Subscribe Us

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

HUDUMA ZA UGANI KUPITIA MATUMIZI YA TEHAMA IMEIMARISHWA VYEMA.

 
Na Sifa Lubasi,Dodoma


MRATIBU wa Programu ya Uhimilivu wa  Mifumo ya Chakula  Nchini, Timoth Semuguluka amesema kuwa wameimarisha huduma za ugani kupitia matumizi ya Tehama ili wakulima waitumie  kupata huduma za ugani pale walipo
.Alisema hayo jana Jijini hapa kwenye maonesho ya wakulima nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni,
Mratibu huyo alisema kuwa wameimarisha mifumo ya kidigitali iliyopo na kutengeneza mifumo rafiki ili wakulima waitumie ili kupata huduma za ugani
Alisema kuwa program ya ugani inalenga kuimarisha upatikanaji huduma ya ugani kwa mazao ya chakula na biashara,kwani ni daraja kati ya teknolojia kwenda vituo vya utafiti Kisha kwaa wakulima.
Alibainisha kuwa mahitaji ya maofisa ugani ni 20,000 lakini waliopo ni 7,000 tu, mapungufu yaliyopo ni zaidi ya asilimia 50“ a'lisema
"Tunachokifanya ni kutumia mifumo ya kidigitali iliyopo na kutengeneza mifumo rafiki ili wakulima waitumie ili kupata huduma za ugani, maofisa ugani wamesajiliwa kupitia mifumo hiyo kupitia simu zao na wamekuwa wakiulizwa maswali na wakulima wamekuwa wakipata masuluhisho mbalimbali,” alisema
Alitaja maeneo mengine ya utekelezaji ni pamoja na kufanya utafiti wa teknoloijia mbalimbali za mbegu za kilimo zinazohimili mabadiliko ya tabia nchi, kuimarisha mifumo ya upatikanaji na udhibiti wa mbegu bora, kuimarisha usimamizi na utumiaji wa miundombinu ya umwagiliaji, kuandaa mfumo mpya wa usimamizi wa uendeshaji wa ghala zote za umma, kupima afya ya udongo katika vijiji vyote vya Tanzania bara  na kuandaa ramani ya afya ya udongo.
Pia alisema lengo la program hiyo ni kuongeza ufanisi, kuleta matokeo chanya ya uwekezaji wa raslimali za umma na masuala ya kisera
,“Utekelezaji wa program hii utaongeza tija na mchango wa uwekezaji wa serikali unaolenga kupunguza athari zinazotokana na uhaba wa maji kwenye mifumo ya mwagiliaji iliyopo na kupunguza upotevu wa mazao baada ya kuvuna,” alisema
Alisema kuwa program hiyo inatekeleza vipaumbele vya mpango wa kuendeleza sekta ya kilimo, sehemu ya mazao ikiwemo ununuzi wa vifaa vya kupimia udongo, ujenzi wa nyumba za maofisa ugani, ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji, ujenzi wa maabara ya kudhibiti wa ubora wa mbegu, uchimbaji wa visima kwa ajili ya umwagiliaji, ujenzi wa maabara ya tissure culture,Pia uzalishaji wa mbegu, ukarabati wa vituo vya maonesho ya nane nane.
mwisho


 


