Subscribe Us

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

TIMU YA MBEYA CITY YAKABIDHI ZAWADI KWA WAGONJWA KATIKA KITENGO CHA WAZAZI META.

Na.Mwandishi wetu Mbeya Katika kusherehekea sikukuu za mwisho wa mwaka, ikiwemo Krismas na Mwaka mpya timu ya Mpira wa Miguu ya Mbeya City ikiongozwa na viongozi wake wametembelea Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya Kitengo cha Wazazi META kwaajili ya kutoa zawadi na kuwafariji wagonjwa ikiwa ni sehemu ya kurudusha kwa jamii. Akiongea kwa niaba ya Uongozi wa Timu ya Mbeya...

UONGOZI DOREFA WAAGIZWA KUFUTILIA MAENEO YALIYOTENGWA KWAJILI YA MICHEZO 

Na Kadala Komba Dodoma Wanamichezo nchini waaswa kupambania tasnia ya michezo ikiwa ni agenda ya kuhakikisha tasnia hiyo inapewa thamani na kipaumbele kama sekta zingine. Hayo yamesemwa na Kaimu Mkurugenzi wa michezo Nchini Ndg.Ally Mayai Tembele wakati akizungumza na wadau wa soka kwenye mkutano mkuu wa mwaka wa chama cha mpira wa miguu jijini Dodoma(DOREFA) uliofanyika...

MKUU WA MKOA DODOMA MHE. ROSEMARY SENYAMULE AMEPOKEA HATI YA PONGEZI KUTOKA CHAMA CHA WAANDISHI WA HABARI GEITA

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rosemary Senyamule amepokea hati ya pongezi kutoka kwa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa wa Geita kwa kutambua mchango wake na kuleta mageuzi katika kipindi ambacho amekua Mkuu wa Mkoa huo. Hati hiyo imewasilishwa leo tarehe 19/12/2022 na Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari wa Mkoa wa Geita Bw. Renatus Masuguliko akiambatana na Katibu...

RWANDA KUBADILI MUDA WA MASOMO SHULE ZOTE IFIKAPO MWAKA 2023

Rwanda wamebadili muda wa kuanza na kumaliza masomo na saa za kazi. Kuanzia Januari 01 2023, Shule zote zitaanza masomo saa 2:30 asubuhi na kumaliza saa 11 jioni.  Saa za kazi ni kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 11 jioni. Hii kuwaongezea muda wa kulala watoto kwani wanaamshwa alfajiri sana na wanasinzia shuleni. Na pia ni kuwawezesha wazazi waweze kuwaona watoto wao na...

WACHAKATAJI WA MAZAO YA UVUVI WAPIGWA MSASA

WACHAKATAJI WA MAZAO YA UVUVI WAPIGWA MSASA. Wachakataji wa mazao ya uvuvi nchini wametakiwa kutumia fursa ya teknolojia katika shughuli zao ili kuboresha mnyororo wa thamani wa mazao ya uvuvi na kukabiliana na upotevu wa mazao hayo katika Ziwa Tanganyika. Hayo yamesemwa na Afisa Mtaalam Mnyororo wa Thamani wa Uvuvi na Ufugaji Viumbe Maji Hashim Muumin wakati wa mafunzo...

JAMII YAHIMIZWA KUPAZA SAUTI VITENDO VYA UKATILI.

Na mwandishi wetu- Dodoma JAMII YAHIMIZWA KUPAZA SAUTI VITENDO VYA UKATILI. Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. John Jingu ameitaka jamii, wadau na kila mmoja kwa nafasi yake kupaza sauti dhidi ya vitendo vya ukatili ambavyo vimekuwa vikiendelea katika maeneo mbalimbali nchini. Dkt. Jingu ameyasema hayo Jijini Dodoma kwa niaba ya Katibu Mkuu Kiongozi...

“UTAFITI WA MBEGU UZINGATIE HALI YA HEWA” DK. JINGU

“UTAFITI WA MBEGU UZINGATIE HALI YA HEWA” DK. JINGU NA MWANDISHI WETU - DODOMA Watafiti wa masuala ya kilimo nchini wametakiwa kutumia matokeo ya utafiti wao wanaofanya katika kuboresha mbegu bora za mazao zinazoendana na mabadiliko ya tabia nchi ili kuwa na tija katika sekta . Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Dkt. John Jingu wakati...

ASKOFU DKT CHANDE AMETOA MSAADA KWA YATIMA NA WAJANE

DODOMA Askofu Dkt Evance Chande wa Kanisa la Karmeli Assemblis Of God la jijini Dodoma Leo ni siku muhimu Kwa watoto yatima,wajane na waishio katika mazingira magumu kupatiwa misaada mbalimbali kutoka. ujumbe Dini iliyo nzuri ni kuwajali yatima na waj...

MKURUGENZI WA MASHTAKA MWAKITALU AMETEMBELEA GEREZA KUU LA ISANGA DODOMA

Na. Mwandishi wetu Dodoma Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Sylvester Mwakitalu ametembelea Gereza Kuu la Isanga jijini Dodoma kwa lengo la kusikiliza changamoto zinazowakabili Maafisa wa Magereza katika kuwatunza wafungwa pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakabili mahabusu. Akizungumza baada ya kutembelea Gereza Kuu la Isanga Mkurugenzi wa Mashtaka amesema kuwa...