Subscribe Us

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

UZINZI NA UASHERATI NI VYANZO VYA VIFUNGO VYA NGUVU ZA GIZA KWENYE MAISHA YA MTU



“Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu”.

Waebrania 13:4

 Siku zote mtu hutumikia adhabu ya kifungo na yapo madhara makubwa yatokanayo na vifungo vya uzinzi na uasherati

 UZINZI ni kufanya tendo la ndoa nje ya agano la ndoa kwa mtu aliye katika ndoa

UASHERATI ni kushiriki tendo la ndoa kabla ya ndoa

BAADHI YA VIFUNGO VITOKANAVYO NA UZINZI NA UASHERATI

(1) - Kuungwa na kuwa mwili mmoja na kahaba 

“Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja”.

1 Wakorintho 6:16

Unapofanya uzinzi au uasherati si tu unafanya dhambi bali pia roho zilizo ndani ya mtu uliyefanya naye uzinzi au uasherati zinaingia ndani mwako pia 
“Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu”.

1 Wakorintho 7:14

✓ Kama ana mapepo hayo mapepo yanaingia ndani yako

✓ Akiwa na roho ya kukataliwa na wewe unaanza kukataliwa

✓ Akiwa na roho ya kutokufanikiwa na wewe unaanza kutokufanikiwa

✓ Kila roho atakayokuwa nayo na wewe unakuwa nayo

✓ Ukizini na jini unakuwa mwili mmoja na jini

(2) - Unapoteza kibali na unakuwa mtu wa kukataliwa, kuzarauliwa unakuwa kitu kichafu 

“Bwana ndiye mwenye haki; Maana nimeiasi amri yake; Sikieni, nawasihi, enyi watu wote, Mkayatazame majonzi yangu; Wasichana wangu na wavulana wangu Wamechukuliwa mateka”.

Maombolezo 1:18

(3) - Unaiua nafsi yako na kupelekea kukosa akili 

“Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake”.

Mithali 6:32

(4) - Nafsi inakamatwa na kufungwa 
“Maana kwa malaya mtu hutiwa katika hali ya kuhitaji kipande cha mkate; Na kahaba humwinda mtu anase nafsi yake iliyo ya thamani”

Mithali 6:26

(5) - Unaharibu nguvu ya agano la ndoa na kupelekea kutokua na ndoa imara, very kutokuolewa, kuvunjika kwa ndoa na kuachana.
6 Unafungua mlango wa mauti kwenye maisha yako kwenye kazi zako roho ya mauti inaanza kukuandama
Unafungulia mlango wa magonjwa ndani yako.
Uasherati haiombewi inahitaji uikimbie mpendwa subiri hadi uingie kwenye ndoa na yule wa kwako uliyekusudiwa na Mungu.




 

SERIKALI YASISITIZA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KATIKA ULINZI NA UFUATILIAJI MIENENDO YA WANYAMAPORI

Na. Mwandishi wetu Morogoro


Serikali Kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imesema itaendelea kutumia teknolojia ya kufuatilia mienendo ya wanyamapori katika maeneo ya hifadhi kwa kuwa imesaidia kwa kiasi kikubwa katika kutambua mienendo ya wanyamapori mbalimbali wakiwemo wale walio hatarini kutoweka na wanaosababisha migogoro kwenye jamii.


Kauli hiyo imetolewa leo mkoani Morogoro na Waziri wa Maliasili na Utalii,  Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana  alipokua akizindua  zoezi la Kuvisha Mikanda yenye Redio za Mawasiliano kwa wanyamapori linalofanywa na Watalaam kutoka Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania ( TAWIRI)  lililofanyika katika Hifadhi ya Taifa ya Mikumi ambapo jumla ya makundi 53 ya wanyamapori  yanatarajiwa kifungwa mikanda hiyo nchi nzima.

