Subscribe Us

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

MBEGU BORA YA MTAMA TARISOR1 LIMA KIDOGO PATA ZAIDI

 
WAKULIMA wa zao la mtama wameshauriwa kutumia mbegu  ya mtama  aina ya TARISOR1 kwa kuwa mtama huo hauliwi na ndege kama ilivyo kwa mtama mwingine.

Mbegu ya mtama TARISOR1 ukomaa kwa siku 120. Nafasi za kupanda sm 75-90 x sm 30 panda mbegu 2, kisha ikiota ing'olei ibaki moja.




*WANANCHI WAJIONEA UTEKELEZAJI MIRADI YA GESI ASILIA NANENANE DODOMA*


📌 *Teknolojia ya Uhalisia Pepe yawa kivutio*

📌 *Elimu Matumizi ya Nishati Safi Kupikia yatolewa*

Maonesho ya Kimataifa ya Nanenane yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma yamekuwa ni sehemu ya wananchi kujionea utekelezaji wa miradi mbalimbali katika Sekta ya Nishati ikiwemo miradi ya Gesi Asilia na Mafuta

Katika Banda la Wizara ya Nishati wananchi wameonesha kuvutiwa na teknolojia ya Uhalisia
Pepe (Virtual reality) ambayo inawawezesha wananchi kuona moja kwa moja miradi ya uzalishaji, uchakataji na usambazaji wa gesi asilia iliyopo mkoani Mtwara na Lindi.

Kupitia teknolojia hiyo wananchi wameweza kuona namna gesi inavyozalishwa kutoka kwenye visima na kuingiwa kwenye mitambo ya uchakataji kisha kusafirishwa kwa bomba kwenda kwenye matumizi mbalimbali ya viwandani, kuzalisha umeme, kwenye magari, taasisi pamoja na matumizi ya majumbani.

Aidha, Wizara ya Nishati inaendelea kutoa elimu ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia (2024-2034).


WAZIRI MAVUNDE, WAZIRI MCHENGERWA KUKUTANA KUSHUGHULIKIA TOZO ZA HALMASHAURI KWENYE MADINI

 




Ni Kufuatia Changamoto za tozo za Halmashauri zilizowasilishwa na wachimbaji Morogoro

Waziri Mavunde awapongeza Morogoro kuvuka lengo la makusanyo ya maduhuli

Serikali kuongeza nguvu ya Utafiti Morogoro

Wachimbaji wamshukuru Rais Samia kwa mashine za uchorongaji

Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde amesema Wizara ya Madini imekubaliana na Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kukutana na kutatua changamoto ya tozo zinazowekwa na Halmashauri kwa wachimbaji wa madini nchini.

Aliyasema hayo  Agosti 5, 2024 Mkoani Morogoro  wakati wa kikao na Wachimbaji wa Mkoa wa Morogoro kwa lengo la kusikiliza na kutatua kero za wachimbaji mkoani hapa.

“Nimesikiliza kwa umakini mkubwa kilio hiki cha tozo za Halmashauri na tozo nyinginezo kwa wachimbaji wadogo,kero hizi sio hapa tu zipo maeneo yote nchini," alisema Mavunde.

Aliongeza kwamba  maelekezo ya Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa kuzitaka Wizara hizo mbili kukutana ili kushughulikia suala hilo.

"Nataka niwahakikishe mimi na Mwenzangu Mhe. Mohamed Mchengerwa tumekubaliana kwamba mara baada ya ziara ya Mh. Rais Dkt. Samia Suluhu mkoani Morogoro tutaitisha kikao cha pamoja ili kushughulikia suala hili,".

Pia, Waziri Mavunde  alitumia fursa hiyo kuwahakikishia wachimbaji wa Morogoro kuhusu dhamira ya Rais Dkt. Hassan kuongeza nguvu kwenye eneo la utafiti wa madini  ikiwemo  Mkoa  Morogoro  kunufaika.

Mhe. Mavunde aliipongeza Ofisi ya Madini Mkoa wa Morogoro kwa kuvuka lengo la ukusanyaji maduhuli kufikia shilingi  bilioni 4.9 zaidi ya lengo lililowekwa la shilingi bilioni 4.2bn.

