Home »
» TAHADHARI IMETOLEWA KWA WANANCHI KUJIKINGA NA MAJANGA YA MOTO
TAHADHARI IMETOLEWA KWA WANANCHI KUJIKINGA NA MAJANGA YA MOTO
Na Sifa Lubasi Dodoma
WANANCHI wametakiwa kuchukua tahadhari wanapotibu majeraha ya moto ili kupunguza uwezekano wa jeraha kuwa kubwa zaidi na kushindwa kutibika kwa wakati na hata kusababisha kifo
Akizungumza leo kwenye maadhimisho ya miaka 70 ya Baraza la Uuguzi na Ukunga yanayofanyika katika viwanja vya Nyerere square,Ofisa Muuguzi Msaidizi Mwandamizi daraja la pili David Mpaguke kutoka hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) alisema majanga ya moto hutokea popote na wakati wowote
Alisema kuwa ulimwenguni kote kila mwaka takribani watu milioni moja hutafuta matibabu kutokana na kuungua moto.
Álisema kuwa hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa mwaka 2020 hadi 2022 imepokea na kulaza wagonjwa 225 walioungua mwa moto asilimia 87 walipona na asilimia 13 walikufa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kucheleweshwa kufikishwa hospitali, mika na desturi ya jamii,Imani na changamoto za Uchumi.
Álisema kuwa kitaalam mtu anapoungua amwagie jeraha maji safi ili kupunguza joto lisiathiri ngozi na misuli, Kisha apewe Panadol kwa ajili ya kutuliza maumivu na awahishwe hospitali
"Majeraha madogo ya moto, haraka mwaga maji baridi juu ya ngozi iliyoungua kwa dakika 15 hadi 30 husaidia kupunguza joti lisiathiri ngozi na misuli,,Álisema
Pia alisema kuwa ulaji wa vyakula vingi vyenye virutubishi vikiwemo protini ya ziada vinahitajika kusaidia kidonda cha moto kuponai
"Mgonjwa apatiwe vyakula vya profini ili Kujenga mwili ili nyama ziwe zinajengwa pia kufanya mazoezi ili kuzuia ulemavu unaoweza kutokea," alisema
Álisema kuwa kama majeraha ya Moto Ni makubwa mgonjwa hufanyiwa upasuaji wa kupandikizwa ngozi.
Álisema kuwa kumekuwa na njia mbalimbali za asili za kutibu majeraha ya Moto lakini nyingi so salama.
Baadhi ya wananchi wakiwa kwenye moja ya mabanda kwenye maadhimisho ya miaka 70 ya Baraza la Uuguzi na Ukunga yanayofanyika katika viwanja vya Nyerere square Jijini
Related Posts:
WOSIA WA MAMA. BINTI YANGU YAJUE HAYA) NDOA INAANZA BAADA YA HARUSI Mwanangu nisikufiche, watu wengi huchangia sherehe ili waje kula na kunywa na kuoneshana fahari zao. Ukoo wa Mume na ukoo wa mke nao wanaoneshana umwamba hawa kwenye Send-off na hawa wanajibu kwenye harusi. Na ule usiku … Read More
JITOKEZENI KWENYE ZOEZI LA SENSA ILI MUHESABIWENa. Mwandishi Wetu. Jitokezeni kwenye zoezi la sensa ili muhesabiwe Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene amehimiza wananchi kujitokeza kuhesabiwa katika zoezi la sensa ya … Read More
ASKOFU MWAKANDULU MIPANGO YOYOTE BILA TAKWIMU HUKUMU YAKE NI UMASIKINI Na. Kadala Komba Dodoma. Askofu Emmanuel Mwakandulu wa kanisa la Baptist jimbo la Dodoma mjini amesema Sensa sio jambo la kisiasa hili kujua idadi ya watu unaowaongoza lazima ujue idadi halisi ya watu, bali ni jambo la k… Read More
HABARI KUBWA KWENYE MAGAZETI YA LEO JUMATANO AGOSTI 24,2022 … Read More
Waziri Simbachawene amshukuru Rais kwa fedha ya miradi maendeleoNa.Mwandishi Wetu. Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Mhe. George Simbachawene ameshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa kiasi cha billioni 16 kwa mwaka ulio… Read More
0 Comments:
Post a Comment