"Katika kufuatilia mienendo ya wanyamapori waliohatarini kutoweka, teknolojia hii husaidia kutambua uwepo wao,  mienendo na mtawanyiko katika mifumo ikolojia yao. Utambuzi huu husaidia katika kuimarisha nyanda za malisho na ulinzi." amesema Balozi Dkt . Chana 

Amesema  kwa upande wa wanyamapori waharibifu, teknolojia hiyo husaidia kutambua makundi na mienendo yao na kutoa taarifa mapema  kuhusu uwepo wa makundi hayo nje ya hifadhi na kichukua hatua kabla ya hayajasababisha madhara. 

"Taarifa hizi husaidia katika kupanga mbinu muafaka za kukabiliana na wanyamapori hao. " amesisitiza Balozi Dkt. Chana 

Katika hatua nyingine ameeleza kuwa zoezi hilo alilolizindulia limelenga kuimarisha uhifadhi na utalii kusini mwa Tanzania hususan katika Hifadhi za Taifa za Nyerere, Ruaha na Mikumi akifafanua kuwa litasaidia kwa kiwango kikubwa katika kupunguza migogoro baina ya jamii zinazozunguka hifadhi.  "Jumla ya makundi ya wanyamapori 53 yatafungwa mikanda hii yenye redio za mawasiliano katika hifadhi hizi tatu." amesisitiza Balozi Dkt. Chana

Sambamba na hayo, Waziri Balozi Dkt. Pindi Chana ameongeza kuwa wanyamapori  watakaofungwa mikanda hiyo ni  pamoja na makundi ya tembo, simba, chui, duma, mbwa mwitu na twiga. 

Aidha, taarifa na takwimu hizo zitasaidia kuandaa ramani za mitawanyiko ya wanyamapori  katika misimu na nyakati mbalimbali ambazo zitasaidia kufungua njia mpya za utalii “tourism circuits” pamoja na kuimarisha uhifadhi wa wanyamapori katika hifadhi hizo.

Naye Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii, Prof. Eliamani Sedoyeka amesema Tekinolojia hiyo itasaidia kuwalinda Wanyamapori na Hifadhi zetu hapa nchini. Pia, itasaidia kufuatilia mienendo ya Wanyamapori hai na kuweza kuwaona kidijitali pindi wanapotaka kuleta madhara.

"Kwa kutumia tekinolojia hii tunaweza kuwaona kidijitali wanapotembea na hasa wanapokaribia maeneo hatarishi ya kuleta madhara kwa wananchi"
 
    
Waziri wa Maliasili na Utalii,  Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana  alipokua akizindua  zoezi la Kuvisha Mikanda yenye Redio za Mawasiliano kwa wanyamapori 



 

 

BODI YA MAZAO MCHANGANYIKO NCHINI [CPB] IMEWATOA HOFU WAKULIMA WA MAZAO YA KUNDE


 

Na. Mwandishi wetu Simiyu

 

Bodi ya mazao mchanganyiko nchini (CPB) imesema kuwa wakulima nchini wenye mazao aina ya kunde, hawana sababu ya kuhangaika na soko la mazao yao kwani Bodi hiyo inao uhitaji mkubwa wa mazao hayo.

Ofisa Masoko wa Bodi hiyo Frank Bubelwa Akizungumza katika maonyesho ya wiki ya Chakula nchini yanayoendelea Mkoani Simiyu, amesema kuwa wakulima hawana sababu ya kuangaika na kutafuta wapi watauza mazao yao. Amesema serikali kupitia wizara ya kilimo, mazao na nafaka tumeona tuingie, tufungue milango kwa wakulima kwa kuweza kununua mazao yao yote ambayo wanalima na kuleta kwetu sisi inamaana kwa lugha nyepesi tunawasaidia kutoka katika changamoto ambayo walikuwa wananung’unika kupata masoko.

