Na Moreen Rojas,
Dodoma.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya,DK.John Jingu amezindua mradi wa mzunguko wa saba wa Mfuko wa Dunia (Global Fund Circle7)ambao utatekelezwa kwa muda wa miaka mitatu kuanzia sasa kwaaijili ya kutokomeza Ukimwi,Kifua kikuu na Malaria nchini Tanzania ili kutokomeza Magonjwa hayo ifikapo Mwaka 2030.
DK.Jingu amezindua mradi huo,Machi 21 Jijini Dodoma, ambapo amewataka wanaotekeleza Mradi huo kufanya kazi kwa ufanisi ili kuongeza tija katika kutokomeza magonjwa hayo.
“Ni muhimu sana sisi ambao tunatekeleza Mradi huu kuhakikisha tunatumia fedha ambazo tumefadhiliwa na Mfuko huu wa Dunia kwa malengo yaliyokusudiwa katika kuwa na huduma bora kwa Wananchi,”Amesema Dk. Jingu
Amefafanua kuwa Serikali ya awamu ya sita ya Rais Dk. Samia imekuwa ikiwekeza fedha nyingi katika Sekta ya afya kwa Lengo la kuboresha afya za Wananchi wake na Kuwataka watumishi hai kufanya kazi zao kwa weledi mkubwa.
Kwa upande Wake,Mganga Mkuu wa Serikali,Profesa Dk.Tumaini Nagu amesema wapo kwaajili yakujipima na kuangalia walipotoka na walipo ili kufikia malengo ya Kidunia namba tatu kwa kutekeleza Strategic Plan ya afya namba tano.
“Serikali imeona umuhimu katika kutokomeza magonjwa haya ambayo ni Ukimwi,Kifua Kikuu na Malaria ili kuhakikisha inatokomeza magonjwa hayo ifikapo Mwaka 2030,”Amesema Profesa Nagu
Awali Mwakilishi wa Serikali ya Marekani ambao Pia wanatekeleza Mradi wa PEPFAR,GETRUDE TEMBA amesema wanatambua mchango wa Tanzania katika mapambano dhidi ya Magonjwa hayo huku akiwasisitiza kufanya kazi kwa umakini katika kuhakikisha rasilimali wanazopatiwa wanazitumia kwa usahihi.
MWISHO
Home »
» UKIMWI,KIFUA KIKUU NA MALARIA MBIONI KUTOKOMEZWA.
UKIMWI,KIFUA KIKUU NA MALARIA MBIONI KUTOKOMEZWA.
Related Posts:
MAKAMU WA RAIS: SERIKALI INATHAMINI MCHANGO WA MADHEHEBU YOTE YA DINIImeelezwa kuwa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan inathamini mchango wa Madhehebu ya dini kupitia mahubiri na kufundisha neno la Mungu kwa watu wote.Hayo yamebainish… Read More
JUKUMU LA KUWAANGALIA WAZEE SIO LA SERIKALI PEKEE.Na Moreen Rojas DodomaKatika nchi nyingi Duniani,Wazee wamekuwa wakituzwa isipokuwa kwamba kila nchi ina namna yake ya kuwatunza wazee wao kwa kulingana na mila,desturi na tamaduni pamoja na hali za kiuchumi za nchi zao.Ha… Read More
WATOTO YATIMA WAIOMBA BAKWATA KUWAWEKEA UZIO Na Peter Mkwavila KONDOAWATOTO wa Kituo cha yatima kinachomilikiwa na taasisi ya All Hafidhu Islamic Orphans Centre kilichopo Bicha wilaya ya Kondoa.Wameliomba Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) kuwajengea uzio … Read More
VIJANA WAKATAA KUCHANJA CHANJO YA UVIKO 19 KWA KUHOFIA KUPOTEZA NGUVU ZA KIUME.Na Moreen Rojas DodomaVijana wengi wameingiwa na hofu ya kukataa kuchanjwa chanjo ya uviko 19 kwa kuhisi watapunguza nguvu za kiume pamoja na kuhisi watajiingiza katika imani za kishirikina.Hayo yamesemwa na Bi.Flora Kima… Read More
BODI YA FILAMU TANZANIA IMEUNDA KAMATI MAALUM YA KURUDISHA UTAMADUNI WA KUTAZAMA FILAMU KATIKA KUMBI ZA SINEMANa Moreen Rojas Dodoma Hatua hiyo inatarajiwa pia kutoa mchango stahiki katika uchumi wa wadau wa Sekta na Taifa kupitia viingilio vya mlangoni. Kwa upande wa usambazaji Serikali ina makubaliano ya kimataifa Televi… Read More
0 Comments:
Post a Comment