Na Moreen Rojas,
Dodoma.
Waziri wa Jeshi la kujenga Taifa(JKT)Mhe.Innocent Bashungwa amewaalika wananchi wa mkoa wa Dodoma kuhudhuria maadhimisho ya miaka 60 ya jeshi hilo yatakayofanyika tarehe 10 julai siku ya jumatatu katika uwanja wa jamuhuri jijini Dodoma.
Waziri Bashungwa ameyasema hayo hii leo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa habari maelezo lengo likiwa ni kutoa muongozo na taratibu kufuatia siku hiyo ya miaka 60 ya JKT.
Aidha amesema kuwa mgeni rasmi katika hafla hiyo ya miaka 60 ya Jeshi la kujenga Taifa ni Mheshimiwa Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan.
Aidha maadhimisho ya miaka 60 ya JKT yalitanguliwa na shughuli mbalimbali ambapo June 25 kulikuwa na tukio la JKT marathon ikiwa ni tukio la kwanza tangu kuanzishwa kwake ambapo mgeni rasmi wa tukio hilo alikuwa Rais mstaafu Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete.
Aidha ameongeza kuwa JKT inajivunia kuwa moja ya taasisi inayotambua na kuvumbua vipaji ikiwemo michezo na sanaa.
"Jeshini vipaji vyote vipo tunavilea tunavijengea ustawi na tunaangalia namna ya kutambua vipaji hivi na kuviendeleza mfano mzuri ukisikiliza bendi ya JKT au waimbaji wetu wa taarabu utaona ni kwa namna gani tunakuza na kuendeleza vipaji" Amesisitiza Waziri Bashungwa.
Sanjari na hayo miaka 60 ya JKT itapambwa na maonyesho ya vifaa mbalimbali kutoka JKT na wasanii mbalimbali bila kusahau gwaride huku wakiwaalika marafiki kupitia chaneli za kidiplomasia ikiwemo Izrael.
Jeshi la kujenga Taifa (JKT)lilianzishwa mwaka 1963 chini ya muasisi wa Taifa Rais Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Home »
» WANANCHI WAALIKWA MIAKA 60 YA JKT
WANANCHI WAALIKWA MIAKA 60 YA JKT
Related Posts:
𝗧𝗔𝗔𝗦𝗜𝗦𝗜 𝗭𝗔 𝗨𝗠𝗠𝗔 𝗭𝗔𝗛𝗜𝗠𝗜𝗭𝗪𝗔 𝗞𝗨𝗘𝗡𝗗𝗘𝗦𝗛𝗔 𝗩𝗜𝗞𝗔𝗢 𝗞𝗪𝗔 𝗡𝗝𝗜𝗔 𝗬𝗔 𝗠𝗧𝗔𝗡𝗗𝗔𝗢 𝗞𝗨𝗣𝗨𝗡𝗚𝗨𝗭𝗔 𝗚𝗛𝗔𝗥𝗔𝗠𝗔 Meneja Mawasiliano Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), Bi. Subira Kaswaga, amezitaka Taasisi za Umma nchini kuendesha vikao kidijitali kwa kutumia mfumo wa e-Mikutano ili kupunguza gharama za uendeshaji wa vikao.Kaswaga… Read More
RC SENYAMULE VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA YA AFYA BONANZA KUPIMA AFYA ZAO. Na.Elimu ya Afya kwa Umma.Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule ametoa wito kwa vijana kuchangamkia fursa za Afya Bonanza ili waweze kupima afya zao na kupata elimu kuhusu masuala mbalimbali ya afya.Seny… Read More
WAZIRI UMMY AMETOA WITO KWA MADAKTARI BIGWA UPASUAJI KUFANYA KAZI MIKOA YOTE. Na Moreen Rojas,Dodoma.Waziri wa Afya Ummy Mwalimu ametoa wito kwa madaktari bigwa upasuaji kufanya kazi mikoa yote na kuhakikisha wanazalisha wataalamu wazuri kwani kuna uhaba wa madaktari bigwa wa upasuaji nchin… Read More
SERIKALI KUJENGA KIWANJA KIPYA CHA MICHEZO JIJINI ARUSHANa Eleuteri Mangi, WUSM, ARUSHAMkoa wa Arusha umepewa dhamana kubwa ya kitaifa ya kujengwa kiwanja kipya cha michezo na kufanya Tanzania kuwa na viwanja vitatu vinavyokidhi vigezo na mahitaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu A… Read More
TANZANIA YAADHIMISHA SIKU YA YOGA DUNIANI Na Eleuteri Mangi, WUSM, Dar es SalaamTanzania imeadhimisha Siku ya Yoga Duniani huku Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo ikisisitiza kuunga mkono sherehe za kitamaduni za mataifa mbalimbali duniani kwa sababu zinasai… Read More
0 Comments:
Post a Comment