 

Aidha ameongeza kuwa mbali na Bodi hiyo kununua mazao kutoka kwa wakulima, bado bei ambazo wamekuwa wakinunulia mazao hayo ni rafiki kwa wakulima Lakini pia katika swala zima la bei za nafaka sisi kama taasisi sio taasisi kandamizi mkulima anapewa fursa na tunampa fedha inayoendana na bei ya sokoni mara nyingi wakulima wanakuwa na changamoto hiyo kubwa, unakuta mkulima anakuja kudalaliwa na mtu wakati kwa bei ya chini ambayo inamfanya yeye hasipate hamu au mtaji wake unaguswa kwaiyo anashindwa kufanya shughuli za kilimo. Sambamba na hilo afisa masoko Frank Bubelwaa amesema  kuwa katika msimu wa kilimo bodi ya nafaka huwa tunaangalia pande zote mbili mkulima hasiumie pia sisi tusipate hasara kwaiyo mara nyingi tunanunua mali kutokana na bei iliyo sokoni kama kwamfano kilo moja ya mahalage ni silingi elfu mbili sokoni sisi tutakuja kununua kwa bei hiyohiyo hatuwezi tukashuka Zaidi ya hapo. Hivyo basi sisi tupo kwaajiri ya kuhakikisha kuwa kilimo kinaendelea kukua lakini pia kwaupande mwingine kuongeza uchumi wa nchi.

 

maonyesho ya wiki ya Chakula nchini yanayoendelea Mkoani Simiyu
 

 

 

 

 

 

 

MIAKA 7 YA BMH: MKURUGENZI AELIMISHA KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE



 Na. Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano Hospitali ya Benjamin Mkapa





Hospitali ya Benjamin Mkapa Dodoma leo Oktoba 13, imetimiza miaka saba tangu ilipoanza kutoa huduma za Afya Oktoba 13, 2015.

 

Mkurugenzi Mtendaji Dkt, Alphonce Chandika amewajengea uwelewa juu ya Msuada wa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote wananchi waliyofika kupata huduma, ambapo mesema  lengo la Mswada huo ni kuhakikisha, kila mwananchi anakuwa na uhakika wa kupata matibabu bila hofu.

 

“Ndugu zangu baadhi yenu mnakuja hapa mara kwa mara kupata huduma, mnafahamu ugonjwa haubishi hodi, bila kuwa na BIMA kuna wenzetu hulazimika kuuza hata viwanja au nyumba wagharamie matibabu” Alidokeza, Dkt. Chandika.

 

Aidha, alifafanua kuwa mantiki ya Mswaada wa BIMA ya Afya kwa wote ni kuhakikisha kuwa, watu wengi wanachangia gharama za matibabu kabla hawajafikwa na maradhi ili kutunisha mfuko hatimae mtu akiugua asikutane na changamoto yoyote ya kukosa huduma kwa kushindwa kulipia gharama za matibabu.

 

“Msingi wa BIMA ya Afya kwa wote, ni suala la upendo zaidi, na baba wa Taifa Mwalimu Nyerere tunaeadhimisha  siku yake kesho alitufundisha kupendana, hivyo tunapochangia wengi, wakaugua baadhi tunakuwa tumewasaidia” Alifafanua Dkt. Chandika.

 

Vile vile, alieleza kuwa mapendekezo ya Mswada huo ni kwa kaya moja kuchangia Shilingi 340,000 na kunufaisha wanafamilia sita, huku mtu mmoja akitakiwa kuchangia kiasi cha shilingi 84,000 ili kupata huduma za Afya kwa mwaka mzima.

 

“Nasisitiza kuwa serikali haina lengo la kumlazimisha mtu kuchangi, bali itaweka mazingira rafiki yatakayomsukuma kila mmoja kuona umuhimu wa kuchangia, na kwa kutumia mifumo ya TASAF na Ustawi wa jamii itawatambua wasiyojiweza na kuwatengenezea mfumo wa kupata matibabu bila usumbufu” Alisema Dkt. Chandika.