Akisoma risala kwa niaba ya wachimbaji, Mwenyekiti wa Chama cha Wachimba Madini Mkoa wa Morogoro(MOREMA) Dkt. Omar Mzeru,  alimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa mashine za uchorongaji kwa wachimbaji  wadogo na kutumia fursa hiyo kumuomba Waziri wa Madini kushughulikia changamoto kubwa inayotokana na uwepo wa tozo nyingi zinatozwa na Halmashauri na Taasisi nyingine za Serikali kwakuwa zimekuwa zikiwarudisha nyuma kimapato wachimbaji wadogo.




WAKULIMA WAMETAKIWA KUCHANGAMKIA FURSA ZAO LA MBAAZI ILONGA 14 M-2

 
Na. Kadala Komba Dodoma

Maonesho ya mwaka huu yaliyobeba kauli mbiu isemayo "Chagua viongozi bora wa Serikali za Mitaa kwa maendeleo endelevu ya Kilimo, mifugo na uvuvi" yalianza tarehe Agosti 01, 2024 na yanategemewa kufika kilele Agosti 08, 2024.

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Wakulima wazalishaji wa Mbegu Dodoma (DASPA) Aithan Chaula Akizungumza na Waandishi wa Habari kwenye viwanja vya Nanenane Nzuguni Jijini Dodoma

"Alisema kuwa mbaazi ni zao linalofanya vizuri baada ya mvua kuisha.
"Mbaazi ni zao la jamii ya mikunde, pia ni  chanzo cha viini lishe vya protini kwa binadamu na wanyama, huvumilia ukame na chanzo cha mapato," alisema".














SIKU YA 4 YA MAONESHO YA NANENANE KITAIFA DODOMA YANAENDELEA VIWANJA VYA NZUGUNI

 Na. Kadala Komba Dodoma

Wananchi kutoka maeneo mbalimbali wametembelea Banda la @DASPA. Elimu  mbalimbali kuhusu Mbegu bora za Mbaazi,Kunde,Uwele, Karanga na Mtama (small packs) zinatolewa bila malipo hadi tarehe 10, Agosti,Mbegu hizi mazao yake yameongezewa thamani kama vile Siagi ya karanga, mafuta na karanga za kukaanga 2024.@shinenewsblog@wizalayakilimo











MATUKIO YA PICHA ZA MAONESHO YA NANENANE KITAIFA DODOMA

Na. Kadala Komba Dodoma


Maonesho ya Nanenane kitaifa yamefunguliwa rasmi  tarehe 1,Agosti, 2024 Jijini Dodoma na Waziri Mkuu wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa hadi Agosti 8,2024 ambapo Elimu  mbalimbali kuhusu Mbegu bora za Mbaazi,Kunde,Uwele, Karanga na Mtama (small packs) zinatolewa bila malipo hadi tarehe 10, Agosti, 2024.

Aithan Chaula Katibu Mtendaji wa Shirika la  Dodoma Agriculture  Seeds Production Association (DASPA),
Akiwaonesha waandishi wa Habari mafuta ya Karanga aina ya Tanzanut 2016.
   




Immaculate Chaula Akitoa maelezo kwa wakulima na wadau wanaotembelea Banda la DASPA



Wadau wakiangalia Mbegu Mbalimbali 


Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Alssem, Dk Emmanuel Monyo Akitoa Elimu ya Mbegu bora za Karanga kwa mwandishi wa Habari wa Tanzania Daima Hamida.



TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

 



*INEC YAWATAKA WATENDAJI WA UBORESHAJI KUTUNZA VIFAA*


 

Na Mwandishi wetu, Kigoma
Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imetaka watendaji wakati wa uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Mpiga Kura Mkoani Kigoma kuhakikisha wanatunza vifaa vya uandikishaji ili vikaweze kutumika maeneo mengine nchini.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs Mwambegeke wakati akifungua mafunzo ya siku mbili kwa Waratibu wa Uandikishaji wa mkoa, Maafisa Waandikishaji, Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Jimbo, Maafisa Uchaguzi, Maafisa Ugavi na Maafisa TEHAMA wa halmashauri yaliyoanza leo tarehe 20 hadi 21 Juni,2024 Mkoani Kigoma.

