Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe.Rosemary Senyamule amesema azima ya Serikali ni kuhakikisha inatatua changamoto za wananchi na kuleta maendeleo kwa watu wake.
Mhe.Senyamule ameyasema hayo alipotembelea Kijiji cha Mpwayungu kilichopo katika Wilaya ya Chamwino ikiwa ni katika utaratibu aliojiwekea wa kusikiliza kero za wananchi wa Dodoma ambapo amebaini changamoto mbalimbali za Wananchi hao ikiwemo upatikanaji wa maji, umeme, na Barabara. Mhe. Senyamule amezipokea kero hizo na kuzipatia ufumbuzi ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa agizo la Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
"Kuja hapa leo ni kuhakikisha matamanio ya Rais wetu yanatimia kwa kusikiliza changamoto mlizonazo na kuzipatia ufumbuzi na zinazo muhusu yeye kuziwasilisha kwake kwa ajili ya utekelezaji " amesema Mhe. Senyamule
Katika Hatua nyingine, akiwa katika mradi wa mashamba ya pamoja ya 'Bulding a Better Tomorrow '(BBT), ametoa shime kwa wasimamizi wa mradi huo kuchukua hatua kwa Changamoto zinazojitokeza zinazopelekea mradi huo kutokwenda kwa kasi iliyokusudiwa.
"Hakikisheni tarehe ambayo imepangwa kwa kazi hii kuwa tayari inatimia ,hivyo basi fanyeni utaratibu wa kuweka mashine za kufyatulia matofali sehemu ya mradi ifikapo Jumatano, mashine ziwe sehemu ya kazi ,pia ongezeni nguvu kazi ili kusadia mradi ukamilike kwa wakati "Amesisitiza Mhe. Senyamule
Kwa Upande Wake, Mkuu wa Wilaya ya chamwino Mhe. Gift Msuya, amemshukuru Mhe. Rais kwa kuendelea kufanya mambo ya maendeleo katika Tarafa ya Mpwayungu pamoja na mradi wa Kilimo cha pamoja, Ujenzi wa Shule Mpya ya Sekondari Nkhambako na mengine.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma amefanya ziara ya kikazi katika Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino ambapo ziara hiyo ametembelea mradi wa Mashamba ya Kilimo cha pamoja, Ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari katika Kata ya Nkhambako na kusikiliza changamoto za wananchi wa tarafa ya Mpwayungu na kuzipatia ufumbuzi.
Home »
» RC SENYAMULE TUMEJIPANGA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WANANCHI DODOMA
RC SENYAMULE TUMEJIPANGA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WANANCHI DODOMA
Related Posts:
JUMUIYA YA MARIDHIANO YAMTUNUKU RAIS SAMIA TUZO YA HESHIMANa. Kadala Komba DodomaJUMUIYA ya Maaridhiano mkoa wa Dodoma imemkadhi Tuzo Rais Samia Suluhu Hassani,kutokana na kuutambua mchango wake mkubwa wa kuiongoza nchi pamoja na Watanzania kwa amani. Tuzo hiyo imepokelewa na Mkuu … Read More
BILIONI 1.7 ZIMETUMIKA KUJENGA BWENI LA WANAFUNZI WA KIKE Na. Moreen Rojas, Dodoma.Taasisi ya Afrika ya sayansi na teknolojia ya Nelson Mandela inadhamiria kupendekeza ujenzi wa bweni la wanafunzi wa kike wenye watoto wadogo na mahitaji maalum ambapo kiasi cha shilingi bili… Read More
BAHI YAFUNGUA MILANGO KWA WANAFUNZI WANAOISHI MAZINGIRA MAGUMU. Na Kadala Komba- Dodoma Diwani wa Kata ya Mpamatwa, Sosthenes Mpandu amewataka wanafunzi kusoma kwa juhudi na kujiamini ili kufanya vizuri katika mitihani yao hatimaye waweze kujiunga na masomo ya elimu ya juu.… Read More
NAIBU WAZIRI WIZARA YA MAJI ATEMBELEA MKOA WA KIGOMA Na Mwandishi wetu Kigoma Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) ametembelea Mradi wa Kuboresha Huduma ya Maji na Usafi wa Mazingira Kigoma. Mradi huu unatumia ziwa Tanganyika kama chanzo cha maji, katik… Read More
ULAJI WA VYAKULA VYENYE SUMUKUVU UNAVYOATHIRI AFYANa mwandishi wetu , SimiyuMADHARA ya sumukuvu huweza kujitokeza ndani ya muda mfupi, baada ya muda mrefu kutegemea na kiasi cha sumukuvu hiyo iliyopo kwenye chakula kilicholiwa,idadi ya milo ya chakula kilichochafuliwa… Read More
0 Comments:
Post a Comment