Subscribe Us

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

*WIZARA YA KATIBA KUTOA HUDUMA ZA KISHERIA KIDIJITALI – DKT NDUMBARO*



Na. Mwandishi wetu Arusha 
 
 
 
Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro amesema Wizara ya Katiba na Sheria imekusudia kuhakikisha huduma za kisheria zinazotolewa na Wizara na Taasisi zilizo chini yake zinapatikana kwa njia ya TEHAMA. 

Dkt. Ndumbaro ameyasema hayo wakati akifungua warsha ya siku mbili kwa Wasajili Wasaidizi wa Watoa Huduma za Msaada wa Kisheria, Wasaidizi wa Kisheria, Mawakili, Wanasheria na Maafisa wa Jeshi la Magereza ambayo inafanyika kuanzia leo Oktoba 17, 2022 Jijini Arusha.

Dkt Ndumbaro amesema “Kwa kutambua umuhimu wa TEHAMA kwenye utoaji wa huduma, Wizara ya Katiba na Sheria imekusudia kuhakikisha huduma za kisheria zinazotolewa na Wizara na Taasisi zilizo chini yake zinapatikana kwa njia ya TEHAMA. Hili litawezesha huduma kupatikana kwa wakati na hatimaye kuwezesha vyombo vingine vya utoaji haki kutoa haki kwa wakati na kwa gharama nafuu.”

Dkt. Ndumbaro ameongeza kuwa TEHAMA imekuwa na mchango mkubwa kwenye utoaji wa huduma na utendaji wa Serikali kwa ujumla. Faida zinazopatikana ni pamoja na  kuwepo kwa utunzaji wa kumbukumbu sahihi za wananchi, kuweka  uwazi na uwajibikaji wa utoaji huduma hususan panapokuwa na malalamiko kutoka kwa wananchi, kurahisisha upatikanaji wa huduma, na vilevile kuondoa mianya ya rushwa kwenye utoaji huduma kwa kuwa  hakuna mwingiliano kati ya mtoa huduma na mteja.

Dkt. Ndumbaro alisisitiza kuwa ni vyema kuwa na mifumo mizuri ya kisheria ambayo itarahisisha upatikanaji wa haki kwa wakati; mifumo ambayo itawezesha wananchi kupata huduma za kisheria popote walipo kwa gharama nafuu katika kuifikia haki. Uwepo wa mifumo, utawapunguzia wananchi muda na gharama za kushughulikia masuala ya kisheria na badala yake watajikita zaidi katika shughuli zingine za kiuchumi na kimaendeleo hivyo basi kuleta maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Aidha, Dkt. Ndumbaro aliongeza kuwa Wizara ina jukumu kubwa la kutoa elimu ya Katiba  na Sheria kwa wananchi hususan vijana kwani hiyo itawasaidia kujua sheria na kudai haki zao.

Dkt. Ndumbaro amesema “Naamini kwamba Wizara ina jukumu kubwa la kutoa elimu ya Katiba kwani huwezi kwenda kutoa kitu kipya wakati hujui cha zamani, tupate elimu ya Katiba iliyopo sasa ili tujue mazuri yakwenda nayo katika Katiba mpya na kuacha mabaya yaliyopo.”

Akimkaribisha Waziri Ndumbaro kufungua warsha hiyo, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Bw. David Lyamongi amesema Wasaidizi wa kisheria wapewe kipaumbele katika kutekeleza kazi zao kwani wanasaidia sana jamii hasa wajane na yatima.

Bw. Lyamongi amesema “mchango wa Wasaidizi wa Kisheria ni mkubwa sana katika jamii hususan katika Mkoa wa Arusha kwenye masuala ya kisheria yaliyomshinda mwananchi au kushindwa kwenda mwenyewe mahakamani hivyo kuhitaji uwakilishi.”

Msajili wa Watoa Huduma za Msaada wa Kisheria nchini Bi. Felistas Mushi amesema mafunzo hayo yamewashirikisha Watoa Huduma za kisheria kutoka kwenye Mashirika kumi na tano, Wasajili Wasaidizi na Maafisa Magereza kutoka mikoa kumi ya Tanzania Bara. Washiriki hao wamechaguliwa kwa sababu wapo karibu na wananchi sanjali na kuwasaidia wananchi wengi wa chini waliopo kwenye maeneo yao, alisema Bi. Mushi.