 

 

Shamrashamra za kutimiza miaka hiyo saba zimeanza saa mbili asubuhi ya leo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo Dkt. Alphonce Chandika kushiriki kutoa huduma za msingi kwa wagonjwa, aliwapokea, kuzungumza nao na kuwasaidia waliyohitaji kutembea kwa msaada wa kiti maalumu (Wheelchair).

 

Kisha aliwashukuru wananchi waliyofika Hospitalini hapo kwa kutoa mchango wao wa maoni, ambayo hupokewa na kufanyiwa kazi kwa wakati na ndiyo umekuwa msingi wa maboresho mbalimbali ya huduma katika Hospitali hiyo kiasi cha kuifanya kutambuliwa kama kinara kwa Utoaji wa huduma bora za Afya kwa Hospitali zote nchini.

 

Kwa asubuhi ya leo, sherehe hizo ziliahanikizwa na ukataji wa keki  maalumu ya miaka saba ya huduma katika Hospitali hiyo, ambayo ilikatwa kwa ushirikiano wa Mteja na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo.

 

Baadaye alielekea katika wodi ya watoto wachanga na kutoa zawadi mabalimbali kwa watoto hao kama sehemu ya kurejesha kwa jamii.






Mkurugenzi Mtendaji Dkt, Alphonce Chandika akizungumza na wanainchi waliyofika kupata huduma   juu ya Msuada wa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote.

WAZIRI WA SHERIA DKT DAMAS NDUMBARO AMETOA UFAFANUZI KUHUSU WANAFUNZI WA SHERIA KUFELI MAFUNZO KWA VITENDO

Na. Kadala Komba Dodoma 
 
 
 
Kumekuwa na sintofahamu  kuhusiana na matokeo ya Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST), mjadala ulioibuka katika sehemu  mbalimbali kwamba kwa nini wanafunzi hao wanafeli sana. Mjadala huu sio mpya, ni wa muda mrefu.

Historia ya wanafunzi  wachache kufaulu mitihani ya Taasisi hii haijaanza leo, ni ya siku nyingi, lakini hailengi kumkomesha mtu yoyote bali inalenga kuweka viwango vya juu.

Waziri wa katiba na Sheria Dkt Damas Ndumbaro amezungumza haya katika kikao na waandishi wa habari jijini Dodoma alisema Vinawekwa viwango vya juu kwa sababu Sheria ni jambo muhimu katika utawala bora, utawala wa Sheria, kuleta amani na utulivu pamoja na utoaji wa haki, hivyo ni lazima tuwe na imani na wanasheria tunaowapa jukumu hilo,
Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania ina Walimu 95 ambapo Walimu 14 kati yao waliobobea katika maeneo mbalimbali ya Sheria wameajiriwa  ajira ya kudumu. 

Kwa uhalisia wa kazi hii hufanyika kwa vitendo, Walimu wengi  wanaochukuliwa ni wataalam waliobobea kwenye maeneo yao ambapo kati ya Walimu 81, Walimu 10 ni Majaji. Kati ya Majaji kumi, watatu ni Majaji ambao bado wako kazini na Majaji saba ni wastaafu ambao wana uzoefu wa kutosha.

Katika orodha ya Walimu 81, Walimu wanne ni Mawakili wa Serikali ambao wengi wamekaa muda mrefu katika nafasi zao na wana uzoefu wa kutosha na Walimu 56 ni Mawakili wa kujitegemea waliobobea katika kazi zao.

 Tangu Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania imeanzishwa, wanafunzi 8,255 kati ya wanafunzi 13,974 wamefaulu sawa na asilimia 59.074 na wanafunzi waliofeli baadhi ya masomo ambao wanaruhusiwa kurudia masomo hayo ni asilimia 21.619.

Takwimu zinaonesha kuwa, asilimia kubwa ya wanaorudia baadhi ya masomo waliyofeli huwa wanafaulu, hivyo ufaulu kwa ujumla utakuwa kwenye asilimia 81.

