Ikiwa ni miaka minne ya Daktari Samia Suluhu Hassan kwenye kiti cha Urais na yamefanyika Maendeleo makubwa chanya
Kupitia shamlashamla hizo za miaka minne ya Daktari Samia Suluhu Hassan Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe Rosemary Senyamule amefanya ziara Wilaya ya Bahi na kukagua Miundombinu ya hospitali ya Wilaya pamoja na miradi inayotekelezwa Katika Hospitali hiyo ikiwemo ukamilishaji wa mochuali ambao tayari lipo jokofu moja kwaajili ya kuhifadhia miili,pia amekagua jengo la kulazwa wanaume na jengo la kulazwa wanawake,
Kupitia ziara hiyo mkuu wa Mkoa ametembelea pia Zahanati ndogo iliyopo Nagulo kata ya Bahi ambayo ilizindiliwa siku za karibuni na kupitia ukaguzi wake ameridhishwa na huduma kwani Zahanati hiyo kwani imekua msaada mkubwa wa kuwahudumia Wananchi wa Nagulo Bahi waliokua wakitembea umbali mrefu kufuata huduma za afya.
Mkuu wa Mkoa Mhe Rosemary Senyamule ameipongeza sana Wilaya ya Bahi na uongozi wake kwa jitihada kubwa wanayoifanya ikiwemo usimamizi mzuri wa fedha za ujenzi wa miradi zinazotolewa na Mhe Rais Samia Suluhu Hassan, na kupitia ziara hiyo amesisitiza kuwa dhana ya uwajibikaji bora iwe nguzo kuu kwa watumishi wote ili kuweza kuchochea maendeleo chanya ndani ya Wilaya na Taifa kwa ujumla.
Home »
» RC SENYAMULE AIPA KONGOLE BAHI USIMAMIZI WA FEDHA ZA UJENZI WA MIRADI
RC SENYAMULE AIPA KONGOLE BAHI USIMAMIZI WA FEDHA ZA UJENZI WA MIRADI
Related Posts:
WAKUU WA MIKOA DHIBITINI MAAMBUKIZI YA MALARIA-MAJALIWA*Aitaja mikoa ya Tabora, Mtwara, Kagera, Shinyanga na Mara kuongoza kwa kiwango cha maambukizi WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa wito kwa mikoa ambayo ina kiwango kikubwa cha Maambukizi ya Malaria ianze kusimamia utekel… Read More
WAJAWAZITO KUPIMWA VIPIMO VYA AWALI BILA MALIPONa. Catherine Sungura-Dodoma. Waziri wa Afya Mhe.Ummy Mwalimu amewataka akina mama wajawazito wanaofika kwenye Kliniki za Uzazi, Mama na Mto kupimwa wingi wa damu, mkojo kuangalia wingi wa protini, shinikizo la damu pamo… Read More
MASHINDANO YA RIADHA MEI MOSI MOROGORO, UTALII WAZIDI KUTANGAZIKA* Wizara ya Maliasili na Utalii imeibuka mshindi namba moja kwenye mbio za mita 800 kwenye mashindano ya Mei Mosi yanayoendelea mkoani Morogoro.Akizungumza leo mkoani humo mara baada ya ushindi&nbs… Read More
ZAIDI YA VIJANA 147 WAMEHITIMU MAFUNZO YA UANAGEZI Na. Kadala KombaDODOMAMkurugenzi wa Idara ya Ukuzaji Ajira na Ujuzi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Ally Msaki ameshauri Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo Dodoma (SIDO) kushiri… Read More
MADAI YA KICHANGA KUGEUKA JIWE MARA, JE NINI MAONI YAKO:? Wakazi katika Manispaa ya Musoma mkoani Mara leo Aprili 20 wameingiwa na taharuki baada ya mwili wa mtoto, AMIRI HAMIS mwenye umri wa mwezi mmoja na siku 12 kudaiwa kugeuka jiwe huku baadhi ya watu wakihusisha tukio hil… Read More
0 Comments:
Post a Comment