![]() |
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.
![]() |
Na Peter Mkwavila CHAMWINO.
ASKOFU wa kanisa la Pentecostal Holiness Association Mission Tanzania PHAM (T) Kanda ya Kati Brayson Msanjila,amewashauri familia zinazogundulika kuwa na wagonjwa wa afya ya akili waache tabia ya kuwapeleka kwa waganga wa kienyeji na wapiga ramli.badala yeke wawapeleke kwenye vituo vya afya ili wakapime afya zao kitaalamu zaidi.
Msanjila amesema hayo alipokuwa apokuwa akizungumza na wakazi wa kijiji cha Chalinze nyama wilaya ya Chamwino kwenye ibada iliyoandaliwa kwa ajili ya kumpongeza mchungaji Saimon Sandiya aliyetimiza miaka 40 toka awe kwenye utumishi wake,
Ibada hiyo iliyofanyika katika kanisa la Pentecostal Holiness Association Mission Tanzania PHAM (T) Usharika wa Yerusalemu Chalinze Nyama Chamwino.
Askofu ameziomba familia hizo pindi zinapotokea kuwepo kwa mgonjwa wa afya ya akili,ni vizuri akapelekwa hosptalini badala ya huko kwa waganga na kwa wapiga ramli.
Alisema kuwa tatizo la afya ya akili likipatiwa matibabu haraka kwa asilimia kubwa linatibika haraka tofauti kama mgonjwa huyo akipelekwa kwa waganga wa kienyeji.
“Hivyo niziombe familia hususah huku vijijini pindi mnapogundua kuna tatizo hilo miongoni mwenu acheni kumkimbiza mgonjwa huyo kwa mganga wa kienyeji na wapiga ramli,bali wapelekeni hospitalini wakapatiwe matibabu ya kitaalam zaidi.
Alisema serikali kupitia hospitali zake kuna wataalamu wa kutosha kwa ajili ya magonjwa ya afya ya akili,hivyo hakuna sababu ya kuwapeleka watu wanaongudulika kuwa na tatizo hilo.
Awali akizungumza na wakazi hao wa kijiji hicho pia amewashauri wakulima kuhakikisha wanaandaa mashamba yao mapema ikiwemo na kuweka mbolea kwa ajili ya maandalizi ya kupanda mbegu kwa wakati.
Naye Mchungaji Saiman Sandiya ambaye kiongozi wa kanisa hilo la Pentecostal Holiness Association Mission Tanzania PHAM (T) Usharika wa Yerusalemu Chalinze Nyama Chamwino.
Kwa upande wake amewataka wazazi na walezi ambao wana wanafunzi waliomaliza elimu ya msingi kuwaendeleza kielimu zaidi badala ya kuwaweka majumbani.
Sandiya ambaye ametimiza miaka 40 ya uchungaji kwa kumtumikia Mungu,alisema kuwa wanafunzi hao wanatakiwa kuwaendeleza kielimu ikiwemo na kwenye vyuo vya ufundi na kwa kufanya hivyo watakuwa wamewawekezea taaluma.
Alisema kuwa watoto hao wakianchwa bila kuendelezwa taifa litakuwa na tabaka la vijana wanaoweza kujikuta wakijiingiza kwenye makundi maovu kama vile panya road na mengineyo.
Mwisho.
Na Mwandishi wetu- Kilimanjaro
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga amewahimiza wadau wa maendeleo na watu binafsi kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kuchangia vifaa vya misaada ya kibinadamu wakati wa maafa.
Mhe. Ummy aliyasema hayo alipofanya ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua ghala la kuhifadhi vifaa vya misaada ya kibinadamu wakati wa maafa Kanda ya Kaskazini lililopo maeneo ya Chekereni, Wilaya ya Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro.
Alisema uungwaji mkono wa serikali kutoka kwa wadau unasadia wananchi kufikiwa na huduma kwa haraka kutokana na majanga yaliyojitokeza ambayo husabababisha madhara kama vifo, ulemavu wa kudumu, mali kuharibika pamoja na miundombinu.
