Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Jumanne Sagini amesema kuwa Serikali haipo tayari kuona Mwananchi yeyote anapoteza uhai wake kwa sababu za ama ujambazi au udereva mbovu barabarani au migogoro baina ya wakulima na wafugaji.
Sagini ameyasema hayo wakati akihitimisha bonanza la michezo lililoandaliwa na Umoja wa Maafisa Usafirishaji (Bodaboda ) Wilaya ya Butiama kwa lengo la kupinga matukio ya mauaji na ukatili katika jamii.
"Nataka niwaambie Serikali ya awamu ya sita chini ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan haitaki kumpoteza kijana hata mmoja au Mwananchi yoyote yule kwa sababu ama za ujambazi au udereva mbovu barabarani au migogoro baina ya wakulima na wafugaji. Ni aibu kuwa na matukio ya uhalifu tutawakamata wahalifu wote. Niwaombe vijana tuache kutumia njia za mkato kujipatia fedha."Alisema Sagini
Sagini amesema kuwa Jeshi la Polisi lipo imara na linawataalamu wenye ujuzi wa kutosha kuwabaini watu mbalimbali wanaojihusisha na matukio ya kihalifu na hivyo amewaasa wale wote wanaotamani kushiriki kufanya uhalifu kuacha mara moja.
Sagini amesema kuwa Serikali inaunga mkono jitihada za bodaboda hao katika kukemea na kupinga matukio ya kikatili na mauaji ni jambo jema na Serikali haitamani kusikia kuendelea kwa matukio hayo.
Katika hatua nyingine Sagini amesema kuwa Jeshi la Polisi lipo imara na linawataalamu wenye ujuzi wa kutosha kuwabaini watu mbalimbali wanaojihusisha na matukio ya kihalifu na hivyo amewaasa wale wote wanaotamani kushiriki kufanya uhalifu kuacha mara moja.
Sagini amesema kuwa Serikali inaunga mkono jitihada za bodaboda hao katika kukemea na kupinga matukio ya kikatili na mauaji ni jambo jema na Serikali haitamani kusikia kuendelea kwa matukio hayo.
Awali akitoa taarifa za lengo la bonanza hilo Mwenyekiti wa Waendesha Bodaboda Samson Samwel Atoo amesema kuwa lengo la Bonanza hilo ni kuwaunganisha kwa pamoja, kupiga vita na kukemea matukio ya kihalifu yakiwemo mauaji yaliyotokea mwezi uliopita ambapo waendesha bodaboda 03 walipoteza maisha kwa kushambuliwa na kuuawa kinyama.
Tamasha hilo lilihusisha michezo mbalimbali ikiwemo mpira wa miguu, kuvuta kamba, kukimbiza kuku,
Home »
» SERIKALI HAIPO TAYARI KUMPOTEZA MTU
SERIKALI HAIPO TAYARI KUMPOTEZA MTU
Related Posts:
SERIKALI IMEOMBWA KUPUNGUZA BEI YA NISHATI YA GESI YA KUPIKIA.Na Moreen Rojas,DodomaMwenyekiti Taifa wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mary Chatanda ameiomba Serikali kupunguza bei ya Nishati ya gesi ili wanawake Waweze kuachana na Matumizi ya kuni na mkaa kwenye shughuli za mapishi.M… Read More
TUENDELEE KUUNGANA KUKABILIANA NA MAAFA NCHINI” MKURUGENZI MSAIDIZI JANE NA. MWANDISHI WETUMkurugenzi Msaidizi Kituo cha Operesheni na Mawasiliano ya Dharura Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Bi. Jane Kikunya amesema Serikali itaendelea kutoa ushirikia… Read More
TUNAIOMBA SERIKALI ITUSAIDIE KUFUNGIA MAKAMPUNI BUBU(UKUTA). Na Moreen Rojas,Dodoma.Umoja wa makampuni binafsi ya ulinzi Tanzania (UKUTA) wameiomba serikali kufungia makampuni bubu kwani wanafungua kampuni hizo bila kufuata sheria jambo ambalo ni sawasawa na kuhujumu uchumi… Read More
HATUKUBALIANI NA SHERIA YA WENZA WA VIONGOZI KULIPWA MAFAO "CHADEMA". Na Moreen Rojas,DodomaCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepinga kitendo cha Bunge kupitisha sheria ya wenza wa viongozi kulipwa mafao huku kikishauri kufanyiwa kwa marejeo ya sheria ya Kikokotoo ambacho kime… Read More
REA YATOA ELIMU YA MATUMIZI YA TEKNOLOJIA YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA. Na Moreen Rojas,Dodoma.Viongozi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wakiongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB); Mhe. Balozi na Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu, Mkurugenzi Mkuu, Mhandisi Hassan Saidy … Read More
0 Comments:
Post a Comment