Kwa takwimu hizi za ufaulu, asilimia ya waliofeli kabisa ni asilimia 19 kati ya asilimia 100 ambayo ni asilimia ndogo na inatokea kokote duniani.

Kama kuna mwanafunzi anayehisi ameonewa, kuna mfumo wa kukata rufaa ambao upo na unafanya kazi.

Serikali imeunda Kamati ya watu saba ambayo imepewa siku 30 kuleta taarifa juu ya tuhuma hizi.  Kamati hii haijahusisha Waalimu wala Mstaafu yeyote wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo (LST) wala Walimu kutoka Vyuo vinavyotoa elimu ya sheria, tumehusisha wadau wengine ili walete majibu ya ukweli na yenye tija.
 

 

WAKATI WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA, DKT. DAMAS NDUMBARO AKITOA UFAFANUZI MBELE YA WAANDISHI WA HABARI JIJINI DODOMA KUHUSU WANAFUNZI WA SHERIA KUFELI MAFUNZO KWA VITENDO*



 

WAZIRI PINDI CHANA AZINDUA BODI YA WAKURUGENZI TAWA



Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana leo tarehe 12 Oktoba, 2022 amezindua Bodi ya Wakurugenzi ya TAWA aliyoiteua hivi Karibuni.

Akizungumza katika hafla ya Uzinduzi iliyofanyika Makao Makuu ya TAWA Mkoani Morogoro, Dkt. Chana amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kwa kumteua Mwenyekiti wa Bodi  ya TAWA na kuwapongeza wajumbe Wote wa Bodi hiyo kuteuliwa  kuiongoza TAWA.

"Nichukue nafasi hii Kumshukuru sana Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Kwa kumteua "Chairman" (Mwenyekiti) wetu Mej. Jen.(Mstaafu) Hamis Semfuko asante sana ametuletea "Chairman" hodari kabisa na Kwakweli tuna matumaini makubwa sana na wewe" amesema

"Kwa dhati kabisa nawapongeza Wakurugenzi wa Bodi wote Kwa kuteuliwa kuiongoza Bodi hii ya TAWA" ameongeza.

Dkt. Pindi Chana amesema uteuzi wa bodi hiyo umefanyika Kwa umakini mkubwa na kuzingatia weledi  na uzoefu wa wakurugenzi hao ambao utaisaidia taasisi hiyo kufikia malengo hususani katika utekelezaji wa mikakati ya kuzuia ujangili, kuongeza idadi ya watalii na mapato na hivyo kuendeleza sekta ya Wanyamapori.

Aidha Waziri Pindi Chana ametoa rai Kwa bodi hiyo Kuweka mikakati ya Changamoto ya ongezeko la matukio ya Wanyamapori wakali na Waharibifu na uvamizi wa mifugo hifadhini.

Sambamba na hilo, Mhe. Dkt. Chana amewataka watu wenye tabia ya kuingiza mifugo ndani ya hifadhi kuacha vitendo hivyo mara moja.

"Nitumie nafasi hii kuushirikisha Umma kwamba maeneo ya hifadhi zetu siyo maeneo ya kulishia mifugo, haya ni maeneo ambayo tunapaswa kuyalinda Kwa maslahi ya Wote" amesema

Dkt. Chana ameongeza vitendo vya kuingiza mifugo hifadhini vinaleta athari kubwa  Kwa kukausha vyanzo vya maji, kuharibu mazingira na athari zake kuwa kubwa Kwa Taifa, hivyo amewaomba wananchi washirikiane na Serikali katika kuhifadhi maeneo yaliyohifadhiwa Kwa lengo la uhifadhi Kwa maslahi ya Nchi yetu.

