Subscribe Us

MAJIKO YA GESI 3,250 KUTOLEWA KWA BEI YA RUZUKU BAHI

 

Na. Kadala Komba Bahi

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza usambazaji wa majiko ya gesi (LAKE ) kwa bei ya ruzuku Wilayani Bahi Mkoani wa Dodoma ikiwa ni utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034.

Hayo yameelezwa Februari 19, 2025 Wilayani Bahi na Afisa mauzo lake gesi campan ,Kisajli Nehemia  wakati wa zoezi la uuzaji wa mitungi ya ges kwa wananchi na watumishi wa Serikali katika ofisi ya mtendaji wa  kata amesema majiko ya gesi 3250 kutolewa katika Halmashauri ya wilaya ya Bahi kwa bei ya ruzuku na zoezi hili litaendeshwa kwa siku mbili.

Kwa upande  wa Mheshimiwa Diwani kata ya Bahi Augustino Ndonu amemshukuru Rais Samia kwa kuwasogezea nishati safi na salama kwajili ya utunzaji wa mazingira na bei nafuu hii nishati ukienda dukani kununua utauziwa Sh. 45000 Helfu leo wananchi wa kata yangu wananunua kwa Sh. 20800, Tunaishukuru sana serikali ya awamu ya sita inahakikisha Watanzania wanaachana na matumizi ya nishati isiyo safi na salama kama ambavyo imeelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Habiba Omar mkazi wa kata ya Bahi  amemshukuru Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwaondolea kero wananchi wa Bahi  hususan wanawake na watoto ya kutembea umbali mrefu kusaka kuni kwa ajili ya kupikia.  wakizungumza kwa nyakati tofauti, Habiba Omar wamepongeza jitihada za Serikali za kuwasambazia nishati safi ya kupikia mbayo wamesema ni hatua nzuri ya kulinda afya zao na mazingira kwa ujumla.


Naye Miraji Bakar mkazi wa Kata ya Bahi amesema uwepo wa nishati safi ya kupikia wilayani hapo ni hatua ya kupongezwa kwani inakwenda kuimarisha afya za wananchi ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakitumia kuni kupikia.

"Tulikuwa tunasikia tuu nishati safi lakini leo tumeelimishwa na pia tumeshuhudia majiko ya gesi yaliyotolewa na Serikali kwa ruzuku," amesema .

Wananchi waliyojitokeza kununua gesi









0 Comments:

Post a Comment