Home »
» TIMU YA MBEYA CITY YAKABIDHI ZAWADI KWA WAGONJWA KATIKA KITENGO CHA WAZAZI META.
TIMU YA MBEYA CITY YAKABIDHI ZAWADI KWA WAGONJWA KATIKA KITENGO CHA WAZAZI META.
Na.Mwandishi wetu Mbeya
Katika kusherehekea sikukuu za mwisho wa mwaka, ikiwemo Krismas na Mwaka mpya timu ya Mpira wa Miguu ya Mbeya City ikiongozwa na viongozi wake wametembelea Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya Kitengo cha Wazazi META kwaajili ya kutoa zawadi na kuwafariji wagonjwa ikiwa ni sehemu ya kurudusha kwa jamii.
Akiongea kwa niaba ya Uongozi wa Timu ya Mbeya City, Paul Nonga mcheza wa timu hiyo amesema hii ni sehemu ya utaratibu wao kama timu lengo likiwa ni kurudisha kwa jamii, hivyo wametembelea Hospitalini hapo kwa lengo la kuwafariji wagonjwa pamoja na kutoa zawadi zikiwemo Sabuni, Mashuka 50, Dawa za Meno, mafuta, pamoja na Mifuko maalumu kwaajili ya kubebea vitu.
“Timu ya Mbeya City pamoja na Mdhamini wetu (Peri March) tumeweza kukabidhi Mashuka 50, na hii ni moja ya vitu huwa tunavifanya kwaajili ya Kurudisha kwa jamii.” – Paul Nonga.
Akipokea zawadi hizo kwa niaba ya Mkuu wa Kitengo cha Wazazi Meta, Muuguzi wa Zamu Bi. Fatuma Saimoni ameushuru uongozi wa Timu hiyo na kuwasihi wandelee kuwa na moyo huo wa upendo wa jamii.
“Kwa hiyo tunashukuru kwa watu wa Mbeya City kwa kweli mna upendo, sisi kama wana META tunawashukuru sana Mungu aendelee kuwabariki kwa upendo huu.” - Fatuma Saimoni
MATUKIO YA PICHA TIMU YA MPIRA WA MIGUU MBEYA CITY WAKIWA NA VIONGOZI WAKITEMBELEA HOSPITAL YA RUFAA KANDA YA KATI KITENGO CHA WAZAZI
Related Posts:
MADAI YA KICHANGA KUGEUKA JIWE MARA, JE NINI MAONI YAKO:? Wakazi katika Manispaa ya Musoma mkoani Mara leo Aprili 20 wameingiwa na taharuki baada ya mwili wa mtoto, AMIRI HAMIS mwenye umri wa mwezi mmoja na siku 12 kudaiwa kugeuka jiwe huku baadhi ya watu wakihusisha tukio hil… Read More
VIONGOZI WANACHAMA SOMENI KATIBA TUJIBIZANE KWA HOJA Na. Kadala Komba Dodoma MBUNGE wa Jimbo la Bahi (CCM) Kenneth Nollo amewataka wanachama na Viongozi wa chama cha mapinduzi ccm Wilayani humo kusoma na kuielewa vyema katiba,kanuni na tarabitu za chama Ili kufanya majukumu … Read More
WAKULIMA WA DODOMA WAMETAKIWA KULIMA MTAMA KWA WINGINa Kadala Komba Dodoma KATIBU Mtendaji wa Shirika la Dodoma Agriculture Seeds Production Association (DASPA) Aithan Chaula Álisema kuwa wanekuwa wakihamasisha wakulima kulima mtama kwani ni zao ambalo Lina sokola úhakika … Read More
MASHINDANO YA RIADHA MEI MOSI MOROGORO, UTALII WAZIDI KUTANGAZIKA* Wizara ya Maliasili na Utalii imeibuka mshindi namba moja kwenye mbio za mita 800 kwenye mashindano ya Mei Mosi yanayoendelea mkoani Morogoro.Akizungumza leo mkoani humo mara baada ya ushindi&nbs… Read More
WAKUU WA MIKOA DHIBITINI MAAMBUKIZI YA MALARIA-MAJALIWA*Aitaja mikoa ya Tabora, Mtwara, Kagera, Shinyanga na Mara kuongoza kwa kiwango cha maambukizi WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa wito kwa mikoa ambayo ina kiwango kikubwa cha Maambukizi ya Malaria ianze kusimamia utekel… Read More
0 Comments:
Post a Comment