk.Peter Majige amesema wanawake 3000 huugua kila mwaka ugonjwa huo nchini huku 1500 pekee wakitibiwa kutokana na matatizo mbalimbali .
Amesema matibabu ya ugonjwa huo huwa yana gharama kubwa hali ambayo wananchi wengi wanashindwa kumudu na hivyo kukilazimu chama hicho kuomba ufadhili kutoka kwenye mashirika mbalimbali ya kitaifa.
Ameiomba serikali kusamehe baadhi ya gharama za matibabu ya ugonjwa huo ili kuwasaidia wagonjwa wengi Zaidi kupata matibabu na kuondokana na tatizo hilo.
Katika hatua nyingine Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Kanda ya Rufaa ya Mbeya, Dk.Francis Rwegoshora amesema Hospital hiyo inatoa huduma ya matibabu ya ugonjwa huo lakini wagonjwa wengi wanashindwa kufika kutokana na uchumi mdogo pamoja na kutopata Taarifa .
Amesema kambi hiyo iliyopelekwa katika Hospitali hiyo itasaidia kuwatambulisha matibabu hayo kwa wananchi wa maeneo mbalimbali ya mikoa ya Kanda ya Nyanda za Juu Kusini ili waende wakatibiwe.
Naibu Waziri wa Maji Maryprisca Mahundi Akiwa na mwakilishi wa chama cha Madaktari wa Upasuaji wa Fistula Tanzania
MATUKIO KATIKA PICHA YA UZINDUZI RASMI WA KAMBI YA MATIBABU YA FISTULA MBEYA
Related Posts:
*MAADHIMISHO YA SIKU YA MWALIMU BUKOMBE 2023*Leo Oktoba 6, 2023 Sherehe ya Siku ya Mwalimu Duniani inaadhimishwa katika wilaya ya Bukombe mkoani Geita ambayo itahudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Kitaifa na Mkoa pamoja na Walimu kutoka wilayani Bukombe. Mgeni rasmi kat… Read More
*GEITA TUPO NJIANI UWT MOTOO MOTOO**ZIARA YA MWENYEKITI NA WAJUMBE WA KAMATI YA UTEKELEZAJI YA BARAZA KUU LA UWT PAMOJA NA WAJUMBE WA NEC MKOA WA GEITA*Ikiongozwa na Mwenyekiti wa UWT Taifa na Mjumbe wa Kamati kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Ndg. Mary Chatand… Read More
UTPC KUENDELEA KUIMARISHA USHIRIKIANO WA WANACHAMA NA WADAU. Na Moreen Rojas,Dodoma.Rais wa UTPC Deogratius Nshokolo amesema katika kipindi cha 2023_2025 UTPC inaendelea kuimarisha ushirikiano kati ya wanachama na wadau wengine wa habari nchini.Rais wa UTPC ameyasema hayo w… Read More
*RAIS SAMIA AMEIBEBA KWA DHATI AJENDA YA MATUMIZI NISHATI MBADALA – NAIBU WAZIRI KAPINGA* *Lilian Lundo, Veronica Simba na Zuena Msuya - Songea*Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameibeba kwa dhati ajenda ya matumizi ya … Read More
IDADI YA WATALII KUTOKA NJE YA NCHI IMEONGEZEKA. Na Moreen RojasDodoma.OFISI ya Taifa ya Takwimu imesema kuwa idadi ya Watalii kutoka nje ya nchi kwa kipindi cha Mwezi Januari hadi Agosti Mwaka 2023 imeongezeka na kufikia 1,131,286 ikilinganishwa na Watalii 900,… Read More
0 Comments:
Post a Comment