“Kwa kusisitiza, ni muhimu kutekeleza majukumu yenu kwa umakini katika kila eneo ikiwemo utunzaji wa vifaa vya uandikishaji hasa ikizingatiwa kuwa, vifaa hivi vimenunuliwa kwa gharama kubwa sana na vinatarajiwa kutumika katika maeneo mengine ya uandikishaji nchini,” alisema Jaji Mwambegele.

Amesema kutokuwa makini katika utunzaji wa vifaa hivi kutapelekea athari kubwa katika ukamilishaji wa zoezi hili muhimu na amewataka kuzingatia maelekezo yote yatakayotolewa na Tume ili muweze kuyafanyia kazi wakati zoezi litakapokuwa limeanza.

Aidha, Jaji Mwambegele amesema matokeo bora ya zoezi hili yanategemea uwepo wa ushirikiano mkubwa kati ya watendaji wote wa uboreshaji, serikali, vyama vya siasa na wadau wengine wa uchaguzi.

“Ninawasihi muwe na ushirikiano mzuri na wa karibu na Tume wakati wote mtakapokuwa mnatekeleza majukumu yenu na ikiwa mnahitaji ufafanuzi au maelekezo yeyote, msisite kuwasiliana na Tume,” alimema Jaji Mwambegele.

Mapema kabla ya kuanza mafunzo hayo, washiriki walikua kiapo cha kujitoa uanachama na kile cha kutunza siri mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Rose Kangwa.

Mafunzo hayo yanahusisha namna ya ujazaji wa fomu pamoja na kutumia mfumo wa kuandikisha wapiga kura (Voters Registration System - VRS) ili waweze kupata uelewa wa pamoja utakaowapa fursa ya kutumia kwa ufasaha mfumo huo pamoja na vifaa vingine vya kuandikisha wapiga kura.

“Mafunzo haya, yanawajengea umahiri wa kuwafundisha Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Kata kisha nao watatoa mafunzo hayo kwa Waendeshaji wa Vifaa vya Bayometriki na Waandishi Wasaidizi ambao ndio watahusika na uandikishaji wa wapiga kura vituoni,” alisema Jaji Mwambegele.

Aidha, Maafisa TEHAMA watapatiwa mafunzo maalum ya jinsi ya kukabiliana na changamoto mbalimbali za kiufundi (Troubleshooting) endapo zitajitokeza wakati wa zoezi la uandikishaji wa wapiga kura vituoni.

Katika hatua nyingine, Jaji Mwambegele amewaambia watendaji hao kuwa  wakati wa uboreshaji wa Daftari mawakala wa vyama vya siasa wataruhusiwa kuwepo katika vituo vya kuandikisha wapiga kura jambo ambalo litasaidia kuleta uwazi katika zoezi zima lakini pia mawakala hao watasaidia kutambua waombaji wa eneo husika hivyo kupunguza kutokea kwa vurugu zisizokuwa za lazima.

Jaji Mwambegele alitoa angalizo kwa mawakala hao kutoka vyama vya siasa kuwa  hawaruhusiwi kuwaingilia watendaji wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yao vituoni.




Tume imetangaza uzinduzi wa zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Mpiga Kura utafanyika tarehe 01 Julai, 2024 mkoani Kigoma ambapo Mgeni rasmi anataraji kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Majaliwa Kassim Majaliwa na kauli mbiu ya uboreshaji ni  “Kujiandikisha Kuwa Mpiga Kura Ni Msingi Wa Uchaguzi Bora”

MBUNGE NOLLO AMPONGEZA RAIS SAMIA KWA MIRADI MINGI YA MAENDELEO JIMBO LA BAHI

 
Na. Kadala Komba Bahi

 

Haya yamebainishwa na Mheshimiwa Mbunge wa jimbo wa Bahi Kenneth Nollo katika mkutano wa hadhara aliyofanya Mkuu wa Mkoa Dodoma Rosemary Senyemule akisikiliza kero za wananchi  kata ya Bahi mtaa wa chuma ulete.
 