“Nitoe wito kwa wadau na watu mbalimbali ambao wanaguswa kushirikiana na serikali kwa kutoa vifaa wafanye hivyo pengine ngaji ya Wilaya, Mkoa na hata kijiji ili tuwe navyo vya kutosha ili yanapotokea tunatoa msaada kwa haraka,” alihimiza Mhe. Ummy.
Pia Mhe. Ummy alisisitiza utunzwaji wa magahala hayo hatua itakayosaidia vifaa hivyo kudumu kwa muda mrefu na kuwa tayari kutumika pindi vinapohitajika katika maeneo yenye maafa.
Aidha aliupongeza uongozi wa mkoa wa Kilimanjaro kwa utayari wa kutoa msaada wa kibinadamu kwa wananchi wanaokumbwa na maafa kwa lengo la kuwasaidia kurejea katika hali yao ya awali.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Kilimanjaro ambaye ni Afisa Mifugo katika Mkoa huo Bwa. James Shao alisema ghala la Kanda ya Kasikazini linahudumia Mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Tanga.
Naibu
Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga
akizungumza wakati alipotembellea na kukagua ghala la kuhifadhi vifaa vya
msaada wa kibinadamu wakati wa maafa
lililopo mkoani Kilimanjaro.
![]() | ||||
| Afisa Ugavi Sekretarieti ya Mkoa wa Kilimanjaro Bwa. Claude Kilala akitoa maelezo kwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu ) Mhe. Ummy Nderiananga alipotembelea ghala hilo. |

Naibu
Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga
akikagua ghala la kuhifadhi vifaa vya msaada wakati wa maafa lililopo mkoani
Kilimanjaro.
NA MWANDISHI WETU
Serikali imetoa rai kwa viongozi wa dini kuendelea kuhimiza jamii kuepuka uraibu wa matumizi ya dawa za kulevya na kujenga uelewa kuhusu madhara ya madawa ya kulevya.
Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa bajeti katika kipindi cha robo ya kwanza ya Mwaka 2022/23 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya UKIMWI na Dawa za Kulevya Mjini Dodoma.
“Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana Dawa za kulevya, itaendelea kushirikiana na Wizara nyingine katika kuona namna nzuri ya kuandaa maudhui ya mtandaoni ili kuelimisha vijana kuhusu athari ya dawa za kulevya kama ambavyo Tume ya Kudhibiti UKIMWI inavyofanya”.
Tupo kwenye utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ambayo imetoa maelekezo mahususi kuhusu kushughulikia dawa za kulevya, Amesema Naibu Waziri.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya UKIMWI na Dawa za Kulevya Dkt. Alice Karungi ameipongeza serikali kwa kiwango cha fedha kilichopelekwa kwenye Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kinachoendana na kwa kiwango cha fedha kilichokadiriwa wakati wa bajeti.
“Zoezi la kuwasaidia vijana wetu waliopata nafuu ya uraibu wa dawa za kulevya kwa kupatiwa mafunzo ya kukuza ujuzi; kama sehemu ya jitihada za Mamlaka, katika kudhibiti na kupambana na dawa za kulevya, liwe endelevu”.
Naye Kamishina Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Gerald Musabila amesema mamlaka imeweka msukumo mkubwa katika kukabiliana dawa zinazotoka nje ya nchi, Heroin, Cocaine na Methamphetamine.
“Bangi imekuwa ikitumika kwa wingi kwa sababu inapatikana kwa bei nafuu na zinalimwa katika maeneo ya kujificha sana”.
Tamaa ya kupata fedha imekuwa ikichochea wananchi kulima bangi kulinganisha na mazao mengine hata hivyo udhibiti unaendelea.
“Tunashirikiana na wenzetu wa Wizara ya Klimo waweze kushauri Mwananchi badala ya kulima bangi walime zao gani ambalo litawasaidia kupata fedha nyingi.”
Naye Mkurugenzi wa Tume ya Kudhibiti UKIMWI Dkt. Leonard Maboko ameihakikishia Kamati ya Kudumu ya Bunge ya UKIMWI na Dawa za Kulevya kwamba fedha za Global Fund zitatoka robo ya pili ya mwaka wa fedha 2022/23.
