Akizungumza
katika kambi ya upasuaji wa mtoto wa jicho inayoendelea kwenye
hospitali ya Wilaya Mbarali Bw. Antony Ndwenywa(83) kutoka kitongoji cha
Mkanyageni-Rujewa ambaye alifanyiwa upasuaji wa mtoto wa jicho macho
yake mawili mwezi Disemba 2022, amesema tangu amefanyiwa upasuaji
anaendelea vizuri na hivi sasa anasoma hata magazeti
"Mimi
nilifanyiwa macho yote mawili yalikuwa na mtoto wa jicho na hadi sasa
naendelea vizuri.Tunaishukuru Serikali kwa kutupatia huduma sisi watu wa
chini ,huduma hizi ni bila malipo ninashukuru sana.
Naye, Bi.
Vailet Mbelewele mkazi wa Mabadaga ambaye alikua na mtoto wa jicho kwa
muda wa mwaka mmoja amewashukuru watoa huduma wakiwemo madaktari na
wauguzi kwa huduma nzuri walizompatia na kuongeza kuwa ametolewa bandeji
na sasa anaona.
Amesema mara baada ya kupata tatizo hilo alikua
akinunua dawa kwenye maduka bila ushauri wa madaktari "nawashauri
wananchi wasijinunulie dawa mje moja kwa moja kwani madaktari wapo na
huduma ni nzuri".
Vilevile Mzee Ahmed Abdallah Mkazi wa Igurusi
ambaye alishakwisha fanyiwa upasuaji wa jicho moja miaka miwili
iliyopita na kwa kambi hii amefanyiwa upasuaji jicho la pili
amemshukuru Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan pamoja na viongozi wake wa
chini kwa jitihada zake kwa kuwasaidia watu wa chini.
"Tunamshukuru
Mama kwa kutusaidia mambo mengi kama barabara,ametuletea mbolea,natoa
sifa kwa Dkt. Samia anatuhudumia sisi watu wa hali hii kwani habagui na
hachagui.
Kambi ya upasuaji wa mtoto wa jicho wilayani Mbarali
imeanza tarehe 11 Aprili,2023 na inatarajiwa kumalizika tarehe 20
Aprili,2023.Inaratibiwa na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Shirika la
Hellen Keler International la hapa nchini.
Home »
» WAKAZI WA MBARALI WAIPONGEZA SERIKALI KWA MATIBABU YA MACHO*
WAKAZI WA MBARALI WAIPONGEZA SERIKALI KWA MATIBABU YA MACHO*
Wakazi wa Mbarali wameipongeza Serikali kupitia Wizara ya Afya na wadau
wa huduma za macho kwa kuwapatia matibabu ya macho bila malipo.
Related Posts:
WATU 12 WAMEPOTEZA MAISHA KWA AJALI DODOMADodoma WATU 12 wamepoteza maisha baada ya basi a Frester lililokuwa likitokea Bukoba kwenda Dar es salaam kugongana uso kwa uso na Lori la Texas majira usiku wa kuamkia leo. Ajali hiyo imetokea eneo Kiiji Cha Silwa wilaya… Read More
NSSF IMEJIPANGA KUANZA KUTOA MAFAO KWA SEKTA ISIYO RASMI Na. Kadala Komba Dodoma. Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii(NSSF)umewataka wafanyakazi wa sekta isiyo rasmi kujiunga na mfuko huo kwa kupeleka michango yao na hatimaye kuwa kwenye mfumo wa mafao hali itakayosaidia kupun… Read More
DK.SWEKE: BAHARI KUU IPO SALAMA TUNATUMIA NDEGE KUFANYA DORIA Na. Kadala Komba Dodoma. MKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi na Bahari Kuu Dkt.Emmanuel Andrew Sweke,ameeleza kuwa katika kulinda usalama wa bahari kuu wameweka mifumo ya kulinda usalama ikiwa ni pamoja na kutum… Read More
UTEUZI: EPHRAIM BALOZI MAFURU ATEULIWA KUWA MTENDAJI MKUU AICC … Read More
PROF.MKENDA :BADO UCHUNGUZI UNAENDELEA KWA WANAFUNZI NA WASIMAMIZI WA MITIHANI KIDATO NNE MWAKA 2022 .Na. Mwandishi wetu Dodoma SERIKALI kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, imesema imedhamiria kukomesha vitendo vya wizi wa mitihani huku ikiridhishwa na uamuzi wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) kwa wanafunz… Read More
0 Comments:
Post a Comment