 "Mhe. Nollo alisema nampongeza rais Samia Hassan kwa kutekeleza miradi mingi ya maendeleo Bahi, Tuna kila sababu ya kumshukuru  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. Samia Suluhu Hassan kwa kuleta fedha nyingi kwajili ya miradi ya maendeleo kwa wananchi wa halmashauri ya wilaya ya Bahi"

Mhe. Nollo amesema  kuwa Rais Samia amefanya kazi kubwa katika wilaya ya Bahi ambapo miradi mingi na mikubwa ya maendeleo imeonekana ikiwemo miundo mbinu ya Barabara,  shule, Afya, Elimu hizi  zote ni juhudi kubwa zinazofanywa na serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia.


Mheshimiwa Mbunge wa jimbo wa Bahi Kenneth Nollo






Mkuu wa Mkoa Dodoma Rosemary Senyemule akisikiliza kero za wananchi  kata ya Bahi mtaa wa chuma ulete.
 

Mkuu wa wilaya ya Bahi Gift Msuya

Y
Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Bahi Stewart Masima na mkuu wa wilaya ya Bahi Gift Msuya





Sosthenes Cosmas Mpandu Diwani Mpamantwa

Baadhi ya wananchi wakielezea kero zinazowakumba kwenye maeneo wanayoishi....


*TOFAUTI ZA DINI, SIASA ZISIWAGAWE WATANZANIA - DKT. BITEKO*


📌 Awataka waumini kushirikiana na Askofu Pangani

📌Serikali kuendelea kushirikiana na taasisi za dini nchini

📌 Rais Samia apewa tuzo kwa uongozi uliotukuka na kulinda amani

*Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati*

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka Watanzania kudumisha amani, mshikamano na  upendo na kamwe wasigawanywe kwa sababu yoyote.

Amesema hayo wakati akimwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ibada ya kuwekwa wakfu Askofu Robert Yondam Pangani wa Kanisa la Moravian Tanzania, Jimbo la Kusini Magharibi iliyofanyika leo Juni 2, 2024 katika viwanja vya Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji mkoani Mbeya.

“Nimefurahi kusikia wewe ni mtu mtulivu na myenyenyekevu sana upokee jambo hili kwa amani, nina imani eneo lako la mahubiri litakuwa kubwa zaidi na sisi tutaendelea kukuombea kwa Mungu ili lile aliloweka ndani yako liweze kujitokeza”, amesema Dkt. Biteko.

Ametoa wito “Waumini wenzangu huyu si malaika ni binadamu itafika wakati atachoka naomba mumtie moyo, na msiache kumuombea na kumtii inawezekana kuna anayejua kuliko yeye lakini yeye amepewa fursa ya kuwaongoza nyinyi hivyo mumtii. Pia tusibaguane kwa dini zetu au vyama vyetu vya siasa, sisi tuliokaa hapa hatujatambuana kwa makabila yetu tunatambuana kwa utanzania wetu, wakati wote muhubiri amani na mtu yeyote mwenye shida aone Tanzania ni mahali salama” .

Pia, amemsii Askofu Pangani  kuwasikiliza watangulizi wake pamoja na Askofu Kiongozi wa Kanisa la Moravian Tanzania kwa kuwa wana heshima na hekima.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Juma Homera amesema kuwa Mhe.Rais  Samia ameunganisha taasisi za dini na alichangia milioni 50 katika Kanisa la Moravian kwa ajili ya ujenzi wa ofisi mkoani Dodoma.

“ Mhe. Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati naomba utusaidie katika  mgogoro wa kiwanja mkoani Dodoma ili waweze kujenga ofisi zao, Rais Samia yuko pamoja nao na ameunganisha taasisi za dini na ukiona taasisi hizi ziko pamoja ni jitihada zake hasa hapa Mbeya”, amesema Mhe. Homera.