“Mradi wa Umoja wa Mataifa wa Kuhusisha UKIMWI kwenye Mpango wa Maendeleo wa Taifa katika bajeti 2022/23 iliyoidhinishwa ya shilingi 2,132,610,000.00, tayari kiasi cha shilingi 1,090,849,597.00
Naye Mhe. Asia Halamga ameomba serikali kubadili baadhi ya Sheria zinazowazuia Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya iweze kufanya kazi zake kikamilifu.
“Fedha tunazotumia kutibu ni vyema tukazitumia kudhibiti ili tusiendelee kuumiza taifa na hasa vijana”.
Naibu
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Mhe. Ummy Nderiananga akizungumza
Mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya UKIMWI na Dawa za Kulevya
alipokuwa akitoa taarifa kuhusu utekelezaji wa bajeti kwa kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2022/23.
Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya UKIMWI na Dawa za Kulevya Dkt. Alice Karungi akizungumza wakati wa kupokea taarifa kuhusu utekelezaji wa bajeti kwa kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2022/23.
Mjumbe wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ukimwi na Dawa za Kulevya Mhe. Neema Mwandabila akizungumza jambo wakati wa kupokea taarifa kuhusu utekelezaji wa bajeti kwa kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2022/23 kwa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu.
Kamishina Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya Gerald Musabila (Kulia) katika picha wakati wa kutoa taarifa kuhusu utekelezaji wa bajeti kwa kipindi cha robo ya kwanza ya mwaka 2022/23.
![]() |
![]() |
| Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.
Rosemary Senyamule wakati ametembelea kiwanda cha mbolea cha Intracom
Tanzania |
| Waandishi wa habari wakipatiwa mafunzo namna ya kutumia vyombo vya habari katika kuelimisha Jamii juu ya kujikinga na Uviko 19 |
| |
WATOTO wa Kituo cha yatima kinachomilikiwa na taasisi ya All Hafidhu Islamic Orphans Centre kilichopo Bicha wilaya ya Kondoa.
Wameliomba Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) kuwajengea uzio utakao wawezesha kudhibiti uharibufu wa vibaka ikiwemo na ulinzi wa mipaka ya kituo hicho na jamii inayowazunguka.
Ombi hilo limetolewa na Mkurugenzi wa taasisi hiyo Ukht Aisha Nobe,kwa niaba yao watoto mbele ya Shekhe wa mkoa wa Dodoma (BAKWATA) Mustaph Rajabu wakati alipokuwa akifunga kongamano la wanawake wakiislamu la siku 3 lililofanyika kituoni hapo.
Aisha,alisema kituo hicho kwa muda mrefu toka kujengwa hakina uzio ambao unaoweza kudhibiti vibaka na hata mipaka ya maeneo yanayozunguka.
“Mbali na kituo hicho kuwa na wanafunzi wa shule ya msingi,pia tunawatunza watoto wenye mahitaji maalumu,ila hakuna uzio ambao unaoweza kulinda mipaka na usalama wa mali na wao wenyewe”alisema.
Akizungumza kwenye kongamano hilo lililowashirikisha wanawake kutoka dini ya kiislamu kwa ajili mafunzo,pia maada mbalimbali zilitolewa ikiwemo ya elimu kwa wanawake,malezi kwa watoto ndoa,ibada na ndoa ya mitaala.
Kwa upande wao washiriki ambao ni wanawake wametakiwa kuwa mabalozi wa elimu waliyoipata kwa wengine ili dini hiyo iweze kuondokana na changamoto zinazowakabiri.
Naye Shekhe wa Mkoa wa Dodoma wa Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Mustapha Rajabu,alisema Kituo hicho kinatakiwa kuwa kwenye usalama zaidi ukizingatia kuna watoto wadogo wanaohitaji usalama mkubwa.
Alisema kutokana na umuhimu huo Bakwata kwa kushirikiana na taasisi zingine na wadau wa elimu watahakikisha wanasaidia kuondoa kero hiyo ya kukosa uzio ambao umesababisha kuwepo kwa mwingiliano.
“Nimesikia kilio chenu sisi kama Bakwata tutahakikisha tunashirikiana na wadau wengine tunatatua kero hii ili watoto wetu wasome kwenye hali ya usalama na hata mali zao ziwe salama pia na hata kwenye mipaka nayo ijulikane pia”alisema.
MWISHO.
| |