Subscribe Us

This is default featured slide 1 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 2 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.

MAJIKO YA GESI 3,250 KUTOLEWA KWA BEI YA RUZUKU BAHI

 

Na. Kadala Komba Bahi

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeanza usambazaji wa majiko ya gesi (LAKE ) kwa bei ya ruzuku Wilayani Bahi Mkoani wa Dodoma ikiwa ni utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034.

Hayo yameelezwa Februari 19, 2025 Wilayani Bahi na Afisa mauzo lake gesi campan ,Kisajli Nehemia  wakati wa zoezi la uuzaji wa mitungi ya ges kwa wananchi na watumishi wa Serikali katika ofisi ya mtendaji wa  kata amesema majiko ya gesi 3250 kutolewa katika Halmashauri ya wilaya ya Bahi kwa bei ya ruzuku na zoezi hili litaendeshwa kwa siku mbili.

Kwa upande  wa Mheshimiwa Diwani kata ya Bahi Augustino Ndonu amemshukuru Rais Samia kwa kuwasogezea nishati safi na salama kwajili ya utunzaji wa mazingira na bei nafuu hii nishati ukienda dukani kununua utauziwa Sh. 45000 Helfu leo wananchi wa kata yangu wananunua kwa Sh. 20800, Tunaishukuru sana serikali ya awamu ya sita inahakikisha Watanzania wanaachana na matumizi ya nishati isiyo safi na salama kama ambavyo imeelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Habiba Omar mkazi wa kata ya Bahi  amemshukuru Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwaondolea kero wananchi wa Bahi  hususan wanawake na watoto ya kutembea umbali mrefu kusaka kuni kwa ajili ya kupikia.  wakizungumza kwa nyakati tofauti, Habiba Omar wamepongeza jitihada za Serikali za kuwasambazia nishati safi ya kupikia mbayo wamesema ni hatua nzuri ya kulinda afya zao na mazingira kwa ujumla.


Naye Miraji Bakar mkazi wa Kata ya Bahi amesema uwepo wa nishati safi ya kupikia wilayani hapo ni hatua ya kupongezwa kwani inakwenda kuimarisha afya za wananchi ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakitumia kuni kupikia.

"Tulikuwa tunasikia tuu nishati safi lakini leo tumeelimishwa na pia tumeshuhudia majiko ya gesi yaliyotolewa na Serikali kwa ruzuku," amesema .

Wananchi waliyojitokeza kununua gesi









MAAFISA ELIMU KATA,WALIMU WAKUU WAJENGEWA UWEZO BAHI

 BAHI


Kupitia Mpango wa Shule bora leo tarehe 10/02/2025 yamefanyika Mafunzo ya Uongozi na Usimamizi wa Shule Wilayani Bahi .

Mafunzo haya yana lengo la kuongeza ushirikiano baina ya Walimu Wakuu,Maafisa Elimu Kata na watumishi walio chini yao ili kuboresha utendaji kazi  na kufanikisha dhana nzima ufundishaji na ujifunzaji ili kupata matokeo bora.

Mafunzo hayo yamefunguliwa na Afisa Elimu Wilaya Ndg.Boniface Wilson na yatafanyika kwa muda wa siku tatu katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bahi kuanzia leo na kutamatika siku juma tano tarehe 13/02/2025.

Aidha,mafunzo haya yatakua endelevu kwa kuanzisha jumuiya za ujifunzaji ngazi ya Shule lengo kuu ikiwa ni kuzidi kupeana uzoefu katika usimamizi wa shule.


MAKATIBU WAKUU NA WADAU WA TANZANIA SAFARI CHANNEL WAKUTANA DODOMA

 





Kamati ya Makatibu Wakuu wa Wizara mbalimbali pamoja na wadau wa televisheni ya Tanzania Safari Channel wamekutana kuzungumzia uendeshaji wa Chaneli ya Utalii ya Tanzania Safari Channel inayomilikiwa na Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Akizungumza mara baada ya Kikao cha Makatibu Wakuu wa Wizara Wadau wa Tanzania Safari Channel kilichofanyika katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma Mwenyekiti wa Kikao hicho ambaye pia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu, Dkt. Jim Yonazi Makatibu Wakuu hao wamekutana kwa lengo la Kupokea na Kujadili taarifa ya kikao cha Wakuu wa taasisi.

Dkt. Yonazi ipo haja ya yakuendelea kuboresha chaneli hiyo ili iendelee kuwa bora na kuwavutia watazamaji wa makundi yote ndani na nje ya Nchi.

Ameongeza kuwa chaneli hiyo itakuwa yakuigwa barani Afrika ambayo itaitangaza Afrika kutokea Tanzania.

Pamoja na hayo kikao hicho kimejadili mikakati mbalimbali ya kuiwezesha chaneli hiyo kuendelea kuendesha shughuli zake za uzalishaji wa vipindi vya utalii vyenye maudhui ya ubunifu zaidi.

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa ameeleza kuwa wizara yake katika kuisimamia TBC inayo dhima ya kuhakikisha kuwa tija ya chaneli hiyo inapatikana na changamoto zote zinatatuliwa ili jamii iweze kunufaika na uwepo wa chaneli hiyo kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii.

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo kutoka Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Bi. Fatma Hamad Rajab ameishauri TBC kufanya kazi kwa ukaribu na Kamisheni ya Utalii Zanzibar ili kutangaza vivutio vingi vya utalii vilivyopo Zanzibar.