Subscribe Us

MAAFISA ELIMU KATA, WALIMU WAKUU, WALIMU WA MAZINGIRA MAAFISA MAENDELEO YA JAMII WA KATA WAJENGEWA UWEZO JINSI YA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI KATIKA MAZINGIRA YA SHULE BAHI

Na. Kadala Komba Bahi 
 
 
 Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Ndugu Boniphace Wilson akifunga mafunzo hayo  kwa niaba ya Mkurugenzi mtendaji  wa Halmshauri ya Wilaya ya Bahi Bi. Zaina Mlawa  ametoa maagizo kwa walimu wa mazingira na  wakuu wa shule za msingi kutunza mazingira ya shule na kupanda miti ya kutosha ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi katika maeneo ya shule zao. Akitoa maagizo hayo ameeleza umuhimu  wa uwepo wa miti shuleni na ujenzi wa madarasa  unaozingatia vigezo vya kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Ndugu Boniphace Wilson
            akifunga semina ya mazingira  ya siku tatu
 
 
 
Hayo yamejiri wakati wa semina ya mazingira  ya siku tatu iliyohusu mafunzo kwa walimu jinsi ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi katika shule zao. Semina hiyo imefanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Bahi.

"Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi Boniphace Wilson akifunga mafunzo hayo ametumia nafasi hiyo  kuishukuru serikali kupitia OR TAMISEMI kwa kuleta mafunzo hayo Bahi pia amewashukuru  wafadhili wa program hiyo ambao ni  Shule Bora kwa kutoa zaidi ya Milioni mia tatu,  kwajili kukamilisha maboma kumi na nane yaliyojengwa kwa kuzingatia vigezo vya kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi pamoja na kuwezesha  mafunzo mbali mbali kwa walimu yakiwepo haya ya mazingira
 
 
picha ya pamoja meza kuu 

 








Kwa upande wa walimu wakiongea kwa niaba, walimu wenzao wa wilaya ya Bahi  mwalimu Kondo,  Mwashi Benedict Cheo na Mkuu wa shule  Bahi English medium bi Farida Aloyce  Wameishukuru serikali kupitia Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa kuwaletea mradi wa mazingira chini ya program ya shule bora  ambao utaenda kubadilisha mazingira ya shule zetu na kukabiliana na mabadiliko ya tabia ya nchi

.Naye Afisa maendeleo ya jamii kata ya Babayu wilaya ya Bahi Nasibu Saidi Amewashukuru wafadhili wa mradi wa mazingira Shule bora kwa kuwakumbuka kata ya Babayu.




Related Posts:

0 Comments:

Post a Comment