Home »
» WAFANYABIASHARA WANAOANZA BIASHARA WAMERUSIWA KUFANYA BIASHARA MIEZI 6 BIRA KULIPA KODI
WAFANYABIASHARA WANAOANZA BIASHARA WAMERUSIWA KUFANYA BIASHARA MIEZI 6 BIRA KULIPA KODI
Na Kadala Komba , Kondoa
WAZIRI wa Viwanda na Biashara Dk Ashatu Kijaji amésema kuwa Rais Samia Suluhu Hassan ametoa kibali cha kuruhusu wafanyabiashara wanaoanza biashara kutokulipa kodi kwa kipindi cha miezi sita hadi mwaka moja
"Rais ametoa kibali ,wale wanaoanza biashara kufanya biashara miezi sità hadi mwaka moja ndipo waanze kulipa Kodi," alisema.
Álisema hayo Jana wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika kimkoa katika wilaya ya Kondoa Mkoani Dodoma
Álisema kuwa jambo hilo linaonesha ni jinsi gani Rais Samia Suluhu Hassan anawajali wananchi wake Ni vyema kila mmoja akäuunga mkono juhudi za Rais katika kuwaletea wananchi maendeleo. .
Pia aliwataka wananchi kuachana na mikopo umiza na Ile ya kausha damu kwani imekuwa ikiumiza wananchi. kutokana na kuwa na riba kubwa.
"Halmashauri zimekuwa zikitoa mikopo ya asilimia nne, wananchi Muende mkope huko pia Rais ametoa fedha kwenye Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (Sido) ambapo mikopo hutolewa kwa riba ya asilimia tisa, Muende Sido mkachukue mikopo na kupatiwa mafunzo ya biashara," alisema.
Álisema kuwa mikopo yenye riba kubwa imekuwa ikiumiza wananchi huku wakiwa hawapati faida yoyote.
Pia aliwataka wanawake wanaofanya biashara mipakani kufuata sheria na taratibu.
"Kama unataka kufanya Biashara mpakani kachukue hati ya kusafiria ili kufanya biashara kihalali,Kuna malalamiko ya wanawake
wanaokamatwa kwa kufanya biashara mipakani bila kuwa na vibali"alisema.
kwa upande wake Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoa wa Dodoma Pili Mbanga alisema kuwa Sasa Kuna janga kubwa kwa watoto wa kiume na ndoa za jinsia moja.
" Tujitahidi kuwalea watoto katika mazuri bila hivyo tutakuwa tunatengeneza taifa chenye kizazi cha ajabu , tusiwe bize na biadhara na kazi tuangalie pia malezi ya watoto" alisema.
Jaji Mstaafu ambaye pia ni mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Mathew Maimu alisema kuwa palipo na mwanamke Kuna amani pia kuna uwepo wa Mungu .
aliwataka wanawake kuendelea kupigania haki zao .
"Tuendelee kumuunga mkono Rais na viongozi wote, tusrudi nyuma tuendelee kukaza buti badala ya kutembea tukimbie," alisema.
.
Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo mkuu wa mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule Álisema bado wanawake ni wachache katika ngazi mbalimbali za uongozi.
Pia aliwataka wanawake kutumia fursa za kiuchumi zilizopo katika mkoa wa Dodoma ili kujiongezea kipato
mwisho.
Related Posts:
WACHAKATAJI WA MAZAO YA UVUVI WAPIGWA MSASAWACHAKATAJI WA MAZAO YA UVUVI WAPIGWA MSASA. Wachakataji wa mazao ya uvuvi nchini wametakiwa kutumia fursa ya teknolojia katika shughuli zao ili kuboresha mnyororo wa thamani wa mazao ya uvuvi na kukabiliana na upotevu wa m… Read More
RWANDA KUBADILI MUDA WA MASOMO SHULE ZOTE IFIKAPO MWAKA 2023Rwanda wamebadili muda wa kuanza na kumaliza masomo na saa za kazi. Kuanzia Januari 01 2023, Shule zote zitaanza masomo saa 2:30 asubuhi na kumaliza saa 11 jioni. Saa za kazi ni kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 11 jioni. Hii… Read More
MKUU WA MKOA DODOMA MHE. ROSEMARY SENYAMULE AMEPOKEA HATI YA PONGEZI KUTOKA CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI GEITA Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amepokea hati ya pongezi kutoka kwa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Geita kwa kutambua mchango wake na kuleta mageuzi katika kipindi ambacho amekua Mkuu wa Mkoa huo. Hati … Read More
TIMU YA MBEYA CITY YAKABIDHI ZAWADI KWA WAGONJWA KATIKA KITENGO CHA WAZAZI META.Na.Mwandishi wetu Mbeya Katika kusherehekea sikukuu za mwisho wa mwaka, ikiwemo Krismas na Mwaka mpya timu ya Mpira wa Miguu ya Mbeya City ikiongozwa na viongozi wake wametembelea Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya Kitengo c… Read More
UONGOZI DOREFA WAAGIZWA KUFUTILIA MAENEO YALIYOTENGWA KWAJILI YA MICHEZO Na Kadala Komba Dodoma Wanamichezo nchini waaswa kupambania tasnia ya michezo ikiwa ni agenda ya kuhakikisha tasnia hiyo inapewa thamani na kipaumbele kama sekta zingine. Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi wa michezo N… Read More
0 Comments:
Post a Comment