Awali akitoa maelezo ya utangulizi Mkuu wa Kitengo cha TEHAMA Bw. Gabriel Ally amesema mafunzo hayo yatafanyika kwa awamu nne kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

Bw. Gabriel amesema huduma za TEHAMA zinarahisisha kufikisha huduma za kisheria kwa wananchi popote pale walipo hivyo ni muhimu makundi hayo manne yakazingatia mafunzo hayo katika utendaji kazi wao kwa kuwa zinahusiana na wananchi kwa kiasi kikubwa.

Mafunzo haya yanahusisha mifumo inayohusu usajili wa watoa huduma za msaada wa kisheria na wasaidizi wa kisheria ambazo zinatolewa chini ya Sheria ya Msaada wa Kisheria ya Mwaka 2017, mfumo wa usajili wa watoa huduma za maridhiano, usuluhishi, na upatanishi kama ilivyobainishwa chini ya Sheria ya Usuluhishi ya Mwaka 2020.  Mifumo mingine ni pamoja na uwasilishaji wa malalamiko, maombi ya huduma za msaada wa kisheria, maombi ya kuongezewa muda wa kuwasilisha mashauri mahakamani nje ya muda pamoja na huduma nyingine za kisheria.
 
 

 Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro

 

ASKOFU KINYAIYA "WAZAZI PELEKENI WATOTO SHULE"



Na. Kadala Komba Dodoma
 
 
 Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma, Mhashamu Beatus Kinyaiya amewataka wazazi  kuwapeleka watoto shule badala ya kuwapa kazi ya kuchunga Ng'ombe .

Askofu huyo aliyasema hayo hivi karibuni wakati wa misa 
ya Sakramenti ya kipaimara iliyofanyika katika  kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Yohane Mbatizaji Wilaya ya Bahi.

Amesema elimu bora  ni haki ya kila mtoto ambapo hatua hiyo itasaidia watoto kutimiza ndoto zao pamoja na kuongeza pato la familia na kuondokana na umasikini.

"Ni  kweli hizi familia zina utajiri wa mali nyie ni wafugaji wa mifugo na kupitia mifugo mnamiliki mali nyingi lakini mali bila elimu ni shida, wapelekeni watoto shule wakapate elimu darasani, wafundisheni watoto  kusoma pindi wanapokuwa Nyumbani, "Alisema Askofu huyo. 

Pia Askofu Mhashamu aliwasihi watoto kutumia vizuri fursa ya elimu wanapopelekwa shule kwa kusoma bidii  kusoma kwa  bidii  na kutokukubali kukatishwa tamaa. 

Katika hatua nyingine Askofu alipongeza Parokia hiyo kwa juhudi za kimaendeleo ambazo Parokia inaendelea kufanya uhakikisha jamii inakuwa na hofu ya Mungu na maadili. 

 "Parokia hii inakuwa kwa kasi hivyo msikubali kukatishwa tamaa na watu, msije kugeuka nyuma ukigeuka nyuma utakuwa jiwe la chumvi hivyo tunatakiwa kutazama  tulijenge Kanisa, "Alihimiza. 

Kwa upande wake Katibu wa  Halmashauri ya Walei Parokia, Eresta Oiso ameeleza kwamba  jumla ya watoto 1,776 wamepata Sakramenti ya ubatizo, komunio ya kwanza 329 na ndoa 71 zilifungwa pamoja na kutoa  Sakramenti ya kipaimara kwa watoto 301 pamoja na kufungisha ndoa 5.

"Parokia ya Bahi ni miongoni mwa Parokia zilizomo ndani ya Jimbo Kuu Katoliki Dodoma, Dekania ya Mtakatifu Yohane Mbatizaji inapatikana mpakani mwa jimbo kuu Katoliki Dodoma na jimbo la Singida takribani kilomita  55 kutoka Dodoma mjini, "Ameeleza.

Aidha amebainisha kuwa  Parokia ya Bahi ina Jumla ya vigango 13 , Vigango 11 na jumuiya ndogo ndogo za kikristo 155.
 