Mbali na shughuli ya Uzinduzi wa Bodi, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana alizindua mitambo mbalimbali iliyonunuliwa na TAWA Kwa fedha za UVIKO - 19 ambayo ni mashine za kuchima visima vya maji, matreka, "caterpillars", boti maalumu kwa ajili ya doria n.k

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii, Prof. Elaimani Sedoyeka amesema TAWA ina maeneo makubwa  takribani asilimia 10 ya maeneo yote Nchini, hivyo anatumaini kwamba itabuni mikakati mbalimbali ya kuongeza idadi ya watalii, mapato na kuimarisha shughuli za Uhifadhi, kuboresha miundombinu ya Utalii, kujenga uwezo wa watumishi pamoja na matumizi ya teknolojia katika kuongeza ufanisi na tija kiutendaji.

Akielezea mikakati ya Bodi mpya ya TAWA, Mwenyekiti wa Bodi Mej. Jen. (Mstaafu) Hamis Semfuko amesema mkakati wa kwanza ambao Bodi itaupa kipaumbele ni kupunguza migongano kati ya watu na Wanyamapori "Human Wildlife Conflicts" Ili kuhakikisha TAWA inakuwa chombo ambacho kinakuwa na faida Kwa Serikali na Umma.

Kamishna wa Uhifadhi TAWA ambaye pia ni Katibu wa Bodi iliyozinduliwa leo, Mabula Misungwi Nyanda amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Kwa kumteua Mej. Jen. Mstaafu Hamis Semfuko kwa awamu nyingine Ili aendelee kufanikisha kazi kubwa aliyokwisha ianzisha.

Aidha amempongeza Mwenyekiti huyo Kwa kuendelea kuaminiwa na kuteuliwa kuiongoza TAWA na kumuahidi ushirikiano Wakati Wote wa utekelezaji wa majukumu ya Bodi Ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.
 
 
Waziri wa Maliasili na Utalii Mhe. Balozi Dkt. Pindi Akizungumza katika hafla ya Uzinduzi iliyofanyika Makao Makuu ya TAWA Mkoani Morogoro
 

 

SERIKALI INAENDELEA KUWEKEZA KWA WATAALAMU WA NDANI WA MIFUMO

Na WAF - DSM

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalaghe amesema kuwa, Serikali itaendelea kuwekeza kwa Wataalamu wa ndani wa mifumo ili kuhakikisha miradi yote inayoanzishwa na Wafadhili inaendelea kusimama siku Wafadhili wanapomaliza muda wao. 

Dkt. Shekalaghe ameeleza hayo, katika majadiliano ya pamoja yaliyoandaliwa na Wizara ya Afya na OR TAMISEMI kwa kushirikiana na Wadau kutoka Shirika lisilo la Kiserikali la PATH linalotekeleza mradi wa "matumizi ya sahihi ya takwimu" (Data Use Patnership - DUP) yaliyofanyika usiku wa Oktoba 12, 2022 Jijini Dar es Salaam. 

Amesema, Serikali inaendelea kuhimiza matumizi ya mifumo katika maeneo mbalimbali, hususan katika vituo vya kutolea huduma za afya kwa wananchi kwani inasaidia kuongeza ufanisi wa utendaji na itasaidia kupata takwimu sahihi na kwa wakati ambazo zitasaidia katika kupanga matumizi sahihi na udhibiti wa magonjwa. 

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu anaeshughulika na masuala ya Afya OR TAMISEMI Dkt. Grace Magembe amesema, ili nchi ipige hatua kwa kasi ni muhimu mifumo ipewe kipaumbele kwani inasaidia kufanya ufuatiliaji na kuongeza utendaji katika maeneo ya kazi na kuepuka gharama zisizo za lazima. 

Aidha, Dkt. Magembe amesema, licha ya kazi kubwa kufanyika katika kuboresha mifumo nchini bado ipo haja ya kuongeza kasi ya uwekezaji katika eneo hilo ili mifumo iweze kuwasiliana baina ya mfumo wa hospitali moja kwenda hospitali nyingine (interoperability), jambo litalosaidia kupunguza gharama kwa mwananchi kwa kuepuka kurudia kufanya vipimo.

