This is default featured slide 1 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.
This is default featured slide 2 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.
This is default featured slide 3 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.
This is default featured slide 4 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.
This is default featured slide 5 title
Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.
UZINZI NA UASHERATI NI VYANZO VYA VIFUNGO VYA NGUVU ZA GIZA KWENYE MAISHA YA MTU
SERIKALI YASISITIZA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KATIKA ULINZI NA UFUATILIAJI MIENENDO YA WANYAMAPORI
Na. Mwandishi wetu Morogoro
![]() | |||
BODI YA MAZAO MCHANGANYIKO NCHINI [CPB] IMEWATOA HOFU WAKULIMA WA MAZAO YA KUNDE
Na. Mwandishi wetu Simiyu
Bodi ya mazao mchanganyiko nchini (CPB) imesema kuwa wakulima nchini wenye mazao aina ya kunde, hawana sababu ya kuhangaika na soko la mazao yao kwani Bodi hiyo inao uhitaji mkubwa wa mazao hayo.
Ofisa Masoko wa Bodi hiyo Frank Bubelwa Akizungumza katika maonyesho ya wiki ya Chakula nchini yanayoendelea Mkoani Simiyu, amesema kuwa wakulima hawana sababu ya kuangaika na kutafuta wapi watauza mazao yao. Amesema serikali kupitia wizara ya kilimo, mazao na nafaka tumeona tuingie, tufungue milango kwa wakulima kwa kuweza kununua mazao yao yote ambayo wanalima na kuleta kwetu sisi inamaana kwa lugha nyepesi tunawasaidia kutoka katika changamoto ambayo walikuwa wananung’unika kupata masoko.
Aidha ameongeza kuwa mbali na Bodi hiyo kununua mazao kutoka kwa wakulima, bado bei ambazo wamekuwa wakinunulia mazao hayo ni rafiki kwa wakulima Lakini pia katika swala zima la bei za nafaka sisi kama taasisi sio taasisi kandamizi mkulima anapewa fursa na tunampa fedha inayoendana na bei ya sokoni mara nyingi wakulima wanakuwa na changamoto hiyo kubwa, unakuta mkulima anakuja kudalaliwa na mtu wakati kwa bei ya chini ambayo inamfanya yeye hasipate hamu au mtaji wake unaguswa kwaiyo anashindwa kufanya shughuli za kilimo. Sambamba na hilo afisa masoko Frank Bubelwaa amesema kuwa katika msimu wa kilimo bodi ya nafaka huwa tunaangalia pande zote mbili mkulima hasiumie pia sisi tusipate hasara kwaiyo mara nyingi tunanunua mali kutokana na bei iliyo sokoni kama kwamfano kilo moja ya mahalage ni silingi elfu mbili sokoni sisi tutakuja kununua kwa bei hiyohiyo hatuwezi tukashuka Zaidi ya hapo. Hivyo basi sisi tupo kwaajiri ya kuhakikisha kuwa kilimo kinaendelea kukua lakini pia kwaupande mwingine kuongeza uchumi wa nchi.
MIAKA 7 YA BMH: MKURUGENZI AELIMISHA KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE
![]() |
WAZIRI WA SHERIA DKT DAMAS NDUMBARO AMETOA UFAFANUZI KUHUSU WANAFUNZI WA SHERIA KUFELI MAFUNZO KWA VITENDO
WAZIRI PINDI CHANA AZINDUA BODI YA WAKURUGENZI TAWA
![]() |
SERIKALI INAENDELEA KUWEKEZA KWA WATAALAMU WA NDANI WA MIFUMO
MCHUNGAJI AWATAKA WAGONJWA WANAONGUDULIKA NA TATIZO LA AFYA AYA AKILI WAPELEKWE HOSPITALI BADALA YA KWA WAGANGA WAKIENYEJI.
Na Peter Mkwavila CHAMWINO.
ASKOFU wa kanisa la Pentecostal Holiness Association Mission Tanzania PHAM (T) Kanda ya Kati Brayson Msanjila,amewashauri familia zinazogundulika kuwa na wagonjwa wa afya ya akili waache tabia ya kuwapeleka kwa waganga wa kienyeji na wapiga ramli.badala yeke wawapeleke kwenye vituo vya afya ili wakapime afya zao kitaalamu zaidi.
Msanjila amesema hayo alipokuwa apokuwa akizungumza na wakazi wa kijiji cha Chalinze nyama wilaya ya Chamwino kwenye ibada iliyoandaliwa kwa ajili ya kumpongeza mchungaji Saimon Sandiya aliyetimiza miaka 40 toka awe kwenye utumishi wake,
Ibada hiyo iliyofanyika katika kanisa la Pentecostal Holiness Association Mission Tanzania PHAM (T) Usharika wa Yerusalemu Chalinze Nyama Chamwino.