 
 Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dodoma, Mhashamu Beatus Kinyaiya

 





 MATUKIO YA PICHA YA KIPAIMARA
 
 

 

RAIS SAMIA ATEMBELEA JENGO LA MAKUMBUSHO YA HAYATI DKT.JOHN POMBE MAGUFULI,AKAGUA HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA YA CHATO MKOANI GEITA


  •  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiomba dua kwenye Kaburi la Rais wa Awamu ya Tano Hayati Dkt. John Pombe Magufuli nyumbani kwake Chato Mkoani Geita.
  •  


  •  


KAMPASI YA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM KUJENGWA KAGERA-WAZIRI MKENDA

 

Na Mathias Canal, WEST-Kagera

 

Katika kuboresha huduma za upatikanaji wa elimu kwa wanafunzi nchini Serikali imepanga kujenga Kampasi ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM) Mkoani Kagera.

 

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia amesema hayo mbele ya Mgeni rasmi-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan tarehe 13 Octoba 2022 wakati wa hafla ya uzinduzi wa Chuo kipya cha Ufundi Stadi na Huduma (VETA) cha Mkoa wa Kagera.

 

Amesema kuwa Kampasi hiyo itajengwa kwenye vijiji vya Itahwa na Kangabusharo kwenye eneo la ekari 323.45. Kati ya ekari 323.45 zilizotolewa, ekari 231.36 ziko katika kijiji cha Itahwa na ekari 92.09 katika kijiji cha Kangabusharo.


Akizungumza kuhusu Chuo kipya cha Ufundi Stadi na Huduma (VETA) cha Mkoa wa Kagera, Waziri Mkenda amesema chuo hicho chenye hadhi ya Kimataifa kimejengwa kwa msaada wa Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kwa thamani ya Yuani za Kichina Milioni 60.18 sawa na Shilingi za Kitanzania Bilioni 22.4, Fedha hizo zinajumuisha shughuli za ujenzi, uwekwaji wa baadhi ya vifaa vya kufundishia na kujifunzia, mashine na samani katika majengo.

 

Waziri Mkenda amesema kuwa Chuo hicho chenye karakana, vifaa na miundo mbinu ya kisasa kilichojengwa kwa msaada wa Serikali ya China kitakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi zaidi ya 1,400 kwa mafunzo ya muda mfupi na mrefu katika fani mbalimbali za ufundi na huduma.

 

Waziri Mkenda amesema kuwa Chuo hicho cha Ufundi Stadi na Huduma cha Mkoa wa Kagera kilichozinduliwa na Mhe Rais ni hatua nyingine muhimu katika mpango wa kukamilisha ujenzi wa vyuo vya ufundi stadi vya ngazi ya Mikoa.

 

“Mheshimiwa Rais Tulibakisha mikoa michache sana. Kwa sasa, mikoa mingine ambayo ujenzi unaendelea ni Njombe, Simiyu, Rukwa na Geita na mpango wa ujenzi wa chuo cha Mkoa wa Songwe unaendelea kukamilishwa ili ujenzi uanze” Amekaririwa Prof Mkenda

 

Prof Mkenda amesema kuwa serikali inaendelea na ujenzi wa vyuo vya ufundi stadi vya ngazi ya wilaya ambavyo hadi sasa Wilaya 77 zina vyuo na ujenzi wa vyuo katika Wilaya 62 unatarajiwa kuanza katika mwaka huu wa fedha 2022/23 ambapo Serikali imetenga shilingi bilioni 100.

 

 


Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia

 

 


 

 


 


 

 


UZINZI NA UASHERATI NI VYANZO VYA VIFUNGO VYA NGUVU ZA GIZA KWENYE MAISHA YA MTU



“Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu”.

Waebrania 13:4

 Siku zote mtu hutumikia adhabu ya kifungo na yapo madhara makubwa yatokanayo na vifungo vya uzinzi na uasherati

 UZINZI ni kufanya tendo la ndoa nje ya agano la ndoa kwa mtu aliye katika ndoa

UASHERATI ni kushiriki tendo la ndoa kabla ya ndoa

BAADHI YA VIFUNGO VITOKANAVYO NA UZINZI NA UASHERATI

(1) - Kuungwa na kuwa mwili mmoja na kahaba 

“Au hamjui ya kuwa yeye aliyeungwa na kahaba ni mwili mmoja naye? Maana asema, Wale wawili watakuwa mwili mmoja”.