WAKULIMA WA ALIZETI KANDA YA KATI KUNUFAIKA NA UWEKEZAJI KIWANDA CHA MAINLAND

 
Na Sifa Lubasi,Dodoma


MKUU wa Wilaya ya Singida Mjini, Godwin Gondwe amesema uwekezaji mkubwa uliofanywa na kiwanda cha mafuta ya alizeti cha kampuni ya Mainland utaleta uhakika wa masoko ya alizeti ya wakulima wa mikoa ya Singida na Dodoma.
Akizungumza wakati alipotembelea banda la Kampuni hiyo kwenye maonesho ya wakulima nanenane yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma,Gondwe alisema kuwa  ujio wa kiwanda hicho Ni suluhisho la mazao ya wakulima wa alizeti.
"Hili litakuwa suluhisho kubwa la soko la wakulima wa kanda ya kati, kwani watakuwa na soko la uhakika"alisema 
Kwa upande wake Ofisa mauzo wa kiwanda hicho, Castro William alisema kuwa kiwanda hicho kipo eneo la Veyula jijini Dodoma ambapo uwekezaji huo kufikia takribani dola milioni 30 unaochukua eneo la mita za mraba 162,000.
A'lisema kuwa kuanzishwa kwa kiwanda hicho cha kuzalisha mafuta ya alizeti Dodoma kutasaidia ukuaji wa kampuni katika bara la Afrika na kuchangia uzalishaji na biashara ya bidhaa za mazao ya kilimo Afrika Mashariki.
Alisema uwekezaji huo mkubwa unalenga kuzalisha mafuta safi ya kupikia,salama na yenye afya.
"Kampuni  itazalisha aina mbili za mafuta iliwemo Merrin Farm ambapo mafuta hayo yamesafishwa na yenye ubora wa hali ya juu ,hutengenezwa kwa mbegu za alizeti safi kwa asilimia 100,"alisema 
Alisema kuwa aina nyingine ni Sunland ambayo ni mafuta ya alizeti yaliyosafishwa hutengenezwa kwa mbegu za alizeti safi, asili  kwa asilimia 100 yenye wingi wa mafuta yatokanayo na mimea na vitamin E yanasaidia lishe bora,kwa afya ya moyo.
Mwisho


 


SIDO IMETOA MIKOPO YENYE THAMANI YA MILIONI 200 KWA WAJASIRIAMALI.

 
  
Na Sifa Lubasi,Dodoma 


MENEJA wa Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) mkoa wa Dodoma Twaha Swedi amesema wametoa mkopo yenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 200 kwa kipindi cha mwaka moja kwa wajasiriamali wadogo na wachakataji wa mazao ya kilimo.
Akizungumza jana wakati wa mahojiano kwenye  maonesho ya wakulima (Nane Nane) yanayoendelea katika viwanja vya Nzuguni Jijini hapa,a'lisema kuwa kati ya waliopata mikopo hiyo wamo wazalishaji wa mvinyo na mafuta ya alizeti.
"SIDO hutoa mikopo kwa wajasiamali wadogo na  wa kati (SME's) kwa ajili ya kukuza mitaji ya miradi mbalimbali ikiwemo uwekezaji kwenye sekta za biashara,uzalishaji pamoja na uwekezaji kwenye miundombinu ya biashara,zana na vifaa vya uzalishaji,"alisema.
Alisema kuwa mwaka huu zaidi ya wakulima 100 wa zabibu na alizeti wamewezeshwa mikopo,  elimu na matumizi ya teknolojia rahisi za Kilimo na usindikaji.
"Wakulima wa zabibu, alizeti na mazao mengine ya kimkakati wamenufaika na fursa mbalimbali kwenye mikopo kupata masoko ya ndani na kimataifa,"alisema 
Alisema kuwa SIDO mkoa wa Dodoma imetoa mikopo yenye zaidi ya Sh milioni 200 katika maeneo tofauti kwa wachakataji na wafanyabiashara wadogo wadogo 
Pia alisema  katika kutekeleza dira ya Maendeleo ya mwaka 2025-2050 Shirika hilo limejipanga katika kusaidia wakulima wa zao la zabibu na mazao mengine ya kimkakati kwenye matumizi ya teknolojia rahisi, kutafuta masoko ya ndani na nje ya nchi.
" Shirika  limejipanga kutekeleza dira ya 2025-2050 kwa kusaidia wakulima wa zabibu, alizeti na mazao mengine ya kimkakati kwenye mnyororo wa thamani,"alisema
Aidha alisema wakulima na wasindikaji wamekuwa waliopata elimu ya kutambua jinsi matumizi ya teknolojia rahisi zinavyoweza kusaidia katika kuchakata mazao ya kilimo.
Pia alisema wamejipanga kuwa na ofisi kila wilaya katika mkoa wa Dodoma na wameanza na wilaya ya Kondoa .
Alisema kuwa mikakati nyingine ni kuinua vikundi cikinsu iya vijana na kimamama kwani nguvu kubwa ya uzalishaji iko kwenye maeneo hayo.
Mwisho