Askofu ameziomba familia hizo pindi zinapotokea kuwepo kwa mgonjwa wa afya ya akili,ni vizuri akapelekwa hosptalini badala ya huko kwa waganga na kwa wapiga ramli.
Alisema kuwa tatizo la afya ya akili likipatiwa matibabu haraka kwa asilimia kubwa linatibika haraka tofauti kama mgonjwa huyo akipelekwa kwa waganga wa kienyeji.
“Hivyo niziombe familia hususah huku vijijini pindi mnapogundua kuna tatizo hilo miongoni mwenu acheni kumkimbiza mgonjwa huyo kwa mganga wa kienyeji na wapiga ramli,bali wapelekeni hospitalini wakapatiwe matibabu ya kitaalam zaidi.
Alisema serikali kupitia hospitali zake kuna wataalamu wa kutosha kwa ajili ya magonjwa ya afya ya akili,hivyo hakuna sababu ya kuwapeleka watu wanaongudulika kuwa na tatizo hilo.
Awali akizungumza na wakazi hao wa kijiji hicho pia amewashauri wakulima kuhakikisha wanaandaa mashamba yao mapema ikiwemo na kuweka mbolea kwa ajili ya maandalizi ya kupanda mbegu kwa wakati.
Naye Mchungaji Saiman Sandiya ambaye kiongozi wa kanisa hilo la Pentecostal Holiness Association Mission Tanzania PHAM (T) Usharika wa Yerusalemu Chalinze Nyama Chamwino.
Kwa upande wake amewataka wazazi na walezi ambao wana wanafunzi waliomaliza elimu ya msingi kuwaendeleza kielimu zaidi badala ya kuwaweka majumbani.
Sandiya ambaye ametimiza miaka 40 ya uchungaji kwa kumtumikia Mungu,alisema kuwa wanafunzi hao wanatakiwa kuwaendeleza kielimu ikiwemo na kwenye vyuo vya ufundi na kwa kufanya hivyo watakuwa wamewawekezea taaluma.
Alisema kuwa watoto hao wakianchwa bila kuendelezwa taifa litakuwa na tabaka la vijana wanaoweza kujikuta wakijiingiza kwenye makundi maovu kama vile panya road na mengineyo.
Mwisho.
WADAU WA MAENDELEO WAHIMIZWA KUCHANGIA VIFAA VYA MISAADA YA KIBINADAMU WAKATI WA MAAFA.
Na Mwandishi wetu- Kilimanjaro
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga amewahimiza wadau wa maendeleo na watu binafsi kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kuchangia vifaa vya misaada ya kibinadamu wakati wa maafa.
Mhe. Ummy aliyasema hayo alipofanya ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua ghala la kuhifadhi vifaa vya misaada ya kibinadamu wakati wa maafa Kanda ya Kaskazini lililopo maeneo ya Chekereni, Wilaya ya Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro.
Alisema uungwaji mkono wa serikali kutoka kwa wadau unasadia wananchi kufikiwa na huduma kwa haraka kutokana na majanga yaliyojitokeza ambayo husabababisha madhara kama vifo, ulemavu wa kudumu, mali kuharibika pamoja na miundombinu.
“Nitoe wito kwa wadau na watu mbalimbali ambao wanaguswa kushirikiana na serikali kwa kutoa vifaa wafanye hivyo pengine ngaji ya Wilaya, Mkoa na hata kijiji ili tuwe navyo vya kutosha ili yanapotokea tunatoa msaada kwa haraka,” alihimiza Mhe. Ummy.
Pia Mhe. Ummy alisisitiza utunzwaji wa magahala hayo hatua itakayosaidia vifaa hivyo kudumu kwa muda mrefu na kuwa tayari kutumika pindi vinapohitajika katika maeneo yenye maafa.
Aidha aliupongeza uongozi wa mkoa wa Kilimanjaro kwa utayari wa kutoa msaada wa kibinadamu kwa wananchi wanaokumbwa na maafa kwa lengo la kuwasaidia kurejea katika hali yao ya awali.
Kwa upande wake Mwakilishi wa Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Kilimanjaro ambaye ni Afisa Mifugo katika Mkoa huo Bwa. James Shao alisema ghala la Kanda ya Kasikazini linahudumia Mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Tanga.
Naibu
Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga
akizungumza wakati alipotembellea na kukagua ghala la kuhifadhi vifaa vya
msaada wa kibinadamu wakati wa maafa
lililopo mkoani Kilimanjaro.
![]() | ||||
| Afisa Ugavi Sekretarieti ya Mkoa wa Kilimanjaro Bwa. Claude Kilala akitoa maelezo kwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu ) Mhe. Ummy Nderiananga alipotembelea ghala hilo. |

Naibu
Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga
akikagua ghala la kuhifadhi vifaa vya msaada wakati wa maafa lililopo mkoani
Kilimanjaro.
