1 Wakorintho 6:16

Unapofanya uzinzi au uasherati si tu unafanya dhambi bali pia roho zilizo ndani ya mtu uliyefanya naye uzinzi au uasherati zinaingia ndani mwako pia 
“Kwa maana yule mume asiyeamini hutakaswa katika mkewe; na yule mke asiyeamini hutakaswa katika mumewe; kama isingekuwa hivyo, watoto wenu wangekuwa si safi; bali sasa ni watakatifu”.

1 Wakorintho 7:14

✓ Kama ana mapepo hayo mapepo yanaingia ndani yako

✓ Akiwa na roho ya kukataliwa na wewe unaanza kukataliwa

✓ Akiwa na roho ya kutokufanikiwa na wewe unaanza kutokufanikiwa

✓ Kila roho atakayokuwa nayo na wewe unakuwa nayo

✓ Ukizini na jini unakuwa mwili mmoja na jini

(2) - Unapoteza kibali na unakuwa mtu wa kukataliwa, kuzarauliwa unakuwa kitu kichafu 

“Bwana ndiye mwenye haki; Maana nimeiasi amri yake; Sikieni, nawasihi, enyi watu wote, Mkayatazame majonzi yangu; Wasichana wangu na wavulana wangu Wamechukuliwa mateka”.

Maombolezo 1:18

(3) - Unaiua nafsi yako na kupelekea kukosa akili 

“Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake”.

Mithali 6:32

(4) - Nafsi inakamatwa na kufungwa 
“Maana kwa malaya mtu hutiwa katika hali ya kuhitaji kipande cha mkate; Na kahaba humwinda mtu anase nafsi yake iliyo ya thamani”

Mithali 6:26

(5) - Unaharibu nguvu ya agano la ndoa na kupelekea kutokua na ndoa imara, very kutokuolewa, kuvunjika kwa ndoa na kuachana.
6 Unafungua mlango wa mauti kwenye maisha yako kwenye kazi zako roho ya mauti inaanza kukuandama
Unafungulia mlango wa magonjwa ndani yako.
Uasherati haiombewi inahitaji uikimbie mpendwa subiri hadi uingie kwenye ndoa na yule wa kwako uliyekusudiwa na Mungu.




 

SERIKALI YASISITIZA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA KATIKA ULINZI NA UFUATILIAJI MIENENDO YA WANYAMAPORI

Na. Mwandishi wetu Morogoro


Serikali Kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii imesema itaendelea kutumia teknolojia ya kufuatilia mienendo ya wanyamapori katika maeneo ya hifadhi kwa kuwa imesaidia kwa kiasi kikubwa katika kutambua mienendo ya wanyamapori mbalimbali wakiwemo wale walio hatarini kutoweka na wanaosababisha migogoro kwenye jamii.


Kauli hiyo imetolewa leo mkoani Morogoro na Waziri wa Maliasili na Utalii,  Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana  alipokua akizindua  zoezi la Kuvisha Mikanda yenye Redio za Mawasiliano kwa wanyamapori linalofanywa na Watalaam kutoka Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania ( TAWIRI)  lililofanyika katika Hifadhi ya Taifa ya Mikumi ambapo jumla ya makundi 53 ya wanyamapori  yanatarajiwa kifungwa mikanda hiyo nchi nzima.

"Katika kufuatilia mienendo ya wanyamapori waliohatarini kutoweka, teknolojia hii husaidia kutambua uwepo wao,  mienendo na mtawanyiko katika mifumo ikolojia yao. Utambuzi huu husaidia katika kuimarisha nyanda za malisho na ulinzi." amesema Balozi Dkt . Chana 

Amesema  kwa upande wa wanyamapori waharibifu, teknolojia hiyo husaidia kutambua makundi na mienendo yao na kutoa taarifa mapema  kuhusu uwepo wa makundi hayo nje ya hifadhi na kichukua hatua kabla ya hayajasababisha madhara. 