Aliendelea kusisitiza kuwa, ni muhimu Wadau kuendelea kushirikiana kwa ukaribu zaidi na Serikali katika kuboresha Sekta ya Afya nchini kupitia matumizi ya mifumo ili kupunguza matumizi ya taarifa za makaratasi, hali inayohatarisha usalama wa taarifa hizo na takwimu katika maeneo ya kutolea huduma. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mradi wa Data Use Patnership (DUP) Dkt. Seif Rashid amesema, matumizi sahihi ya takwimu yanasaidia kufanya maamuzi sahihi, hususan katika kutenga fedha na rasilimali watu kwa usahihi na kwa wakati kulingana na mahitaji. 

Nae, Mkurugenzi wa Tehama OR-TAMISEMI Bw. Eric Kitali amewataka Mashirika na Taasisi kutoka nchini kupenda kuwatumia Wataalamu wa ndani kutengeneza mifumo yao ili kutunza taarifa za taasisi zao, pia kufanya hivyo ni ishara ya uzalendo.

"Tupende vya nyumbani, tupende mifumo inayotengenezwa na Wataalamu kutoka ndani ya nchi, pia itasaidia kuongeza usalama."Amesema. 

Mwisho.
 
 
 

 
 

 

 

MCHUNGAJI AWATAKA WAGONJWA WANAONGUDULIKA NA TATIZO LA AFYA AYA AKILI WAPELEKWE HOSPITALI BADALA YA KWA WAGANGA WAKIENYEJI.

Na Peter Mkwavila CHAMWINO.

 

 

ASKOFU wa kanisa la Pentecostal Holiness Association Mission Tanzania PHAM (T) Kanda ya Kati Brayson Msanjila,amewashauri familia zinazogundulika kuwa na wagonjwa wa afya ya akili waache tabia ya kuwapeleka kwa waganga wa kienyeji na wapiga ramli.badala yeke wawapeleke kwenye vituo vya afya ili wakapime afya zao kitaalamu zaidi.

 

Msanjila amesema hayo alipokuwa apokuwa akizungumza na wakazi wa kijiji cha Chalinze nyama wilaya ya Chamwino kwenye ibada iliyoandaliwa kwa ajili ya kumpongeza mchungaji Saimon Sandiya aliyetimiza  miaka 40 toka awe kwenye utumishi wake,

 

Ibada hiyo iliyofanyika katika kanisa la   Pentecostal Holiness Association Mission Tanzania PHAM (T) Usharika wa Yerusalemu Chalinze Nyama Chamwino.

 

Askofu ameziomba familia hizo pindi zinapotokea kuwepo kwa mgonjwa wa afya ya akili,ni vizuri akapelekwa hosptalini badala ya huko kwa waganga na kwa wapiga ramli.

 

Alisema kuwa tatizo la afya ya akili likipatiwa matibabu haraka kwa asilimia kubwa linatibika haraka tofauti kama mgonjwa huyo akipelekwa kwa waganga wa kienyeji.

 

“Hivyo niziombe familia hususah huku vijijini pindi mnapogundua kuna tatizo hilo miongoni mwenu acheni kumkimbiza mgonjwa huyo kwa mganga wa kienyeji na wapiga ramli,bali wapelekeni hospitalini wakapatiwe matibabu ya kitaalam zaidi.

 

Alisema serikali kupitia hospitali zake kuna wataalamu wa kutosha kwa ajili ya magonjwa ya afya ya akili,hivyo hakuna sababu ya kuwapeleka watu wanaongudulika kuwa na tatizo hilo.

Awali akizungumza na wakazi hao wa kijiji hicho pia amewashauri wakulima kuhakikisha wanaandaa mashamba yao mapema ikiwemo na kuweka mbolea kwa ajili ya maandalizi ya kupanda mbegu kwa wakati.

