Subscribe Us

MBUNGE WA JIMBO LA BAHI MHE. KENNETH NOLLO AMSHUKURU MHE.RAIS SAMIA KWA FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO BAHI

 
Na. Kadala Komba Bahi

Mbunge wa Jimbo la Bahi Mhe. Kenneth Nollo amemshukuru Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutoa fedha za miradi ya Maendeleo  kwa wananchi wa wilaya ya Bahi.

Hayo yamejiri wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa  wa Dodoma Mhe. Rosemary  Senyamule  akikagua  miradi ya maendeleo  katika Halmashauri ya Wilaya ya Bahi katika hospitali ya wilaya Bahi,  tar 19/03/2025  alisema Hospitali hii nikama ndoto kwa wana Bahi ni ukombozi mkubwa sana sisi watu wa Bahi yunasababu zote kumshukuru Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan rais wetu kwa kutoa fedha za kutekeleza miradi mbalimbali ya Maendeleo inayoendelea katika Halmashauri ya Bahi.

Katika sekta ya afya katika mwaka 2021hadi sasa mwaka 2025 vijiji kumi na saba vimepata  vituo vya Afya (Zahanati) ambapo awali vijiji kumi na tisa vilikuwa havina kituo cha afya  (Zahanati)


Related Posts:

0 Comments:

Post a Comment