Naye, Askofu Robert Yondam Pangani amesema kuwa amepokea kwa heshima na  kwa unyenyekevu mkubwa nafasi aliyopewa na anaahidi kuungana na viongozi wa dini kuhakikisha amani inadumu pamoja na kuimarisha ushirikiano na Serikali.

Askofu Pangani ametaja shughuli mbalinbali zinazofanywa na Kanisa hilo la  Moravian Jimbo la Kusini Magharibi ikiwemo kuwa na miradi inayotoa ajira kwa vijana na kutunza watoto yatima sambamba na kuwasomesha katika ngazi mbalimbali za elimu kuanzia awali, shule za msingi hadi vyuo vikuu.

“Watu 1,203 wenye mahitaji maalum wameendelea kupatiwa mahitaji mbalimbali na Kanisa ikiwa ni pamoja na mafunzo kwa wajasiriamali, Kanisa pia linaungana   Serikali katika utunzaji wa mazingira ili kutunza vyanzo vyetu vya maji na kutatua changamoto ya maji kama ambavyo Rais wetu amedhamiria kumtua mama ndoo kichwani”, amesema Askofu Pangani.

Amesisitiza “Nampongeza Mhe. Rais Samia kwa mambo muhimu anayoendelea kufanya katika Taifa hili la kulinda amani pamoja na kutekeleza miradi mbalimbali ya maji, barabara na umeme ambao uko nchi nzima mijini na vijini, na mimi naahidi kuwa Kanisa litaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali na tutaendelea kuwaombea viongozi wetu”.

Mwakilishi wa Mtendaji Mkuu wa Kanisa la Moravian Duniani, Mchungaji  Erord Rupia  Simae wakati akisoma barua ya salamu kutoka kwa Rais wa Moravian Duniani, amesema kuwa wanampongeza Askofu Robert Yondam Pangani kwa kupata fursa ya kuongeza Kanisa hilo katika Jimbo la Kusini Magharibi na kuwa yeye ni mchungaji aliyepewa namba 380 tangu kuanzishwa kwa kanisa hilo duniani mwaka 1457 na pia amepewa namba 318 tangu Kanisa hilo kufanywa upya mwaka 1727.

Awali, Askofu Ezekiel Yona akimzungumzia
Askofu  Robert Yondam Pangani amesema kuwa amepewa nafasi na heshima hiyo  na Mungu hivyo akatende haki katika kutekeleza majukumu yake kwa kuwa watu wanataka kuona Askofu anayewarudisha watu kwa bwana na kuponya mioyo yao.

“Lazima tumtangulize Mungu ndani ya Ofisi ya Baba Askofu na kwa kuwa wewe umepitia ngazi nyingi katika kanisa hivyo kwa sasa unalijua kanisa vizuri zaidi ndani na nje. Ofisi yako ndio ya kujenga kanisa la kuabudu ndio na kweli”, amesisitiza Askofu Yona

Ameongeza kuwa Jimbo la Kusini Magharibi ni jimbo kubwa katika majimbo ya Kanisa la Moravian duniani na hivyo ashughulike nalo huku akiwaomba waamini wa kanisa hilo kutoa ushirikiano kwa Askofu huyo.

Pamoja na hayo, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dkt. Doto Biteko amepanda mti katika maktaba ya Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji kilichopo Mbeya ikiwa ni kumbukumbu ya ushiriki wake katika ibada hiyo.

Pia katika ibada hiyo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepewa tuzo maalum ya utumishi uliotukuka, viongozi wengine waliopewa tuzo za utumishi uliotukuka pamoja na Naibu Waziri  Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko, Spika wa Bunge na Rais wa Mabunge Duniani, Mhe. Tulia Ackson na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera.

Aidha, tendo la kumweka wakfu Askofu Robert Yondam Pangani limeongozwa na Askofu Kiongozi wa Kanisa la Moravian Tanzania, Conrad Nguvumali Sikombe pamoja na maaskofu wengine wa Kanisa hilo. Ibada hiyo pia imehudhuriwa na maaskofu kutoka nchi za Uingereza na Zambia.

Mwisho.