"Taarifa hizi husaidia katika kupanga mbinu muafaka za kukabiliana na wanyamapori hao. " amesisitiza Balozi Dkt. Chana 

Katika hatua nyingine ameeleza kuwa zoezi hilo alilolizindulia limelenga kuimarisha uhifadhi na utalii kusini mwa Tanzania hususan katika Hifadhi za Taifa za Nyerere, Ruaha na Mikumi akifafanua kuwa litasaidia kwa kiwango kikubwa katika kupunguza migogoro baina ya jamii zinazozunguka hifadhi.  "Jumla ya makundi ya wanyamapori 53 yatafungwa mikanda hii yenye redio za mawasiliano katika hifadhi hizi tatu." amesisitiza Balozi Dkt. Chana

Sambamba na hayo, Waziri Balozi Dkt. Pindi Chana ameongeza kuwa wanyamapori  watakaofungwa mikanda hiyo ni  pamoja na makundi ya tembo, simba, chui, duma, mbwa mwitu na twiga. 

Aidha, taarifa na takwimu hizo zitasaidia kuandaa ramani za mitawanyiko ya wanyamapori  katika misimu na nyakati mbalimbali ambazo zitasaidia kufungua njia mpya za utalii “tourism circuits” pamoja na kuimarisha uhifadhi wa wanyamapori katika hifadhi hizo.

Naye Katibu Mkuu wa Maliasili na Utalii, Prof. Eliamani Sedoyeka amesema Tekinolojia hiyo itasaidia kuwalinda Wanyamapori na Hifadhi zetu hapa nchini. Pia, itasaidia kufuatilia mienendo ya Wanyamapori hai na kuweza kuwaona kidijitali pindi wanapotaka kuleta madhara.

"Kwa kutumia tekinolojia hii tunaweza kuwaona kidijitali wanapotembea na hasa wanapokaribia maeneo hatarishi ya kuleta madhara kwa wananchi"
 
    
Waziri wa Maliasili na Utalii,  Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana  alipokua akizindua  zoezi la Kuvisha Mikanda yenye Redio za Mawasiliano kwa wanyamapori 



 

 

BODI YA MAZAO MCHANGANYIKO NCHINI [CPB] IMEWATOA HOFU WAKULIMA WA MAZAO YA KUNDE


 

Na. Mwandishi wetu Simiyu

 

Bodi ya mazao mchanganyiko nchini (CPB) imesema kuwa wakulima nchini wenye mazao aina ya kunde, hawana sababu ya kuhangaika na soko la mazao yao kwani Bodi hiyo inao uhitaji mkubwa wa mazao hayo.

Ofisa Masoko wa Bodi hiyo Frank Bubelwa Akizungumza katika maonyesho ya wiki ya Chakula nchini yanayoendelea Mkoani Simiyu, amesema kuwa wakulima hawana sababu ya kuangaika na kutafuta wapi watauza mazao yao. Amesema serikali kupitia wizara ya kilimo, mazao na nafaka tumeona tuingie, tufungue milango kwa wakulima kwa kuweza kununua mazao yao yote ambayo wanalima na kuleta kwetu sisi inamaana kwa lugha nyepesi tunawasaidia kutoka katika changamoto ambayo walikuwa wananung’unika kupata masoko.

 

Aidha ameongeza kuwa mbali na Bodi hiyo kununua mazao kutoka kwa wakulima, bado bei ambazo wamekuwa wakinunulia mazao hayo ni rafiki kwa wakulima Lakini pia katika swala zima la bei za nafaka sisi kama taasisi sio taasisi kandamizi mkulima anapewa fursa na tunampa fedha inayoendana na bei ya sokoni mara nyingi wakulima wanakuwa na changamoto hiyo kubwa, unakuta mkulima anakuja kudalaliwa na mtu wakati kwa bei ya chini ambayo inamfanya yeye hasipate hamu au mtaji wake unaguswa kwaiyo anashindwa kufanya shughuli za kilimo. Sambamba na hilo afisa masoko Frank Bubelwaa amesema  kuwa katika msimu wa kilimo bodi ya nafaka huwa tunaangalia pande zote mbili mkulima hasiumie pia sisi tusipate hasara kwaiyo mara nyingi tunanunua mali kutokana na bei iliyo sokoni kama kwamfano kilo moja ya mahalage ni silingi elfu mbili sokoni sisi tutakuja kununua kwa bei hiyohiyo hatuwezi tukashuka Zaidi ya hapo. Hivyo basi sisi tupo kwaajiri ya kuhakikisha kuwa kilimo kinaendelea kukua lakini pia kwaupande mwingine kuongeza uchumi wa nchi.

