Na Mwandishi Wetu,Mtwara.
SHIRIKA la Uwakala wa Meli Tanzania(TASAC)limetoa elimu kwa wananchi kuhusu namna Shirika linavyotekeleza Majukumu yake kwa Mujibu wa Sheria.
Elimu hiyo imetolewa katika maonesho ya Bishara, Uwekezaji na Fursa yanayofanyika katika viwanja vya Mashujaa kuanzia tarehe 19 hadi 31 Machi, 2023 Mkoani Mtwara.
Akizungumza na Vyombo ya habari Kaimu Afisa Mfawidhi wa Mkoa wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania Mkoa wa Mtwara, Mha. Jospeh Myaka amesema kuwa katika kutekeleza majukumu yao Shirika hilo limejikita katika kutoa elimu kwa wananchi kufahamu shirika hilo linavyotekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria.
Amesema kuwa licha ya majukumu makubwa waliyonayo pia TASAC imeshiriki maonesho hayo ili kuwapa elimu wananchi kuhusu fursa za biashara zilizopo katika Sekta ya Usafiri kwa njia ya Maji sambamba na elimu kuhusu Usalama, Ulinzi na Utunzaji wa mazingira majini jukumu linalotekelezwa na Shirika hilo.
“TASAC tunashiriki maonesho haya ya Biashara Uwekezaji na Fursa mkoani Mtwara ili kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu yanayotekezwa Kisheria. kama mdhibiti wa shughuli za usafiri kwa njia ya maji tunasimamia huduma zinazotolewa na Bandari, tunadhibiti na kusimamia ulinzi, usalama na utunzaji wa mazingira na kuratibu shughuli za uokoaji na utafutaji pale panapotokea dhoruba majini”
“Pia tunatoa elimu kwa wananchi wa Mtwara na wadau wa usafiri kwa njia ya maji katika jukumu letu la Udhibiti wa Safari kwa njia ya Maji na udhibiti Usalama, Ulinzi na Utunzaji wa Mazingira majini, wanaweza kufanya shughuli zao kwa usalama na kupata maendeleo na kuongeza pato la Taifa.” Ameeleza Myaka.
Kwa mujibu wa Sheria, TASAC ina wajibu wa kusimamia kazi mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuhimiza usimizi na shughuli za uwakala wa meli wenye ufanisi, kuhimiza shughuli za bandari na huduma za meli zenye ufanisi, kuhakikisha kunakuwepo usalama na ulinzi wa shehena, kuhimiza na kutunza mazingira, usalama na ulinzi wa bahari, maziwa na mito.
Maonesho hayo ya Biashara, Uwekezaji na Fursa ni maonesho ya Kwanza kufanyika Mkoani Mtwara yakiwa na lengo la kuwaleta pamoja wadau mbalimbali katika Sekta hiyo ili kubadilishana uzoefu wa kitaalamu na kujifunza biashara na uwekezaji wa kisasa pamoja na fursa zilizopo katika sekta hiyo na Mkoa wa Mtwara kwa ujumla.
Home »
» TASAC YATOA ELIMU KWA WANANCHI MTWARA.
TASAC YATOA ELIMU KWA WANANCHI MTWARA.
Related Posts:
WAZIRI WA SHERIA DKT DAMAS NDUMBARO AMETOA UFAFANUZI KUHUSU WANAFUNZI WA SHERIA KUFELI MAFUNZO KWA VITENDONa. Kadala Komba Dodoma Kumekuwa na sintofahamu kuhusiana na matokeo ya Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST), mjadala ulioibuka katika sehemu mbalimbali kwamba kwa … Read More
WADAU WA MAENDELEO WAHIMIZWA KUCHANGIA VIFAA VYA MISAADA YA KIBINADAMU WAKATI WA MAAFA. Na Mwandishi wetu- Kilimanjaro Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga amewahimiza wadau wa maendeleo na watu binafsi kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kuchangia vifaa vya mi… Read More
SERIKALI INAENDELEA KUWEKEZA KWA WATAALAMU WA NDANI WA MIFUMONa WAF - DSMKatibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe amesema kuwa, Serikali itaendelea kuwekeza kwa Wataalamu wa ndani wa mifumo ili kuhakikisha miradi yote inayoanzishwa na Wafadhili inaendelea kusimama siku Wafad… Read More
MCHUNGAJI AWATAKA WAGONJWA WANAONGUDULIKA NA TATIZO LA AFYA AYA AKILI WAPELEKWE HOSPITALI BADALA YA KWA WAGANGA WAKIENYEJI.Na Peter Mkwavila CHAMWINO. ASKOFU wa kanisa la Pentecostal Holiness Association Mission Tanzania PHAM (T) Kanda ya Kati Brayson Msanjila,amewashauri familia zinazogundulika kuwa na wagonjwa wa afya ya akili waac… Read More
WAZIRI PINDI CHANA AZINDUA BODI YA WAKURUGENZI TAWAWaziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana leo tarehe 12 Oktoba, 2022 amezindua Bodi ya Wakurugenzi ya TAWA aliyoiteua hivi Karibuni.Akizungumza katika hafla ya Uzinduzi iliyofanyika Makao Makuu ya TAWA Mk… Read More
0 Comments:
Post a Comment