 

Naye Mchungaji Saiman Sandiya ambaye kiongozi wa kanisa hilo la Pentecostal Holiness Association Mission Tanzania PHAM (T) Usharika wa Yerusalemu Chalinze Nyama Chamwino.

 

Kwa upande wake amewataka wazazi na walezi ambao wana wanafunzi waliomaliza elimu ya msingi kuwaendeleza kielimu zaidi badala ya kuwaweka majumbani.

 

Sandiya ambaye ametimiza miaka 40 ya uchungaji kwa kumtumikia Mungu,alisema kuwa wanafunzi hao wanatakiwa kuwaendeleza kielimu ikiwemo na kwenye vyuo vya ufundi na kwa kufanya hivyo watakuwa wamewawekezea taaluma.

 

Alisema kuwa watoto hao wakianchwa bila kuendelezwa taifa litakuwa na tabaka la vijana wanaoweza kujikuta wakijiingiza kwenye makundi maovu kama vile panya road na mengineyo.

Mwisho.


 

 

WADAU WA MAENDELEO WAHIMIZWA KUCHANGIA VIFAA VYA MISAADA YA KIBINADAMU WAKATI WA MAAFA.

 

Na Mwandishi wetu- Kilimanjaro

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga amewahimiza wadau wa maendeleo na watu binafsi kuendelea kushirikiana na Serikali kwa kuchangia vifaa vya misaada ya kibinadamu wakati wa maafa.

Mhe. Ummy aliyasema hayo alipofanya ziara ya kikazi ya kutembelea na kukagua ghala la kuhifadhi vifaa vya misaada ya kibinadamu wakati wa maafa Kanda ya Kaskazini  lililopo maeneo ya Chekereni, Wilaya ya Moshi Vijijini mkoani Kilimanjaro.

Alisema uungwaji mkono wa serikali kutoka kwa wadau unasadia wananchi kufikiwa na huduma kwa haraka kutokana na majanga yaliyojitokeza ambayo husabababisha madhara kama vifo, ulemavu wa kudumu, mali kuharibika pamoja na miundombinu.

“Nitoe wito kwa wadau na watu mbalimbali ambao wanaguswa kushirikiana na serikali kwa kutoa vifaa wafanye hivyo pengine ngaji ya Wilaya, Mkoa na hata kijiji ili tuwe navyo vya kutosha ili yanapotokea tunatoa msaada kwa haraka,” alihimiza Mhe. Ummy.

Pia Mhe. Ummy alisisitiza utunzwaji wa magahala hayo hatua itakayosaidia vifaa hivyo kudumu kwa muda mrefu na kuwa tayari kutumika pindi vinapohitajika katika maeneo yenye maafa.

Aidha aliupongeza uongozi wa mkoa wa Kilimanjaro kwa utayari wa kutoa msaada wa kibinadamu kwa wananchi wanaokumbwa na maafa kwa lengo la kuwasaidia kurejea katika hali yao ya awali.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Kilimanjaro ambaye ni Afisa Mifugo katika Mkoa huo  Bwa. James Shao alisema ghala la Kanda ya Kasikazini linahudumia Mikoa ya Arusha, Manyara, Kilimanjaro na Tanga.

 


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga akizungumza wakati alipotembellea na kukagua ghala la kuhifadhi vifaa vya msaada  wa kibinadamu wakati wa maafa lililopo mkoani Kilimanjaro.

 

Afisa Ugavi Sekretarieti ya Mkoa wa Kilimanjaro Bwa. Claude Kilala akitoa maelezo kwa Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu ) Mhe. Ummy Nderiananga alipotembelea ghala hilo.    
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga (aliyeinama) akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Nurdin Hassan Babu (kulia)

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga akikagua ghala la kuhifadhi vifaa vya msaada wakati wa maafa lililopo mkoani Kilimanjaro.
      

 
 
Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Ummy Nderiananga (wa tatu kushoto) akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya watendaji kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro na Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Mkoa huo.