 

maonyesho ya wiki ya Chakula nchini yanayoendelea Mkoani Simiyu
 

 

 

 

 

 

 

MIAKA 7 YA BMH: MKURUGENZI AELIMISHA KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE



 Na. Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano Hospitali ya Benjamin Mkapa





Hospitali ya Benjamin Mkapa Dodoma leo Oktoba 13, imetimiza miaka saba tangu ilipoanza kutoa huduma za Afya Oktoba 13, 2015.

 

Mkurugenzi Mtendaji Dkt, Alphonce Chandika amewajengea uwelewa juu ya Msuada wa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote wananchi waliyofika kupata huduma, ambapo mesema  lengo la Mswada huo ni kuhakikisha, kila mwananchi anakuwa na uhakika wa kupata matibabu bila hofu.

 

“Ndugu zangu baadhi yenu mnakuja hapa mara kwa mara kupata huduma, mnafahamu ugonjwa haubishi hodi, bila kuwa na BIMA kuna wenzetu hulazimika kuuza hata viwanja au nyumba wagharamie matibabu” Alidokeza, Dkt. Chandika.

 

Aidha, alifafanua kuwa mantiki ya Mswaada wa BIMA ya Afya kwa wote ni kuhakikisha kuwa, watu wengi wanachangia gharama za matibabu kabla hawajafikwa na maradhi ili kutunisha mfuko hatimae mtu akiugua asikutane na changamoto yoyote ya kukosa huduma kwa kushindwa kulipia gharama za matibabu.

 

“Msingi wa BIMA ya Afya kwa wote, ni suala la upendo zaidi, na baba wa Taifa Mwalimu Nyerere tunaeadhimisha  siku yake kesho alitufundisha kupendana, hivyo tunapochangia wengi, wakaugua baadhi tunakuwa tumewasaidia” Alifafanua Dkt. Chandika.

 

Vile vile, alieleza kuwa mapendekezo ya Mswada huo ni kwa kaya moja kuchangia Shilingi 340,000 na kunufaisha wanafamilia sita, huku mtu mmoja akitakiwa kuchangia kiasi cha shilingi 84,000 ili kupata huduma za Afya kwa mwaka mzima.

 

“Nasisitiza kuwa serikali haina lengo la kumlazimisha mtu kuchangi, bali itaweka mazingira rafiki yatakayomsukuma kila mmoja kuona umuhimu wa kuchangia, na kwa kutumia mifumo ya TASAF na Ustawi wa jamii itawatambua wasiyojiweza na kuwatengenezea mfumo wa kupata matibabu bila usumbufu” Alisema Dkt. Chandika.

 

 

Shamrashamra za kutimiza miaka hiyo saba zimeanza saa mbili asubuhi ya leo kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo Dkt. Alphonce Chandika kushiriki kutoa huduma za msingi kwa wagonjwa, aliwapokea, kuzungumza nao na kuwasaidia waliyohitaji kutembea kwa msaada wa kiti maalumu (Wheelchair).

 

Kisha aliwashukuru wananchi waliyofika Hospitalini hapo kwa kutoa mchango wao wa maoni, ambayo hupokewa na kufanyiwa kazi kwa wakati na ndiyo umekuwa msingi wa maboresho mbalimbali ya huduma katika Hospitali hiyo kiasi cha kuifanya kutambuliwa kama kinara kwa Utoaji wa huduma bora za Afya kwa Hospitali zote nchini.

 

Kwa asubuhi ya leo, sherehe hizo ziliahanikizwa na ukataji wa keki  maalumu ya miaka saba ya huduma katika Hospitali hiyo, ambayo ilikatwa kwa ushirikiano wa Mteja na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali hiyo.

 

Baadaye alielekea katika wodi ya watoto wachanga na kutoa zawadi mabalimbali kwa watoto hao kama sehemu ya kurejesha kwa jamii.






Mkurugenzi Mtendaji Dkt, Alphonce Chandika akizungumza na wanainchi waliyofika kupata huduma   juu ya Msuada wa Sheria ya Bima ya Afya kwa wote.

WAZIRI WA SHERIA DKT DAMAS NDUMBARO AMETOA UFAFANUZI KUHUSU WANAFUNZI WA SHERIA KUFELI MAFUNZO KWA VITENDO

Na. Kadala Komba Dodoma 
 
 
 
Kumekuwa na sintofahamu  kuhusiana na matokeo ya Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania (LST), mjadala ulioibuka katika sehemu  mbalimbali kwamba kwa nini wanafunzi hao wanafeli sana. Mjadala huu sio mpya, ni wa muda mrefu.

Historia ya wanafunzi  wachache kufaulu mitihani ya Taasisi hii haijaanza leo, ni ya siku nyingi, lakini hailengi kumkomesha mtu yoyote bali inalenga kuweka viwango vya juu.

Waziri wa katiba na Sheria Dkt Damas Ndumbaro amezungumza haya katika kikao na waandishi wa habari jijini Dodoma alisema Vinawekwa viwango vya juu kwa sababu Sheria ni jambo muhimu katika utawala bora, utawala wa Sheria, kuleta amani na utulivu pamoja na utoaji wa haki, hivyo ni lazima tuwe na imani na wanasheria tunaowapa jukumu hilo,
Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania ina Walimu 95 ambapo Walimu 14 kati yao waliobobea katika maeneo mbalimbali ya Sheria wameajiriwa  ajira ya kudumu. 

Kwa uhalisia wa kazi hii hufanyika kwa vitendo, Walimu wengi  wanaochukuliwa ni wataalam waliobobea kwenye maeneo yao ambapo kati ya Walimu 81, Walimu 10 ni Majaji. Kati ya Majaji kumi, watatu ni Majaji ambao bado wako kazini na Majaji saba ni wastaafu ambao wana uzoefu wa kutosha.

Katika orodha ya Walimu 81, Walimu wanne ni Mawakili wa Serikali ambao wengi wamekaa muda mrefu katika nafasi zao na wana uzoefu wa kutosha na Walimu 56 ni Mawakili wa kujitegemea waliobobea katika kazi zao.

 Tangu Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo Tanzania imeanzishwa, wanafunzi 8,255 kati ya wanafunzi 13,974 wamefaulu sawa na asilimia 59.074 na wanafunzi waliofeli baadhi ya masomo ambao wanaruhusiwa kurudia masomo hayo ni asilimia 21.619.

Takwimu zinaonesha kuwa, asilimia kubwa ya wanaorudia baadhi ya masomo waliyofeli huwa wanafaulu, hivyo ufaulu kwa ujumla utakuwa kwenye asilimia 81.

Kwa takwimu hizi za ufaulu, asilimia ya waliofeli kabisa ni asilimia 19 kati ya asilimia 100 ambayo ni asilimia ndogo na inatokea kokote duniani.

Kama kuna mwanafunzi anayehisi ameonewa, kuna mfumo wa kukata rufaa ambao upo na unafanya kazi.

Serikali imeunda Kamati ya watu saba ambayo imepewa siku 30 kuleta taarifa juu ya tuhuma hizi.  Kamati hii haijahusisha Waalimu wala Mstaafu yeyote wa Taasisi ya Mafunzo ya Uanasheria kwa Vitendo (LST) wala Walimu kutoka Vyuo vinavyotoa elimu ya sheria, tumehusisha wadau wengine ili walete majibu ya ukweli na yenye tija.
 

 

WAKATI WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA, DKT. DAMAS NDUMBARO AKITOA UFAFANUZI MBELE YA WAANDISHI WA HABARI JIJINI DODOMA KUHUSU WANAFUNZI WA SHERIA KUFELI MAFUNZO KWA VITENDO*